Jueni kuwa vipenzi vya Mwenyezi Mungu hawatakuwa na khofu wala hawatahuzunika.
Enyi watu! Tanabahini na mjue ya kuwa wenye kumuelekea Mwenyezi Mungu kwa Imani na ut'iifu Yeye anawapenda, na wao wanampenda. Hawana khofu ya kuhizika duniani, wala kupata adhabu ya Akhera. Wala wao hawahuzuniki kwa kukosa starehe za duniani, kwa kuwa watapata kwa Mwenyezi Mungu yaliyo makubwa na mengi kuliko hayo.
Na hao ndio walio yasadiki yote yaliyo toka kwa Mwenyezi Mungu, na wakaifuata Haki, na wakayaepuka maasi, na wakamkhofu Mwenyezi Mungu katika kila walitendalo.
Wao wana bishara njema katika maisha ya dunia na katika Akhera. Hapana mabadiliko katika maneno ya Mwenyezi Mungu. Huko ndiko kufuzu kukubwa.
Kwa wapenzi hawa wa Mwenyezi Mungu pana bishara ya kheri hapa duniani, kwa vile Mwenyezi Mungu amewaahidi kuwapa ushindi na utukufu, na Akhera itatimia ahadi ya Mwenyezi Mungu. Na ahadi ya Mwenyezi Mungu haigeuki. Na haya ndiyo waliyo bashiriwa kwayo duniani, na watayapata Akhera. Na huko ndiko kufuzu kukubwa.
Wala yasikuhuzunishe maneno yao. Hakika utukufu wote ni wa Mwenyezi Mungu. Yeye ndiye Mwenye kusikia Mwenye kujua.
Ewe Mtume! Usihuzunuke kwa wayasemayo washirikina ya kejeli, na matusi, na kukadhibisha. Wala usidhani kuwa hali yao hii itadumu. Bali ushindi ni wako, na Uislamu utatukuka, kwani utukufu wote ni wa Mwenyezi Mungu Mtukufu, na ushindi upo mkononi mwake, na Yeye atakunusuru uwashinde hao makafiri. Na Yeye Subhanahu ni Mwenye kuyasikia wanayo kuzulia, na Mwenye kuyajua wanayo dhamiria. Na Yeye atawalipa kwa hayo.
Jueni kuwa ni vya Mwenyezi Mungu vyote viliomo mbinguni na ardhinii.Na wala hawawafuati hao wanao waomba badala ya Mwenyezi Mungu kuwa ni washirika wake. Wao hawafuati ila dhana tu, na hawasemi ila uwongo.
Enyi watu! Jueni kuwa ni vya Mwenyezi Mungu peke yake vyote viliomo mbinguni na duniani, kwa kuviumba, na kuvimiliki, na kuviendesha. Na hao wanao mshirikisha Mwenyezi Mungu kwa hakika hawawafuati hao miungu ya ushirikina. Hao si chochote ila wanafuata mawazo tu, wanadhani kuwa uwezo umo katika vitu ambavyo havijifai wenyewe, la kwa manufaa wala madhara.
Yeye ndiye aliye kujaalieni usiku mpate kutulia humo, na mchana wa kuonea. Hakika katika haya zipo Ishara kwa watu wanao sikia.
Hakika huyo Mwenye kumiliki viliomo katika mbingu na ardhi, ndiye aliye kuumbieni usiku mpate kupumzika na mahangaiko ya mchana. Na amekuumbieni mchana wenye kuangaza mpate kufanya kazi na mshughulikie maslaha yenu. Hakika katika kuumbwa usiku na mchana zipo dalili zilizo wazi kwa wenye kusikia na wakapima.
Wamesema: Mwenyezi Mungu ana mwana. Subhanahu, Aliye takasika! Yeye ni Mkwasi, Mwenye Kujitosheleza. Vyote viliomo katika mbingu na katika ardhi ni vyake peke yake. Nyinyi hamna uthibitisho wowote wa haya! Mnamzulia Mwenyezi Mungu msiyo yajua?
Na ikiwa wanao abudu masanamu wamefanya ushirikina wa kuabudu mawe, na hawakumtakasa Mwenyezi Mungu kwa haki ya kumtakasa, na wakasema kuwa Allah, Mwenyezi Mungu, ana mwana, basi Mwenyezi Mungu ametakasika na hayo. Yeye hana haja ya kuwa na mwana; kwani kuwa na mwana kunaonyesha wazi kutaka kubakia ukoo wako baada ya kufa kwako. Na Mwenyezi Mungu hafi. Yeye ni Mwenye kubakia milele. Na vyote viliomo katika mbingu na viliomo katika ardhi ni vyake, vimeumbwa na vinaendeshwa na Yeye. Na nyinyi wazushi, hamna hoja yoyote wala dalili ya hayo mnayo zua! Basi msikhitalifiane juu ya Mwenyezi Mungu kwa mambo yasiyo na msingi wa hakika.
Hiyo ni starehe ya katika dunia tu, kisha marejeo yao ni kwetu. Tena tutawaonjesha adhabu kali kwa sababu ya kukufuru kwao.
Wao wana starehe hapa duniani ya kudanganyika nayo. Nayo ni chache, ikiwa itachukua muda mrefu au mfupi, ukilinganisha na hayo yanayo wangojea! Kisha marejeo yao ni kwetu, Sisi. Tutawahisabia na tutawaonjesha adhabu ya kutia uchungu kwa sababu ya ukafiri wao.
Contents of the translations can be downloaded and re-published, with the following terms and conditions:
1. No modification, addition, or deletion of the content.
2. Clearly referring to the publisher and the source (QuranEnc.com).
3. Mentioning the version number when re-publishing the translation.
4. Keeping the transcript information inside the document.
5. Notifying the source (QuranEnc.com) of any note on the translation.
6. Updating the translation according to the latest version issued from the source (QuranEnc.com).
7. Inappropriate advertisements must not be included when displaying translations of the meanings of the Noble Quran.
نتائج البحث:
API specs
Endpoints:
Sura translation
GET / https://quranenc.com/api/v1/translation/sura/{translation_key}/{sura_number} description: get the specified translation (by its translation_key) for the speicified sura (by its number)
Parameters: translation_key: (the key of the currently selected translation) sura_number: [1-114] (Sura number in the mosshaf which should be between 1 and 114)
Returns:
json object containing array of objects, each object contains the "sura", "aya", "translation" and "footnotes".
GET / https://quranenc.com/api/v1/translation/aya/{translation_key}/{sura_number}/{aya_number} description: get the specified translation (by its translation_key) for the speicified aya (by its number sura_number and aya_number)
Parameters: translation_key: (the key of the currently selected translation) sura_number: [1-114] (Sura number in the mosshaf which should be between 1 and 114) aya_number: [1-...] (Aya number in the sura)
Returns:
json object containing the "sura", "aya", "translation" and "footnotes".