Na lau kuwa Haki ingeli fuata matamanio yao, basi zingeli haribika mbingu na ardhi na waliomo ndani. Bali tumewaletea ukumbusho wao, nao wanajitenga mbali na ukumbusho wao.
Ingeli kuwa Haki inafuata matamanio yao ufisadi ungeli enea ulimwenguni, na hawa za nafsi zingeli pambana wenyewe kwa wenyewe. Lakini Sisi tumewapelekea Qur'ani ambayo inawakumbusha haki ambayo inapasa wote wajumuike juu yake. Na juu ya hivyo wao wanayapuuza hayo. "Na lau kuwa Haki ingeli fuata matamanio yao, basi zingeli haribika mbingu na ardhi na waliomo ndani. Bali tumewaletea ukumbusho wao, nao wanajitenga mbali na ukumbusho wao." Hilo neno "Haki" ni tamko lenye maana kadhaa. Huweza kuwa maana yake ni "Mwenyezi Mungu" Subhanahu wa Taa'la , mfano wa kauli yake Mtukufu: "Ametukuka Mwenyezi Mungu wa Haki". Pengine huwa maana yake ni "Qur'ani" , kwa mfano :"Hakika Sisi tumekutuma kwa Haki". Na huenda kukusudiwa "Dini yote", yaani miongoni mwake ni Qur'ani na Sunna (Hadithi) Sahihi, mfano wa kauli yake: "Na sema: Imekuja Haki na uwongo umetoweka". Na iliyo dhaahiri katika tamko la Haki hapa ni kuwa makusudio yake ni ile maana ya kwanza, yaani "Mwenyezi Mungu" Aliye takasika na kutukuka. Na kwa hivyo maana iliyo kusudiwa na Aya ni: Lau kuwa mwenendo wa Mwenyezi Mungu unafuatana na watakayo na wanayo yapendekeza makafiri mpango usingeli bakia katika hali iliyo simamia shani ya mpango wa mbingu na ardhi na wa viumbe viliomo ndani yake. Lakini Mwenyezi Mungu Mwenye hikima kuu na uwezo wa kutenda na ujuzi wake ulio enea kwa viumbe vyake na hikima yake ikadhamini kwa mpango madhubuti, na Qur'ani kusema kwa uwazi ya kwamba mbingu zina viumbe, anatuelekeza tufahamu: Kwanza kuwa Kuamini hayo kwa jumla ni yakini, tuache tafsili yake mpaka apendavyo Mwenyezi Mungu Subhanahu kuidhihirisha kwa kuambatana na kauli yake: "Tutawaonyesha Ishara zetu angani na katika nafsi zao." Pili: Anatuelekeza kwenye utafiti wa kisayansi kama tunaweza "kwani kufikilia hakika hii inatutilia nguvu Imani yetu. Na Imani ndiyo lengo muhimu katika kuelekea kwetu kwenye Ishara hizo."
Contents of the translations can be downloaded and re-published, with the following terms and conditions:
1. No modification, addition, or deletion of the content.
2. Clearly referring to the publisher and the source (QuranEnc.com).
3. Mentioning the version number when re-publishing the translation.
4. Keeping the transcript information inside the document.
5. Notifying the source (QuranEnc.com) of any note on the translation.
6. Updating the translation according to the latest version issued from the source (QuranEnc.com).
7. Inappropriate advertisements must not be included when displaying translations of the meanings of the Noble Quran.
نتائج البحث:
API specs
Endpoints:
Sura translation
GET / https://quranenc.com/api/v1/translation/sura/{translation_key}/{sura_number} description: get the specified translation (by its translation_key) for the speicified sura (by its number)
Parameters: translation_key: (the key of the currently selected translation) sura_number: [1-114] (Sura number in the mosshaf which should be between 1 and 114)
Returns:
json object containing array of objects, each object contains the "sura", "aya", "translation" and "footnotes".
GET / https://quranenc.com/api/v1/translation/aya/{translation_key}/{sura_number}/{aya_number} description: get the specified translation (by its translation_key) for the speicified aya (by its number sura_number and aya_number)
Parameters: translation_key: (the key of the currently selected translation) sura_number: [1-114] (Sura number in the mosshaf which should be between 1 and 114) aya_number: [1-...] (Aya number in the sura)
Returns:
json object containing the "sura", "aya", "translation" and "footnotes".