د قرآن کریم د معناګانو ژباړه - سواحلي ژباړه - عبد الله محمد او ناصر خمیس * - د ژباړو فهرست (لړلیک)


د معناګانو ژباړه آیت: (44) سورت: المائدة
إِنَّآ أَنزَلۡنَا ٱلتَّوۡرَىٰةَ فِيهَا هُدٗى وَنُورٞۚ يَحۡكُمُ بِهَا ٱلنَّبِيُّونَ ٱلَّذِينَ أَسۡلَمُواْ لِلَّذِينَ هَادُواْ وَٱلرَّبَّٰنِيُّونَ وَٱلۡأَحۡبَارُ بِمَا ٱسۡتُحۡفِظُواْ مِن كِتَٰبِ ٱللَّهِ وَكَانُواْ عَلَيۡهِ شُهَدَآءَۚ فَلَا تَخۡشَوُاْ ٱلنَّاسَ وَٱخۡشَوۡنِ وَلَا تَشۡتَرُواْ بِـَٔايَٰتِي ثَمَنٗا قَلِيلٗاۚ وَمَن لَّمۡ يَحۡكُم بِمَآ أَنزَلَ ٱللَّهُ فَأُوْلَٰٓئِكَ هُمُ ٱلۡكَٰفِرُونَ
Hakika tumeiteremsha Taurati. Ndani yake muna uongozi wa kumuepusha mtu na upotevu na ufafanuzi wa hukumu ambazo Mitume wamezitumia katika kuhukumu. Mitume ambao waliiandama na kuikubali hukumu ya Mwenyezi Mungu kati ya Mayahudi na wasitoke nje ya hukumu Yake wala wasiipotoshe. Pia walihukumu, kutumia sheria hiyo, wafanyi ibada wa Kiyahudi na wasomi wao ambao wanawalea watu kwa sheria za Mwenyezi Mungu. Hilo ni kwamba Manabii wao waliwaamini kwa kuwapa majukumu ya kuifikisha Taurati, kukielewa Kitabu cha Mwenyezi Mungu na kukitumia. Na wacha-Mungu na wanavyuoni walikuwa ni mashahidi ya kwamba Manabii wao walihukumu kati ya Mayahudi kwa Kitabu cha Mwenyezi Mungu. Na Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka, Anasema kuwaambia wasomi wa Kiyahudi na wanavyuoni wao, «Msiwaogope watu katika kupitisha hukumu yangu, kwani wao hawawezi kuwanufaisha nyinyi wala kuwadhuru. Lakini niogopeni, kwani mimi Ndiye Mwenye kunufaisha, Mwenye kudhuru. Wala msichukue, kwa kuacha kuhukumu kwa sheria nilizoziteremsha, badali twevu.» Kwani kuhukumu kwa ambayo hayakuteremshwa na Mwenyezi Mungu ni katika vitendo vya makafiri. Na wenye kubadilisha hukumu ya Mwenyezi Mungu Aliyoiteremsha kwenye Kitabu Chake, wakaificha, wakaikana na wakahukumu kwa isiyokuwa hiyo wakiitakidi uhalali wake na kufaa kwake, basi hao ndio makafiri.
عربي تفسیرونه:
 
د معناګانو ژباړه آیت: (44) سورت: المائدة
د سورتونو فهرست (لړلیک) د مخ نمبر
 
د قرآن کریم د معناګانو ژباړه - سواحلي ژباړه - عبد الله محمد او ناصر خمیس - د ژباړو فهرست (لړلیک)

په سواهیلي ژبه کې د قرآن کریم د معناګانو ژباړه، د ډاکټر عبدالله محمد ابوبکر او شیخ ناصر خمیس لخوا ژباړل شوی.

بندول