Check out the new design

Bản dịch ý nghĩa nội dung Qur'an - 斯瓦西里语翻译 - 阿卜杜拉·穆罕默德和纳索尔·胡麦斯 * - Mục lục các bản dịch


Ý nghĩa nội dung Câu: (44) Chương: Al-Ma-idah
إِنَّآ أَنزَلۡنَا ٱلتَّوۡرَىٰةَ فِيهَا هُدٗى وَنُورٞۚ يَحۡكُمُ بِهَا ٱلنَّبِيُّونَ ٱلَّذِينَ أَسۡلَمُواْ لِلَّذِينَ هَادُواْ وَٱلرَّبَّٰنِيُّونَ وَٱلۡأَحۡبَارُ بِمَا ٱسۡتُحۡفِظُواْ مِن كِتَٰبِ ٱللَّهِ وَكَانُواْ عَلَيۡهِ شُهَدَآءَۚ فَلَا تَخۡشَوُاْ ٱلنَّاسَ وَٱخۡشَوۡنِ وَلَا تَشۡتَرُواْ بِـَٔايَٰتِي ثَمَنٗا قَلِيلٗاۚ وَمَن لَّمۡ يَحۡكُم بِمَآ أَنزَلَ ٱللَّهُ فَأُوْلَٰٓئِكَ هُمُ ٱلۡكَٰفِرُونَ
Hakika tumeiteremsha Taurati. Ndani yake muna uongozi wa kumuepusha mtu na upotevu na ufafanuzi wa hukumu ambazo Mitume wamezitumia katika kuhukumu. Mitume ambao waliiandama na kuikubali hukumu ya Mwenyezi Mungu kati ya Mayahudi na wasitoke nje ya hukumu Yake wala wasiipotoshe. Pia walihukumu, kutumia sheria hiyo, wafanyi ibada wa Kiyahudi na wasomi wao ambao wanawalea watu kwa sheria za Mwenyezi Mungu. Hilo ni kwamba Manabii wao waliwaamini kwa kuwapa majukumu ya kuifikisha Taurati, kukielewa Kitabu cha Mwenyezi Mungu na kukitumia. Na wacha-Mungu na wanavyuoni walikuwa ni mashahidi ya kwamba Manabii wao walihukumu kati ya Mayahudi kwa Kitabu cha Mwenyezi Mungu. Na Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka, Anasema kuwaambia wasomi wa Kiyahudi na wanavyuoni wao, «Msiwaogope watu katika kupitisha hukumu yangu, kwani wao hawawezi kuwanufaisha nyinyi wala kuwadhuru. Lakini niogopeni, kwani mimi Ndiye Mwenye kunufaisha, Mwenye kudhuru. Wala msichukue, kwa kuacha kuhukumu kwa sheria nilizoziteremsha, badali twevu.» Kwani kuhukumu kwa ambayo hayakuteremshwa na Mwenyezi Mungu ni katika vitendo vya makafiri. Na wenye kubadilisha hukumu ya Mwenyezi Mungu Aliyoiteremsha kwenye Kitabu Chake, wakaificha, wakaikana na wakahukumu kwa isiyokuwa hiyo wakiitakidi uhalali wake na kufaa kwake, basi hao ndio makafiri.
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
 
Ý nghĩa nội dung Câu: (44) Chương: Al-Ma-idah
Mục lục các chương Kinh Số trang
 
Bản dịch ý nghĩa nội dung Qur'an - 斯瓦西里语翻译 - 阿卜杜拉·穆罕默德和纳索尔·胡麦斯 - Mục lục các bản dịch

阿卜杜拉·穆罕默德·艾布·比克尔和谢赫纳索尔·胡麦斯翻译

Đóng lại