Check out the new design

د قرآن کریم د معناګانو ژباړه - سواحلي ژباړه - د رواد الترجمة مرکز * - د ژباړو فهرست (لړلیک)


د معناګانو ژباړه سورت: ذاریات   آیت:

Adh-Dhariyat

وَٱلذَّٰرِيَٰتِ ذَرۡوٗا
Ninaapa kwa pepo zinazotawanya.
عربي تفسیرونه:
فَٱلۡحَٰمِلَٰتِ وِقۡرٗا
Na zinazobeba mizigo.
عربي تفسیرونه:
فَٱلۡجَٰرِيَٰتِ يُسۡرٗا
Na zinazokwenda kwa wepesi.
عربي تفسیرونه:
فَٱلۡمُقَسِّمَٰتِ أَمۡرًا
Na zinazogawanya kwa amri.
عربي تفسیرونه:
إِنَّمَا تُوعَدُونَ لَصَادِقٞ
Hakika mnayoahidiwa bila ya shaka ni kweli.
عربي تفسیرونه:
وَإِنَّ ٱلدِّينَ لَوَٰقِعٞ
Na kwa hakika malipo bila ya shaka yatatokea.
عربي تفسیرونه:
وَٱلسَّمَآءِ ذَاتِ ٱلۡحُبُكِ
Ninaapa kwa mbingu zenye njia.
عربي تفسیرونه:
إِنَّكُمۡ لَفِي قَوۡلٖ مُّخۡتَلِفٖ
Hakika nyinyi bila ya shaka mmo katika kauli inayohitalifiana.
عربي تفسیرونه:
يُؤۡفَكُ عَنۡهُ مَنۡ أُفِكَ
Anageuzwa kutokana na haki mwenye kugeuzwa.
عربي تفسیرونه:
قُتِلَ ٱلۡخَرَّٰصُونَ
Wazushi wameangamizwa.
عربي تفسیرونه:
ٱلَّذِينَ هُمۡ فِي غَمۡرَةٖ سَاهُونَ
Ambao wameghafilika katika ujinga.
عربي تفسیرونه:
يَسۡـَٔلُونَ أَيَّانَ يَوۡمُ ٱلدِّينِ
Wanauliza: 'Ni lini hiyo siku ya malipo?'
عربي تفسیرونه:
يَوۡمَ هُمۡ عَلَى ٱلنَّارِ يُفۡتَنُونَ
Hiyo ni siku watakayoadhibiwa Motoni.
عربي تفسیرونه:
ذُوقُواْ فِتۡنَتَكُمۡ هَٰذَا ٱلَّذِي كُنتُم بِهِۦ تَسۡتَعۡجِلُونَ
Onjeni adhabu yenu! Haya ndiyo mliyokuwa mkiyafanyia haraka.
عربي تفسیرونه:
إِنَّ ٱلۡمُتَّقِينَ فِي جَنَّٰتٖ وَعُيُونٍ
Hakika wacha Mungu watakuwa katika Mabustani ya mbinguni na chemchemi.
عربي تفسیرونه:
ءَاخِذِينَ مَآ ءَاتَىٰهُمۡ رَبُّهُمۡۚ إِنَّهُمۡ كَانُواْ قَبۡلَ ذَٰلِكَ مُحۡسِنِينَ
Wanapokea yale aliyowapa Mola wao Mlezi. Kwa hakika hao walikuwa kabla ya haya wakifanya mema.
عربي تفسیرونه:
كَانُواْ قَلِيلٗا مِّنَ ٱلَّيۡلِ مَا يَهۡجَعُونَ
Walikuwa wakilala kidogo tu usiku.
عربي تفسیرونه:
وَبِٱلۡأَسۡحَارِ هُمۡ يَسۡتَغۡفِرُونَ
Na kabla ya alfajiri wakiomba maghfira.
عربي تفسیرونه:
وَفِيٓ أَمۡوَٰلِهِمۡ حَقّٞ لِّلسَّآئِلِ وَٱلۡمَحۡرُومِ
Na katika mali yao ipo haki ya mwenye kuomba na asiyeomba.
عربي تفسیرونه:
وَفِي ٱلۡأَرۡضِ ءَايَٰتٞ لِّلۡمُوقِنِينَ
Na katika ardhi zipo Ishara kwa wenye yakini.
عربي تفسیرونه:
وَفِيٓ أَنفُسِكُمۡۚ أَفَلَا تُبۡصِرُونَ
Na pia katika nafsi zenu - Je, hamwoni?
عربي تفسیرونه:
وَفِي ٱلسَّمَآءِ رِزۡقُكُمۡ وَمَا تُوعَدُونَ
Na katika mbingu ziko riziki zenu na yale mnayoahidiwa.
عربي تفسیرونه:
فَوَرَبِّ ٱلسَّمَآءِ وَٱلۡأَرۡضِ إِنَّهُۥ لَحَقّٞ مِّثۡلَ مَآ أَنَّكُمۡ تَنطِقُونَ
Basi ninaapa kwa Mola Mlezi wa mbingu na ardhi, hakika haya ni kweli kama ilivyo kweli kuwa nyinyi mnasema.
عربي تفسیرونه:
هَلۡ أَتَىٰكَ حَدِيثُ ضَيۡفِ إِبۡرَٰهِيمَ ٱلۡمُكۡرَمِينَ
Je, imekufikia hadithi ya wageni wa Ibrahim wanaoheshimiwa?
عربي تفسیرونه:
إِذۡ دَخَلُواْ عَلَيۡهِ فَقَالُواْ سَلَٰمٗاۖ قَالَ سَلَٰمٞ قَوۡمٞ مُّنكَرُونَ
Walipoingia kwake na wakasema: 'Salama!' Na yeye akasema: 'Salama! Nyinyi ni watu nisiowajua.'
عربي تفسیرونه:
فَرَاغَ إِلَىٰٓ أَهۡلِهِۦ فَجَآءَ بِعِجۡلٖ سَمِينٖ
Basi akaenda kwa ahali yake na akaja na ndama aliyenona.
عربي تفسیرونه:
فَقَرَّبَهُۥٓ إِلَيۡهِمۡ قَالَ أَلَا تَأۡكُلُونَ
Akawakaribishia, akasema: 'Mbona hamli?'
عربي تفسیرونه:
فَأَوۡجَسَ مِنۡهُمۡ خِيفَةٗۖ قَالُواْ لَا تَخَفۡۖ وَبَشَّرُوهُ بِغُلَٰمٍ عَلِيمٖ
Kwa hivyo, akahisi kuwaogopa katika nafsi yake. Wakasema: 'Usiwe na hofu.' Basi wakambashiria kupata kijana mwenye elimu.
عربي تفسیرونه:
فَأَقۡبَلَتِ ٱمۡرَأَتُهُۥ فِي صَرَّةٖ فَصَكَّتۡ وَجۡهَهَا وَقَالَتۡ عَجُوزٌ عَقِيمٞ
Ndipo mkewe akawaelekea, na huku anasema na akijipiga usoni kwa mastaajabu, na kusema: Mimi ni kikongwe na tasa!
عربي تفسیرونه:
قَالُواْ كَذَٰلِكِ قَالَ رَبُّكِۖ إِنَّهُۥ هُوَ ٱلۡحَكِيمُ ٱلۡعَلِيمُ
Wakasema: Ndivyo vivyo hivyo alivyosema Mola wako Mlezi. Hakika Yeye ni Mwenye hekima, Mwenye kujua.
عربي تفسیرونه:
۞ قَالَ فَمَا خَطۡبُكُمۡ أَيُّهَا ٱلۡمُرۡسَلُونَ
Akasema: 'Basi ujumbe wenu ni nini, enyi mliotumwa?'
عربي تفسیرونه:
قَالُوٓاْ إِنَّآ أُرۡسِلۡنَآ إِلَىٰ قَوۡمٖ مُّجۡرِمِينَ
Wakasema: 'Hakika sisi tumetumwa kwa watu wakosefu.'
عربي تفسیرونه:
لِنُرۡسِلَ عَلَيۡهِمۡ حِجَارَةٗ مِّن طِينٖ
Tuwatupie mawe ya udongo.
عربي تفسیرونه:
مُّسَوَّمَةً عِندَ رَبِّكَ لِلۡمُسۡرِفِينَ
Yaliyotiwa alama kutoka kwa Mola wako Mlezi kwa ajili ya wanaopindukia mipaka.
عربي تفسیرونه:
فَأَخۡرَجۡنَا مَن كَانَ فِيهَا مِنَ ٱلۡمُؤۡمِنِينَ
Kwa hivyo tutawatoa katika hao wale walioamini.
عربي تفسیرونه:
فَمَا وَجَدۡنَا فِيهَا غَيۡرَ بَيۡتٖ مِّنَ ٱلۡمُسۡلِمِينَ
Lakini hatukupata humo ila nyumba moja tu yenye Waislamu!
عربي تفسیرونه:
وَتَرَكۡنَا فِيهَآ ءَايَةٗ لِّلَّذِينَ يَخَافُونَ ٱلۡعَذَابَ ٱلۡأَلِيمَ
Na tukaacha humo Ishara kwa ajili ya wanaoiogopa adhabu chungu.
عربي تفسیرونه:
وَفِي مُوسَىٰٓ إِذۡ أَرۡسَلۡنَٰهُ إِلَىٰ فِرۡعَوۡنَ بِسُلۡطَٰنٖ مُّبِينٖ
Na katika habari za Musa, tulipomtuma kwa Firauni na hoja wazi.
عربي تفسیرونه:
فَتَوَلَّىٰ بِرُكۡنِهِۦ وَقَالَ سَٰحِرٌ أَوۡ مَجۡنُونٞ
Lakini alipuuza kwa sababu ya nguvu zake na akasema: 'Huyu ni mchawi au mwendawazimu!'
عربي تفسیرونه:
فَأَخَذۡنَٰهُ وَجُنُودَهُۥ فَنَبَذۡنَٰهُمۡ فِي ٱلۡيَمِّ وَهُوَ مُلِيمٞ
Basi tukamkamata yeye na majeshi yake na tukawatupa baharini, na yeye ndiye wa kulaumiwa.
عربي تفسیرونه:
وَفِي عَادٍ إِذۡ أَرۡسَلۡنَا عَلَيۡهِمُ ٱلرِّيحَ ٱلۡعَقِيمَ
Na katika habari za 'Adi tulipowatumia upepo wa kukata uzazi.
عربي تفسیرونه:
مَا تَذَرُ مِن شَيۡءٍ أَتَتۡ عَلَيۡهِ إِلَّا جَعَلَتۡهُ كَٱلرَّمِيمِ
Haukuacha chochote ulichokifikia ila ulikifanya kama kilichonyambuka.
عربي تفسیرونه:
وَفِي ثَمُودَ إِذۡ قِيلَ لَهُمۡ تَمَتَّعُواْ حَتَّىٰ حِينٖ
Na katika habari za Thamudi walipoambiwa: 'Jifurahisheni kwa muda mdogo tu.'
عربي تفسیرونه:
فَعَتَوۡاْ عَنۡ أَمۡرِ رَبِّهِمۡ فَأَخَذَتۡهُمُ ٱلصَّٰعِقَةُ وَهُمۡ يَنظُرُونَ
Wakaasi amri ya Mola wao Mlezi. Basi ukawanyakua moto wa radi nao wanaona.
عربي تفسیرونه:
فَمَا ٱسۡتَطَٰعُواْ مِن قِيَامٖ وَمَا كَانُواْ مُنتَصِرِينَ
Basi hawakuweza kusimama wala hawakuwa wenye kujitetea.
عربي تفسیرونه:
وَقَوۡمَ نُوحٖ مِّن قَبۡلُۖ إِنَّهُمۡ كَانُواْ قَوۡمٗا فَٰسِقِينَ
Na kaumu ya Nuhu hapo mbele. Hakika hao walikuwa watu wapotovu.
عربي تفسیرونه:
وَٱلسَّمَآءَ بَنَيۡنَٰهَا بِأَيۡيْدٖ وَإِنَّا لَمُوسِعُونَ
Na mbingu tumezifanya kwa nguvu na uwezo na hakika Sisi bila ya shaka ndio wenye uwezo wa kuzitanua.
عربي تفسیرونه:
وَٱلۡأَرۡضَ فَرَشۡنَٰهَا فَنِعۡمَ ٱلۡمَٰهِدُونَ
Na ardhi tumeitandaza; basi watandazaji wazuri namna gani Sisi!
عربي تفسیرونه:
وَمِن كُلِّ شَيۡءٍ خَلَقۡنَا زَوۡجَيۡنِ لَعَلَّكُمۡ تَذَكَّرُونَ
Na katika kila kitu tumeumba kwa jozi ili mzingatie.
عربي تفسیرونه:
فَفِرُّوٓاْ إِلَى ٱللَّهِۖ إِنِّي لَكُم مِّنۡهُ نَذِيرٞ مُّبِينٞ
Basi kimbilieni kwa Mwenyezi Mungu, hakika mimi ni mwonyaji kwenu wa kubainisha nitokae kwake.
عربي تفسیرونه:
وَلَا تَجۡعَلُواْ مَعَ ٱللَّهِ إِلَٰهًا ءَاخَرَۖ إِنِّي لَكُم مِّنۡهُ نَذِيرٞ مُّبِينٞ
Wala msifanye kuwa kuna mungu mwengine pamoja na Mwenyezi Mungu. Hakika mimi ni mwonyaji kwenu wa kubainisha nitokae kwake.
عربي تفسیرونه:
كَذَٰلِكَ مَآ أَتَى ٱلَّذِينَ مِن قَبۡلِهِم مِّن رَّسُولٍ إِلَّا قَالُواْ سَاحِرٌ أَوۡ مَجۡنُونٌ
Basi ndio hivyo hivyo, hakuwajia kabla yao Mtume ila walisema: 'Huyu ni mchawi au mwendawazimu.'
عربي تفسیرونه:
أَتَوَاصَوۡاْ بِهِۦۚ بَلۡ هُمۡ قَوۡمٞ طَاغُونَ
Je, wameambizana kwa haya? Bali hawa ni watu waasi.
عربي تفسیرونه:
فَتَوَلَّ عَنۡهُمۡ فَمَآ أَنتَ بِمَلُومٖ
Basi waachilie mbali, nawe hulaumiwi.
عربي تفسیرونه:
وَذَكِّرۡ فَإِنَّ ٱلذِّكۡرَىٰ تَنفَعُ ٱلۡمُؤۡمِنِينَ
Na kumbusha, kwani ukumbusho huwafaa Waumini.
عربي تفسیرونه:
وَمَا خَلَقۡتُ ٱلۡجِنَّ وَٱلۡإِنسَ إِلَّا لِيَعۡبُدُونِ
Nami sikuwaumba majini na watu ila waniabudu Mimi.
عربي تفسیرونه:
مَآ أُرِيدُ مِنۡهُم مِّن رِّزۡقٖ وَمَآ أُرِيدُ أَن يُطۡعِمُونِ
Na sitaki kwao riziki, wala sitaki wanilishe.
عربي تفسیرونه:
إِنَّ ٱللَّهَ هُوَ ٱلرَّزَّاقُ ذُو ٱلۡقُوَّةِ ٱلۡمَتِينُ
Hakika Mwenyezi Mungu ndiye Mwenye kuruzuku, Mwenye nguvu, Madhubuti.
عربي تفسیرونه:
فَإِنَّ لِلَّذِينَ ظَلَمُواْ ذَنُوبٗا مِّثۡلَ ذَنُوبِ أَصۡحَٰبِهِمۡ فَلَا يَسۡتَعۡجِلُونِ
Hakika wale waliodhulumu wana fungu lao la adhabu kama fungu la wenzao. Basi wasiniharakishe.
عربي تفسیرونه:
فَوَيۡلٞ لِّلَّذِينَ كَفَرُواْ مِن يَوۡمِهِمُ ٱلَّذِي يُوعَدُونَ
Basi ole wao wale walioikanusha siku yao waliyoahidiwa.
عربي تفسیرونه:
 
د معناګانو ژباړه سورت: ذاریات
د سورتونو فهرست (لړلیک) د مخ نمبر
 
د قرآن کریم د معناګانو ژباړه - سواحلي ژباړه - د رواد الترجمة مرکز - د ژباړو فهرست (لړلیک)

دا ژباړه د مرکز رواد الترجمة ټیم لخوا د ربوہ د تبلیغ ټولنې او د اسلامي منځپانګې د خدماتو ټولنې په همکارۍ شوې.

بندول