Check out the new design

د قرآن کریم د معناګانو ژباړه - سواحلي ژباړه - د رواد الترجمة مرکز * - د ژباړو فهرست (لړلیک)


د معناګانو ژباړه سورت: قلم   آیت:

Al-Qalam

نٓۚ وَٱلۡقَلَمِ وَمَا يَسۡطُرُونَ
Nuun. Ninaapa kwa kalamu na yale wayaandikayo.[1]
[1] Herufi hii "Nuun" na herufi nyinginezo za mkato zilizo mwanzoni mwa sura mbalimbali zinaonyesha hali ya ushindi wa Qur-ani. Kwani, washirikina walipewa changamoto kwayo, lakini wakashindwa na hawakuweza kuipinga, ilhali inajumuisha herufi hizi zinazounda lugha ya Kiarabu. Kwa hivyo, kutoweza kwa Waarabu kuleta kitu kama hicho - ingawa walikuwa ndio watu wenye ufasaha zaidi - kunaonyesha kwamba Qur-ani ni ufunuo (wahyi) kutoka kwa Mwenyezi Mungu.
عربي تفسیرونه:
مَآ أَنتَ بِنِعۡمَةِ رَبِّكَ بِمَجۡنُونٖ
Kwa neema ya Mola wako Mlezi wewe si mwendawazimu.
عربي تفسیرونه:
وَإِنَّ لَكَ لَأَجۡرًا غَيۡرَ مَمۡنُونٖ
Na kwa hakika wewe una malipo yasiyokatika.
عربي تفسیرونه:
وَإِنَّكَ لَعَلَىٰ خُلُقٍ عَظِيمٖ
Na hakika wewe una tabia tukufu.
عربي تفسیرونه:
فَسَتُبۡصِرُ وَيُبۡصِرُونَ
Karibu utaona, na wao wataona.
عربي تفسیرونه:
بِأَييِّكُمُ ٱلۡمَفۡتُونُ
Ni nani kati yenu aliyepandwa na wazimu.
عربي تفسیرونه:
إِنَّ رَبَّكَ هُوَ أَعۡلَمُ بِمَن ضَلَّ عَن سَبِيلِهِۦ وَهُوَ أَعۡلَمُ بِٱلۡمُهۡتَدِينَ
Hakika Mola wako Mlezi ndiye Yeye ajuaye zaidi nani aliyeipotea Njia yake, na Yeye ndiye anayewajua zaidi walioongoka.
عربي تفسیرونه:
فَلَا تُطِعِ ٱلۡمُكَذِّبِينَ
Basi usiwatii wanaokadhibisha.
عربي تفسیرونه:
وَدُّواْ لَوۡ تُدۡهِنُ فَيُدۡهِنُونَ
Wanatamani lau ungelainisha ili nao wakulainishie.
عربي تفسیرونه:
وَلَا تُطِعۡ كُلَّ حَلَّافٖ مَّهِينٍ
Wala usimtii kila mwingi wa kuapa wa kudharauliwa.
عربي تفسیرونه:
هَمَّازٖ مَّشَّآءِۭ بِنَمِيمٖ
Mtapitapi, apitaye akifitini.
عربي تفسیرونه:
مَّنَّاعٖ لِّلۡخَيۡرِ مُعۡتَدٍ أَثِيمٍ
Mwenye kuzuia mno heri, dhalimu, mwingi wa madhambi.
عربي تفسیرونه:
عُتُلِّۭ بَعۡدَ ذَٰلِكَ زَنِيمٍ
Mkavu, na juu ya hayo, mshari, amejipachika tu.
عربي تفسیرونه:
أَن كَانَ ذَا مَالٖ وَبَنِينَ
Ati kwa kuwa ana mali na watoto!
عربي تفسیرونه:
إِذَا تُتۡلَىٰ عَلَيۡهِ ءَايَٰتُنَا قَالَ أَسَٰطِيرُ ٱلۡأَوَّلِينَ
Anaposomewa Aya zetu, husema: Hizi ni simulizi za uongo za watu wa zamani!
عربي تفسیرونه:
سَنَسِمُهُۥ عَلَى ٱلۡخُرۡطُومِ
Tutamtia kovu juu ya pua yake.
عربي تفسیرونه:
 
د معناګانو ژباړه سورت: قلم
د سورتونو فهرست (لړلیک) د مخ نمبر
 
د قرآن کریم د معناګانو ژباړه - سواحلي ژباړه - د رواد الترجمة مرکز - د ژباړو فهرست (لړلیک)

دا ژباړه د مرکز رواد الترجمة ټیم لخوا د ربوہ د تبلیغ ټولنې او د اسلامي منځپانګې د خدماتو ټولنې په همکارۍ شوې.

بندول