Check out the new design

Ibisobanuro bya qoran ntagatifu - Ibisobanuro bya Qur'an mu rurimi rw'igiswahili - Ali Muhsin Al-Barwani. * - Ishakiro ry'ibisobanuro

XML CSV Excel API
Please review the Terms and Policies

Ibisobanuro by'amagambo Isura: Al A’ala   Umurongo:

Al-A'la

سَبِّحِ ٱسۡمَ رَبِّكَ ٱلۡأَعۡلَى
Litakase jina la Mola wako Mlezi aliye juu kabisa!
Litakase jina la Mola wako Mlezi lilio tukufu na kila kitu kisicho kuwa kinaelekeana nalo.
Ibisobanuro by'icyarabu:
ٱلَّذِي خَلَقَ فَسَوَّىٰ
Aliye umba, na akaweka sawa!
Aliye umba kila kitu, na akajaalia uumbaji wote sawa sawa katika hukumu na kupangana.
Ibisobanuro by'icyarabu:
وَٱلَّذِي قَدَّرَ فَهَدَىٰ
Na ambaye amekadiria na akaongoa,.
Na akakadiria kwa kila kitu kwa mujibu wa maslaha yake, na akakiongoza.
Ibisobanuro by'icyarabu:
وَٱلَّذِيٓ أَخۡرَجَ ٱلۡمَرۡعَىٰ
Na aliye otesha malisho!
Na ambaye akatoa kwenye ardhi mimea namna mbali mbali ya kuwalisha wanyama.
Ibisobanuro by'icyarabu:
فَجَعَلَهُۥ غُثَآءً أَحۡوَىٰ
Kisha akayafanya makavu, meusi.
Na akaifanya mimea hiyo baada ya kuwa kijani imestawi, ikakauka na imekuwa myeusi!
Ibisobanuro by'icyarabu:
سَنُقۡرِئُكَ فَلَا تَنسَىٰٓ
Tutakusomesha wala hutasahau!
Ewe Muhammad! Sisi tutakujaalia uwe ni mwenye kuisoma Qur'ani kwa ufunuo kutoka kwetu, na wala hutosahau utacho kihifadhi.
Ibisobanuro by'icyarabu:
إِلَّا مَا شَآءَ ٱللَّهُۚ إِنَّهُۥ يَعۡلَمُ ٱلۡجَهۡرَ وَمَا يَخۡفَىٰ
Ila akipenda Mwenyezi Mungu. Hakika Yeye anayajua yaliyo dhaahiri na yaliyo fichikana.
Isipo kuwa anacho taka Mwenyezi Mungu ukisahau, kwani hakika Yeye Mtukufu anayajua wanayo yadhihirisha waja wake na wanayo yaficha, ikiwa maneno au vitendo.
Ibisobanuro by'icyarabu:
وَنُيَسِّرُكَ لِلۡيُسۡرَىٰ
Na tutakusahilishia yawe mepesi.
Na tutakuwezesha kupita njia ya kufikilia kwa wepesi mambo yako yote.
Ibisobanuro by'icyarabu:
فَذَكِّرۡ إِن نَّفَعَتِ ٱلذِّكۡرَىٰ
Basi kumbusha, kama kukumbusha kunafaa.
Basi wakumbushe watu ikiwa kukumbusha kutaleta manufaa, kwani inavyo faa ndio kuwanafiisha.
Ibisobanuro by'icyarabu:
سَيَذَّكَّرُ مَن يَخۡشَىٰ
Atakumbuka mwenye kuogopa.
Watanafiika kwa ukumbusho wako wanao mwogopa Mwenyezi Mungu.
Ibisobanuro by'icyarabu:
 
Ibisobanuro by'amagambo Isura: Al A’ala
Urutonde rw'amasura numero y'urupapuro
 
Ibisobanuro bya qoran ntagatifu - Ibisobanuro bya Qur'an mu rurimi rw'igiswahili - Ali Muhsin Al-Barwani. - Ishakiro ry'ibisobanuro

byasobanuwe na Ali Muhsen Al-Barwaniy.

Gufunga