Siku ambayo kila nafsi itakuta mema iliyo yafanya yamehudhurishwa, na pia ubaya ilio ufanya. Itapenda nafsi lau kungekuwako masafa marefu baina ya ubaya huo na yeye. Na Mwenyezi Mungu anakuhadharisheni naye. Na Mwenyezi Mungu ni Mpole kwa waja wake.
Basi na watahadhari wale wanao ikhalifu amri yake na Siku ambayo kila mtu atakuta vitendo vyake vya kheri hata kilicho kichache kimeletwa hadharani; na pia uovu wake alio utenda ambao angetamani lau kuwa uko mbali, mwisho wa umbali, hata asiuone kwa kuuchukia na kukhofu kutumbukia katika adhabu zake. Na Mwenyezi Mungu anakuhadharisheni na adhabu zake pindi mkitokana na ulinzi wake na utawala wake, ambao ni upole na rehema kwa waja wake.
Sema: Ikiwa nyinyi mnampenda Mwenyezi Mungu basi nifuateni mimi, Mwenyezi Mungu atakupendeni na atakufutieni madhambi yenu. Na Mwenyezi Mungu ni Mwenye kufuta madhambi na Mwenye kurehemu.
Sema: Ikiwa nyinyi ni wakweli katika madai yenu, kuwa mnampenda Mwenyezi Mungu na mnataka Mwenyezi Mungu akupendeni, basi nifuateni mimi kwa ninayo kuamrisheni na ninayo kukatazeni. Kwani mimi nimetumwa na Mwenyezi Mungu. Basi Mwenyezi Mungu atakupendeni kwa hivyo, na atakulipeni kwa kukufanyieni hisani na kusamehe makosa yenu. Na Mwenyezi Mungu ni mwingi wa kuwasamehe na kuwarehemu waja wake.
Sema: Mt'iini Mwenyezi Mungu na Mtume. Na wakigeuka basi Mwenyezi Mungu hawapendi makafiri.
Sema: Mt'iini Mwenyezi Mungu na Mtume. Na wakikukataa basi hao ni makafiri, wamemkataa Mwenyezi Mungu na Mtume wake. Na Mwenyezi Mungu hawapendi makafiri.
Hakika Mwenyezi Mungu alimteuwa Adam na Nuhu na ukoo wa Ibrahim na ukoo wa Imran juu ya walimwengu wote.
Kama Mwenyezi Mungu alivyo mteua Muhammad afikishe ujumbe wake, na akajaalia kumfuata Muhammad ni njia ya kufikia mapenzi ya Mwenyezi Mungu na kupata maghfira na rehema yake, kadhaalika ametaja Mwenyezi Mungu kuwa Yeye alimteua Adam na akamjaalia ni katika wateule wa walimwengu. Pia alimteua Nuhu kwa kumpa ujumbe, na akamteua Ibrahim na ukoo wake, nao ni Ismail na Is-haq na Manabii wengine kutokana na wana wao hao. Miongoni mwao ni Musa a.s. Akawakhitari ukoo wa Imran, na miongoni mwao akamkhitari Isa na mama yake. Alimfanya Isa awe ni Mtume kwa Wana wa Israili, na Maryam akamfanya awe ni mama wa Isa bila ya baba.
Ni wazao wao kwa wao; na Mwenyezi Mungu ni Mwenye kusikia na Mwenye kujua.
Amewakhitari hao ukoo ulio safi, wakirithiana usafi na fadhila na kheri. Na Mwenyezi Mungu ni Mwenye kusikia maneno ya waja wake kwa vitendo vyao na vinavyo fichwa vifuani mwao.
Alipo sema mke wa Imran: Mola wangu Mlezi! Nimekuwekea nadhiri kilichomo tumboni mwangu kuwa wakfu; basi nikubalie. Hakika Wewe ndiye Mwenye kusikia na Mwenye kujua.
Ewe Nabii! Taja hali ya mke wa Imran alipo weka nadhiri wakati alipo kuwa na mimba, kuwa mwana aliomo tumboni mwake awe ni wa kumtumikia Mwenyezi Mungu tu na kukhudumia nyumba yake. Alisema: Ewe Mola! Hakika mimi nimekuwekea nadhiri huyu aliyomo tumboni mwangu awe ni wa kukhudumia nyumba yako, basi nikubalie haya. Hakika Wewe ni Mwenye kusikia kila kauli, na Mwenye kujua kila hali.
Basi alipo mzaa alisema: Mola wangu Mlezi! Nimemzaa mwanamke - na Mwenyezi Mungu anajua sana aliye mzaa - Na mwanamume si sawa na mwanamke. Na mimi nimemwita Maryamu. Nami namkinga kwako, yeye na uzao wake, uwalinde na Shet'ani aliye laaniwa.
Alipo jifungua mimba akasema kwa kujiudhuru kumwambia Mola wake Mlezi: Niliye mzaa ni mwanamke - na Mwenyezi Mungu anajua vilivyo alicho kizaa, na kuwa mwana wenyewe ni mwanamke ni bora kuliko alivyo taka mama kuwa awe mwanamume. Akasema yule mama: Mimi nimemwita Maryamu, na mimi nakuomba umlinde yeye na ukoo wake na uharibifu wa Shetani maluuni.
Tena Mola wake Mlezi akampokea kwa mapokeo mema na akamkuza makuzo mema, na akamfanya Zakariya awe mlezi wake. Kila mara Zakariya alipo ingia chumbani kwake alimkuta na vyakula. Basi alimwambia: Ewe Maryamu! Unavipata wapi hivi? Naye akasema: Hivi vinatoka kwa Mwenyezi Mungu; na Mwenyezi Mungu humruzuku amtakaye bila ya hisabu.
Mwenyezi Mungu alimpokea Maryamu kuwa ni nadhiri aliyo iweka mama yake, akamwitikia maombi yake, akamkuza makuzo mema, na akamlea katika kheri yake, Mola Mlezi, huku akimruzuku na kumshughulikia kwa malezi mazuri ya kumpa nguvu mwili wake na roho yake. Mwenyezi Mungu akamkabidhi Zakariya a.s. awe mlezi wake. Zakariya kila akiingia chumbani, alipo kuwa Maryamu anaabudu, akikuta chakula wasicho kizowea wakati ule. Zakariya akasema kwa kustaajabu: Ewe Maryamu! Umepata wapi riziki hii? Naye akamjibu: Hichi ni katika fadhila za Mwenyezi Mungu. Ni shani yake kumruzuku mja wake amtakaye riziki nyingi bila ya hisabu au kipimo.
Contents of the translations can be downloaded and re-published, with the following terms and conditions:
1. No modification, addition, or deletion of the content.
2. Clearly referring to the publisher and the source (QuranEnc.com).
3. Mentioning the version number when re-publishing the translation.
4. Keeping the transcript information inside the document.
5. Notifying the source (QuranEnc.com) of any note on the translation.
6. Updating the translation according to the latest version issued from the source (QuranEnc.com).
7. Inappropriate advertisements must not be included when displaying translations of the meanings of the Noble Quran.
සෙවීමේ ප්රතිඵල:
API specs
Endpoints:
Sura translation
GET / https://quranenc.com/api/v1/translation/sura/{translation_key}/{sura_number} description: get the specified translation (by its translation_key) for the speicified sura (by its number)
Parameters: translation_key: (the key of the currently selected translation) sura_number: [1-114] (Sura number in the mosshaf which should be between 1 and 114)
Returns:
json object containing array of objects, each object contains the "sura", "aya", "translation" and "footnotes".
GET / https://quranenc.com/api/v1/translation/aya/{translation_key}/{sura_number}/{aya_number} description: get the specified translation (by its translation_key) for the speicified aya (by its number sura_number and aya_number)
Parameters: translation_key: (the key of the currently selected translation) sura_number: [1-114] (Sura number in the mosshaf which should be between 1 and 114) aya_number: [1-...] (Aya number in the sura)
Returns:
json object containing the "sura", "aya", "translation" and "footnotes".