Check out the new design

Përkthimi i kuptimeve të Kuranit Fisnik - Përkthimi suahilisht - Abdullah Muhammed dhe Nasir Khamis * - Përmbajtja e përkthimeve


Përkthimi i kuptimeve Surja: El Enbija   Ajeti:
وَمِنَ ٱلشَّيَٰطِينِ مَن يَغُوصُونَ لَهُۥ وَيَعۡمَلُونَ عَمَلٗا دُونَ ذَٰلِكَۖ وَكُنَّا لَهُمۡ حَٰفِظِينَ
Na tulimdhalilishia Sulaymān, kati ya mashetani, mashetani ambao alikuwa akiwatuma kufanya yale ambayo wasiokuwa wao wanashindwa nayo, walikuwa wakipiga mbizi baharini wakimtolea lulu na johari, na walikuwa wakimtengenezea vitu avitakavayo kwao, hawakuwa wakiweza kukataa kufanya ayatakayo kutoka kwao. Mwenyezi Mungu Amewahifadhi kwa nguvu Zake na enzi Yake , kutakata na sifa za upungufu ni Kwake na kutukuka ni Kwake.
Tefsiret në gjuhën arabe:
۞ وَأَيُّوبَ إِذۡ نَادَىٰ رَبَّهُۥٓ أَنِّي مَسَّنِيَ ٱلضُّرُّ وَأَنتَ أَرۡحَمُ ٱلرَّٰحِمِينَ
Na kumbuka, ewe Mtume, mja wetu Ayyūb, tulipomtahini kwa madhara na ugonjwa mkubwa mwilini mwake, na akakosa watu wake, mali yake na watoto wake, akasubiri kwa kutaka thawabu, na akamlingania Mola wake, Aliyetukuka na kushinda, kwa kumuomba, «Mimi nimepatikana na madhara, na wewe Ndiye Mwenye huruma kuliko wenye huruma, basi niepushie nayo!»
Tefsiret në gjuhën arabe:
فَٱسۡتَجَبۡنَا لَهُۥ فَكَشَفۡنَا مَا بِهِۦ مِن ضُرّٖۖ وَءَاتَيۡنَٰهُ أَهۡلَهُۥ وَمِثۡلَهُم مَّعَهُمۡ رَحۡمَةٗ مِّنۡ عِندِنَا وَذِكۡرَىٰ لِلۡعَٰبِدِينَ
Hapo tukayakubali maombi yake, tukamuondolea matatizo na tukamrudishia alichokikosa miongoni mwa wake, watoto na mali mara mbili zaidi. Tulimfanyia hayo kwa huruma itokayo kwetu na ili awe ni kiolezo kwa kila mwenye kuvumilia mitihani, mwenye matumaini ya kupata rehema ya Mola wake na mwenye kumuabudu.
Tefsiret në gjuhën arabe:
وَإِسۡمَٰعِيلَ وَإِدۡرِيسَ وَذَا ٱلۡكِفۡلِۖ كُلّٞ مِّنَ ٱلصَّٰبِرِينَ
Na kumbuka Ismā'īl, Idrīs na Dhulkifl. Wote hao ni miongoni mwa wavumilivu katika kumtii Mwenyezi Mungu, kutakata na sifa za upungufu ni Kwake na kutukuka ni Kwake, katika kujiepusha na kumuasi na juu ya makadirio Yake, na kwa hivyo walistahiki kutajwa kwa sifa nzuri.
Tefsiret në gjuhën arabe:
وَأَدۡخَلۡنَٰهُمۡ فِي رَحۡمَتِنَآۖ إِنَّهُم مِّنَ ٱلصَّٰلِحِينَ
Na tukawatia ndani ya rehema yetu. Kwa hakika wao ni miongoni mwa wale ambao imetengenea ndani yao na nje yao, wakamtii Mwenyezi Mungu na wakafanya matendo yanayolingana na maamrisho Yake.
Tefsiret në gjuhën arabe:
وَذَا ٱلنُّونِ إِذ ذَّهَبَ مُغَٰضِبٗا فَظَنَّ أَن لَّن نَّقۡدِرَ عَلَيۡهِ فَنَادَىٰ فِي ٱلظُّلُمَٰتِ أَن لَّآ إِلَٰهَ إِلَّآ أَنتَ سُبۡحَٰنَكَ إِنِّي كُنتُ مِنَ ٱلظَّٰلِمِينَ
Na kumbuka kisa cha mtu wa chewa, naye ni Yūnus mwana wa Mattā, amani imshukie, Mwenyezi Mungu Alimtumiliza kwa watu wake, akawalingania wasimuamini, akawaonya kuwa wataadhibiwa, lakikni hawakurudi nyuma. Na asiwavumilie kama vile Mwenyezi Mungu Alivyomuamrisha na akaondoka kutoka kwao akiwa na hasira juu yao, akiwa amebanwa na kifua kwa kuasi kwao. Na akadhani kwamba Mwenyezi Mungu Hatampa dhiki na kumuadhibu kwa ukiukaji huu. Mwenyezi Mungu Akamtahini kwa dhiki nyingi na kifungo na akamezwa na tewa baharini, na akamlingania Mola wake kwa kumuomba katika magiza ya usiku, bahari na tumbo la tewa hali ya kutubia na kukubali ukiukaji wake kwa kuacha kuwavumilia watu wake, huku akisema, «Hapana muabudiwa kwa haki isipokuwa wewe! Kutakasika na sifa za upungufu ni kwako! kwa hakika mimi nimekuwa miongoni mwa wenye kudhulumu!»
Tefsiret në gjuhën arabe:
فَٱسۡتَجَبۡنَا لَهُۥ وَنَجَّيۡنَٰهُ مِنَ ٱلۡغَمِّۚ وَكَذَٰلِكَ نُـۨجِي ٱلۡمُؤۡمِنِينَ
Basi hapo tukamkubalia maombi yake na tukamuondolea unguliko la shida. Na hivyo ndivyo tunavyowaokoa wakweli wenye kuzifuata sheria zetu kivitendo.
Tefsiret në gjuhën arabe:
وَزَكَرِيَّآ إِذۡ نَادَىٰ رَبَّهُۥ رَبِّ لَا تَذَرۡنِي فَرۡدٗا وَأَنتَ خَيۡرُ ٱلۡوَٰرِثِينَ
Na kumbuka, ewe Mtume, kisa cha mja wa Mwenyezi Mungu Zakariyya alipomuomba Mola wake Amtunukie wana, wakati umri wake ulipokuwa mkubwa, kwa kusema, «Mola wangu! Usiniache pweke ni siwe na mwana! Basi nitunuku mrithi wa kusimamia mambo ya Dini kwa watu baada yangu mimi, na wewe Ndiye bora wa wenye kusalia na bora wa wenye kusimamia mambo yangu baada yangu kwa uzuri!»
Tefsiret në gjuhën arabe:
فَٱسۡتَجَبۡنَا لَهُۥ وَوَهَبۡنَا لَهُۥ يَحۡيَىٰ وَأَصۡلَحۡنَا لَهُۥ زَوۡجَهُۥٓۚ إِنَّهُمۡ كَانُواْ يُسَٰرِعُونَ فِي ٱلۡخَيۡرَٰتِ وَيَدۡعُونَنَا رَغَبٗا وَرَهَبٗاۖ وَكَانُواْ لَنَا خَٰشِعِينَ
Tukamkubalia maombi yake na tukamtunuku yeye, akiwa katika hali ya uzee, mwanawe Yaḥyā, na tukamfanya mke wake ni mwema wa tabia na ni mwenye kufaa kushika mimba na kuzaa baada ya kuwa tasa. Kwa kweli, wao walikuwa wakiikimbilia kila kheri, na wakituomba wakitumai kupata mazuri yaliyoko kwetu wakiogopa mateso yetu na walikuwa wadhalilifu na wanyonge kwetu.
Tefsiret në gjuhën arabe:
 
Përkthimi i kuptimeve Surja: El Enbija
Përmbajtja e sureve Numri i faqes
 
Përkthimi i kuptimeve të Kuranit Fisnik - Përkthimi suahilisht - Abdullah Muhammed dhe Nasir Khamis - Përmbajtja e përkthimeve

Përkthyer nga Dr. Abdullah Muhammed Abu Bekr dhe Shejh Nasir Khamis.

Mbyll