Check out the new design

Përkthimi i kuptimeve të Kuranit Fisnik - Përkthimi suahilisht - Abdullah Muhammed dhe Nasir Khamis * - Përmbajtja e përkthimeve


Përkthimi i kuptimeve Surja: El Ahzab   Ajeti:
وَإِذۡ أَخَذۡنَا مِنَ ٱلنَّبِيِّـۧنَ مِيثَٰقَهُمۡ وَمِنكَ وَمِن نُّوحٖ وَإِبۡرَٰهِيمَ وَمُوسَىٰ وَعِيسَى ٱبۡنِ مَرۡيَمَۖ وَأَخَذۡنَا مِنۡهُم مِّيثَٰقًا غَلِيظٗا
Na kumbuka utaje, ewe Nabii, tulipochukua kutoka kwa Manabii ahadi ya mkazo kutekeleza ujumbe, na tukachukua ahadi kutoka kwako, na kutoka kwa Nūḥ, Ibrāhīm, Mūsā na Īsā mwana wa Maryam (nao ndio Mitume wenye nyoyo thabiti, katika kauli iliyo mashuhuri), na tukachukua kutoka kwao ahadi ya mkazo ya kufikisha ujumbe na kutekeleza amana na kuaminiana wao kwa wao.
Tefsiret në gjuhën arabe:
لِّيَسۡـَٔلَ ٱلصَّٰدِقِينَ عَن صِدۡقِهِمۡۚ وَأَعَدَّ لِلۡكَٰفِرِينَ عَذَابًا أَلِيمٗا
Mwenyezi Mungu Alichukua ahadi hiyo kutoka kwa Mitume hao, ili Apate kuwauliza waliotumwa vile walivyojibiwa na ummah wao, ili Mwenyezi Mungu Awalipe Pepo wenye kuamini. Na Amewaandalia makafiri, Siku ya Kiyama, adhabu kali ndani ya Jahanamu.
Tefsiret në gjuhën arabe:
يَٰٓأَيُّهَا ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ ٱذۡكُرُواْ نِعۡمَةَ ٱللَّهِ عَلَيۡكُمۡ إِذۡ جَآءَتۡكُمۡ جُنُودٞ فَأَرۡسَلۡنَا عَلَيۡهِمۡ رِيحٗا وَجُنُودٗا لَّمۡ تَرَوۡهَاۚ وَكَانَ ٱللَّهُ بِمَا تَعۡمَلُونَ بَصِيرًا
Enyi Waumini! Ikumbukeni neema ya Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka, Aliyowaneemesha nyinyi katika Madina siku ya vita vya Makundi (Aḥzāb), navyo ndivyo vita vya Shimo (Khandaq), walipojikusanya dhidi yenu washirikina kutoka nje ya Madina, na Mayahudi na wanafiki wakiwa ndani ya Madina na pambizoni mwake, wakawaviringa nyinyi, hapo tukayatumia yale makundi upepo mkali uliong’oa mahema yao na kuvirusha vyungu vyao, na tukawatumia Malaika kutoka mbinguni msiowaona, hapo basi nyoyo zao zikaingia kicho. Na Mwenyezi Mungu ni Mwenye kuyaona mnayoyatenda, hakuna chochote kinachofichamana kwake katika hayo.
Tefsiret në gjuhën arabe:
إِذۡ جَآءُوكُم مِّن فَوۡقِكُمۡ وَمِنۡ أَسۡفَلَ مِنكُمۡ وَإِذۡ زَاغَتِ ٱلۡأَبۡصَٰرُ وَبَلَغَتِ ٱلۡقُلُوبُ ٱلۡحَنَاجِرَ وَتَظُنُّونَ بِٱللَّهِ ٱلظُّنُونَا۠
Kumbukeni pindi walipowajia kwa juu yenu kutoka sehemu ya juu ya bonde lilioko upande wa mashariki na kwa chini yenu kutoka sehemu ya kati ya bonde lilioko upande wa magharibi, na pindi macho yalipokodoka kwa kuduwaa sana na kushutuka, na nyoyo zikafika kwenye magorombo (ya koo) kwa kitisho kikali, na wanafiki wakajawa na ukataji tamaa na uvumi ukazidi, na mkawa mnamdhania Mwenyezi Mungu dhana mbaya ya kuwa Yeye Hataiokoa Dini Yake na Hatalikuza jina Lake.
Tefsiret në gjuhën arabe:
هُنَالِكَ ٱبۡتُلِيَ ٱلۡمُؤۡمِنُونَ وَزُلۡزِلُواْ زِلۡزَالٗا شَدِيدٗا
Katika msimamo huo mgumu, Imani za Waumini zilijaribiwa na watu wakakaguliwa, na akajulikana mnafiki kwa kutengwa na Muumini, na wakasukikasukika msukosuko mkali kwa kuingiwa na kicho na babaiko, ili Imani yao ibainike na yakini yao izidi
Tefsiret në gjuhën arabe:
وَإِذۡ يَقُولُ ٱلۡمُنَٰفِقُونَ وَٱلَّذِينَ فِي قُلُوبِهِم مَّرَضٞ مَّا وَعَدَنَا ٱللَّهُ وَرَسُولُهُۥٓ إِلَّا غُرُورٗا
Na pindi waliposema wanafiki na wale ambao ndani ya nyoyo zao mna shaka, nao ni wale madhaifu wa Imani, «Ahadi ya Mwenyezi Mungu Aliyotuahidi ya kupata ushindi na utulivu, haikuwa isipokuwa ni maneno ya urongo na udanganyifu, basi msimuamini.»
Tefsiret në gjuhën arabe:
وَإِذۡ قَالَت طَّآئِفَةٞ مِّنۡهُمۡ يَٰٓأَهۡلَ يَثۡرِبَ لَا مُقَامَ لَكُمۡ فَٱرۡجِعُواْۚ وَيَسۡتَـٔۡذِنُ فَرِيقٞ مِّنۡهُمُ ٱلنَّبِيَّ يَقُولُونَ إِنَّ بُيُوتَنَا عَوۡرَةٞ وَمَا هِيَ بِعَوۡرَةٍۖ إِن يُرِيدُونَ إِلَّا فِرَارٗا
Na kumbuka, ewe Nabii, neno la kipote cha wanafiki wakiwaita Waumini miongoni mwa watu wa Madina, «Enyi watu wa Yathrib (nalo ni jina la zamani la Madina), ‘Msikae kwenye vita ambavyo mtashindwa, rudini majumbani mwenu ndani ya Madina’» Na pote lingine la wanafiki linamuomba ruhusa Mtume, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, kurudi majumbani mwao kwa kisingizio kuwa hayako imara, na kwa hivyo wanayaogopea, na ukweli ni kwamba hayo si hivyo, na lengo lao halikuwa isipokuwa ni kukimbia vita.
Tefsiret në gjuhën arabe:
وَلَوۡ دُخِلَتۡ عَلَيۡهِم مِّنۡ أَقۡطَارِهَا ثُمَّ سُئِلُواْ ٱلۡفِتۡنَةَ لَأٓتَوۡهَا وَمَا تَلَبَّثُواْ بِهَآ إِلَّا يَسِيرٗا
Na lau jeshi la makundi lingaliingia Madina kupitia pambizoni mwake, kisha wakatakwa hawa wanafiki wamshirikishe Mwenyezi Mungu na warudi kutoka kwenye Uislamu, wangalilikubali hilo kwa haraka, na hawangalichelewesha kurudi kwenye ushirikina isipokuwa kwa muda mchache.
Tefsiret në gjuhën arabe:
وَلَقَدۡ كَانُواْ عَٰهَدُواْ ٱللَّهَ مِن قَبۡلُ لَا يُوَلُّونَ ٱلۡأَدۡبَٰرَۚ وَكَانَ عَهۡدُ ٱللَّهِ مَسۡـُٔولٗا
Na kwa hakika, wanafiki hawa walimuahidi Mwenyezi Mungu kupitia kwa Mtume Wake kabla ya vita vya Shimo (Khandaq) kuwa hawatakimbia watakapohudhuria vita na hawatachelewa watakapoitwa kwenda Jihadi, lakini wao walihini ahadi yao. Na Mwenyezi Mungu Atawahesabu kwa hilo na Atawauliza kuhusu ahadi hiyo. Hakika ahadi ya Mwenyezi Mungu itaulizwa na itahesabiwa.
Tefsiret në gjuhën arabe:
 
Përkthimi i kuptimeve Surja: El Ahzab
Përmbajtja e sureve Numri i faqes
 
Përkthimi i kuptimeve të Kuranit Fisnik - Përkthimi suahilisht - Abdullah Muhammed dhe Nasir Khamis - Përmbajtja e përkthimeve

Përkthyer nga Dr. Abdullah Muhammed Abu Bekr dhe Shejh Nasir Khamis.

Mbyll