Përkthimi i kuptimeve të Kuranit Fisnik - Përkthimi suahilisht - Abdullah Muhammed dhe Nasir Khamis * - Përmbajtja e përkthimeve


Përkthimi i kuptimeve Ajeti: (26) Surja: Suretu El Fet-h
إِذۡ جَعَلَ ٱلَّذِينَ كَفَرُواْ فِي قُلُوبِهِمُ ٱلۡحَمِيَّةَ حَمِيَّةَ ٱلۡجَٰهِلِيَّةِ فَأَنزَلَ ٱللَّهُ سَكِينَتَهُۥ عَلَىٰ رَسُولِهِۦ وَعَلَى ٱلۡمُؤۡمِنِينَ وَأَلۡزَمَهُمۡ كَلِمَةَ ٱلتَّقۡوَىٰ وَكَانُوٓاْ أَحَقَّ بِهَا وَأَهۡلَهَاۚ وَكَانَ ٱللَّهُ بِكُلِّ شَيۡءٍ عَلِيمٗا
Pindi wale waliokanusha walipoingiza ndani ya nyoyo zao ghera, ghera za watu wa zama za ujinga, ili wasikubali utume wa Muhammad, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, na miongoni mwa hayo ni kule kukataa kwao kwandika «Bi ism Allāh al-Raḥmān al-Raḥīm» katika mapatano ya Ḥudaybiyah, na wakakataa kuandika, «Haya ndiyo yale aliyoyapitisha Muhammad, Mtume wa Mwenyezi Mungu.» Na Mwenyezi Mungu Akamteremshia utulivu Mtume Wake na Waumini pamoja na yeye, Akawathibitishia neno «Lā ilāha illā Allāh» ambalo ndio kichwa cha ya kila uchamungu. Na Mtume, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, na Waumini pamoja na yeye ndio wanaostahiki zaidi neno la uchamungu kuliko washirikina. Na hivyo ndivyo walivyokuwa, walistahiki neno hili na sio washirikina. Na Mwenyezi Mungu ni Mwingi wa ujuzi wa kila kitu, hakuna kitu chochote kinachofichamana Kwake.
Tefsiret në gjuhën arabe:
 
Përkthimi i kuptimeve Ajeti: (26) Surja: Suretu El Fet-h
Përmbajtja e sureve Numri i faqes
 
Përkthimi i kuptimeve të Kuranit Fisnik - Përkthimi suahilisht - Abdullah Muhammed dhe Nasir Khamis - Përmbajtja e përkthimeve

Përkthimi i kuptimeve të Kuranit në suahilishte - Përkthyer nga Abdullah Muhammed dhe Nasir Khamis - Botuar nga Kompleksi Mbreti Fehd për Botimin e Mushafit Fisnik në Medinë. Viti i botimit: 1435 h.

Mbyll