Përkthimi i kuptimeve të Kuranit Fisnik - Përkthimi suahilisht - Abdullah Muhammed dhe Nasir Khamis * - Përmbajtja e përkthimeve


Përkthimi i kuptimeve Ajeti: (2) Surja: Suretu El Hashr
هُوَ ٱلَّذِيٓ أَخۡرَجَ ٱلَّذِينَ كَفَرُواْ مِنۡ أَهۡلِ ٱلۡكِتَٰبِ مِن دِيَٰرِهِمۡ لِأَوَّلِ ٱلۡحَشۡرِۚ مَا ظَنَنتُمۡ أَن يَخۡرُجُواْۖ وَظَنُّوٓاْ أَنَّهُم مَّانِعَتُهُمۡ حُصُونُهُم مِّنَ ٱللَّهِ فَأَتَىٰهُمُ ٱللَّهُ مِنۡ حَيۡثُ لَمۡ يَحۡتَسِبُواْۖ وَقَذَفَ فِي قُلُوبِهِمُ ٱلرُّعۡبَۚ يُخۡرِبُونَ بُيُوتَهُم بِأَيۡدِيهِمۡ وَأَيۡدِي ٱلۡمُؤۡمِنِينَ فَٱعۡتَبِرُواْ يَٰٓأُوْلِي ٱلۡأَبۡصَٰرِ
Yeye, kutakasika ni Kwake, Ndiye Aliyewatoa wale walioukanusha unabii wa Muhammad, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, miongoni mwa watu waliopewa Kitabu, nao ni Mayahudi wa ukoo wa Banū al Nadīr, kutoka majumbani mwao ambayo wakiwa humo walikuwa ni majirani na Waislamu pambizoni mwa Madina. Huko kulikuwa ndio mwanzo wa kutolewa nje ya Bara Arabu hadi Shām. Hamkudhani, enyi Waislamu, kuwa watatoka majumbani mwao kwa unyonge huu na utwevu, kwa silaha kali waliokuwa nazo na hifadhi ya nguvu waliokuwa nayo. Na walidhani Mayahudi kuwa ngome zao zitawakinga na adhabu ya Mwenyezi Mungu na kuwa hakuna anayeziweza. Basi amri ya Mwenyezi Mungu ilizijilia kwa namna ambayo haikupita kwenye akili zao, na Mwenyezi Mungu Akawatia hofu na kicho kikubwa, wakawa wanazivunja nyumba zao kwa mikono yao na mikono ya Waumini, basi zingatieni, enyi wenye busara timamu na akili nyingi kwa hayo yaliyowafika wao.
Tefsiret në gjuhën arabe:
 
Përkthimi i kuptimeve Ajeti: (2) Surja: Suretu El Hashr
Përmbajtja e sureve Numri i faqes
 
Përkthimi i kuptimeve të Kuranit Fisnik - Përkthimi suahilisht - Abdullah Muhammed dhe Nasir Khamis - Përmbajtja e përkthimeve

Përkthimi i kuptimeve të Kuranit në suahilishte - Përkthyer nga Abdullah Muhammed dhe Nasir Khamis - Botuar nga Kompleksi Mbreti Fehd për Botimin e Mushafit Fisnik në Medinë. Viti i botimit: 1435 h.

Mbyll