23 : 43

وَكَذَٰلِكَ مَآ أَرۡسَلۡنَا مِن قَبۡلِكَ فِي قَرۡيَةٖ مِّن نَّذِيرٍ إِلَّا قَالَ مُتۡرَفُوهَآ إِنَّا وَجَدۡنَآ ءَابَآءَنَا عَلَىٰٓ أُمَّةٖ وَإِنَّا عَلَىٰٓ ءَاثَٰرِهِم مُّقۡتَدُونَ

Hivyo ndivyo ilivyo, hatukutuma kabla yako, ewe Mtume, muonyaji yoyote kwenye kijiji chochote, mwenye kuwaonya na adhabu yetu kwa kutukanusha, na akawaonya na kuwatahadharisha na adhabu yetu, isipokuwa wale ambao ziliwatia kiburi neema miongoni mwa viongozi, na wakubwa huwa wakisema, ”Sisi tuliwakuta baba zetu kwenye mila na dini, na sisi ni wenye kufuata mwenendo wao na njia yao.” info
التفاسير: |
prev

Az-Zukhruf

next
:
0:00 0:00