Check out the new design

పవిత్ర ఖురాన్ యొక్క భావార్థాల అనువాదం - స్వాహిలి అనువాదం - అబ్దుల్లాహ్ ముహమ్మద్ మరియు నాసర్ ఖమీస్ * - అనువాదాల విషయసూచిక


భావార్ధాల అనువాదం సూరహ్: అల్-హష్ర్   వచనం:
فَكَانَ عَٰقِبَتَهُمَآ أَنَّهُمَا فِي ٱلنَّارِ خَٰلِدَيۡنِ فِيهَاۚ وَذَٰلِكَ جَزَٰٓؤُاْ ٱلظَّٰلِمِينَ
Basi mwisho wa Shetani na yule binadamu aliyemtii na akakufuru ni kwamba wote wawili wataingia Motoni hali ya kukaa humo milele. Na hayo ndiyo malipo ya wenye kudhulumu na kukiuka mipaka ya Mwenyezi Mungu.
అరబీ భాషలోని ఖుర్ఆన్ వ్యాఖ్యానాలు:
يَٰٓأَيُّهَا ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ ٱتَّقُواْ ٱللَّهَ وَلۡتَنظُرۡ نَفۡسٞ مَّا قَدَّمَتۡ لِغَدٖۖ وَٱتَّقُواْ ٱللَّهَۚ إِنَّ ٱللَّهَ خَبِيرُۢ بِمَا تَعۡمَلُونَ
Enyi mliomuamini Mwenyezi Mungu na Mtume Wake na mkafuata Sheria Zake kivitendo! Muogopeni Mwenyezi Mungu na jihadharini na mateso Yake kwa kuyafanya Aliyowaamrisha na kuyaacha Aliyowakataza, na kila mtu ayazingatie matendo aliyoyatanguliza kwa Siku ya Kiyama. Na muogopeni Mwenyezi Mungu katika kila mnachokitenda na mnachokiacha, hakika Mwenyezi Mungu , Aliyetakasika, ni Mtambuzi wa mnayoyafanya, hakuna chochote kinachofichamana Kwake miongoni mwa matendo yenu, na Yeye ni Mwenye kuwalipa nyinyi kwa hayo.
అరబీ భాషలోని ఖుర్ఆన్ వ్యాఖ్యానాలు:
وَلَا تَكُونُواْ كَٱلَّذِينَ نَسُواْ ٱللَّهَ فَأَنسَىٰهُمۡ أَنفُسَهُمۡۚ أُوْلَٰٓئِكَ هُمُ ٱلۡفَٰسِقُونَ
Na msiwe, enyi Waumini, kama wale walioacha kutekeleza haki ya Mwenyezi Mungu Aliyoipasisha juu yao, na kwa sababu hiyo Akawasahaulisha wao kujifanyia wema nafsi zao kwa kufanya matendo mema yenye kuwaokoa wao na adhabu ya Siku ya Kiyama. Hao ndio wenye kusifika kwa uasi, wenye kutoka nje ya utiifu kwa Mwenyezi Mungu na utiifu kwa Mtume Wake.
అరబీ భాషలోని ఖుర్ఆన్ వ్యాఖ్యానాలు:
لَا يَسۡتَوِيٓ أَصۡحَٰبُ ٱلنَّارِ وَأَصۡحَٰبُ ٱلۡجَنَّةِۚ أَصۡحَٰبُ ٱلۡجَنَّةِ هُمُ ٱلۡفَآئِزُونَ
Hawalingani sawa, watu wa Motoni wanaoadhibiwa na watu wa Peponi wanaostareheshwa. Watu wa Peponi ndio wenye kupata kila kinachotakiwa, ndio wenye kuokoka na kila kinachochukiwa.
అరబీ భాషలోని ఖుర్ఆన్ వ్యాఖ్యానాలు:
لَوۡ أَنزَلۡنَا هَٰذَا ٱلۡقُرۡءَانَ عَلَىٰ جَبَلٖ لَّرَأَيۡتَهُۥ خَٰشِعٗا مُّتَصَدِّعٗا مِّنۡ خَشۡيَةِ ٱللَّهِۚ وَتِلۡكَ ٱلۡأَمۡثَٰلُ نَضۡرِبُهَا لِلنَّاسِ لَعَلَّهُمۡ يَتَفَكَّرُونَ
Lau tungaliiteremsha hii Qur’ani juu ya jabali moja miongoni mwa majabali, na likaelewa yaliyo ndani yake ya ahadi ya malipo mema kwa watu wema na malipo mabaya kwa watu wabaya, ungaliliona, pamoja na nguvu zake, ugumu wake na ukuu wake, limenyenyekea, limejidhalilisha na limepasukapasuka kwa kumuogopa Mwenyezi Mungu Aliyetukuka. Na hiyo ni mifano tunawapigia watu na kuwabainishia, huenda wao wakafikiria juu ya uweza wa Mwenyezi Mungu na ukubwa Wake. Katika aya hii pana kuhimiza kuizingatia Qur’ani na kujifahamisha maana yake na kuitumia.
అరబీ భాషలోని ఖుర్ఆన్ వ్యాఖ్యానాలు:
هُوَ ٱللَّهُ ٱلَّذِي لَآ إِلَٰهَ إِلَّا هُوَۖ عَٰلِمُ ٱلۡغَيۡبِ وَٱلشَّهَٰدَةِۖ هُوَ ٱلرَّحۡمَٰنُ ٱلرَّحِيمُ
Yeye Ndiye Mwenyezi Mungu, Aliyetakasika na kutukuka, Anayeabudiwa kwa haki, Ambaye hakuna muabudiwa isipokuwa Yeye, Mjuzi wa yaliyofichika na yaliyojitokeza, Anayajua yaliyoghibu na yaliyoko. Yeye Ndiye Mwingi wa rehema Ambaye rehema Yake imeenea kila kitu, Anayewarehemu wenye kumuamini.
అరబీ భాషలోని ఖుర్ఆన్ వ్యాఖ్యానాలు:
هُوَ ٱللَّهُ ٱلَّذِي لَآ إِلَٰهَ إِلَّا هُوَ ٱلۡمَلِكُ ٱلۡقُدُّوسُ ٱلسَّلَٰمُ ٱلۡمُؤۡمِنُ ٱلۡمُهَيۡمِنُ ٱلۡعَزِيزُ ٱلۡجَبَّارُ ٱلۡمُتَكَبِّرُۚ سُبۡحَٰنَ ٱللَّهِ عَمَّا يُشۡرِكُونَ
Yeye Ndiye Mwenyezi Mungu Mwenye kuabudiwa kwa haki, Ambaye hakuna Mola isipokuwa Yeye, Mmiliki wa vitu vyote, Anayeviendesha bila kizuizi chochote wala upinzani, Aliyetakasika na kila upungufu, Aliyeepukana na kila aibu, Anayewasadikisha Mitume Wake na Manabii kwa dalili zilizo wazi Alizowatuma nazo, Anayewatunza viumbe Wake katika matendo yao, Aliye Mshindi Ambaye hakuna wa kushindana na Yeye, Aliye Jebari Ambaye Amewatendesha nguvu waja wote, na Ambaye viumbe vyote vimemdhalilikia, Aliye Mkubwa Mwenye kiburi na utukufu. Ametakasika Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka, na kila kile ambacho wanamshirikisha nacho katika kumuabudu.
అరబీ భాషలోని ఖుర్ఆన్ వ్యాఖ్యానాలు:
هُوَ ٱللَّهُ ٱلۡخَٰلِقُ ٱلۡبَارِئُ ٱلۡمُصَوِّرُۖ لَهُ ٱلۡأَسۡمَآءُ ٱلۡحُسۡنَىٰۚ يُسَبِّحُ لَهُۥ مَا فِي ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضِۖ وَهُوَ ٱلۡعَزِيزُ ٱلۡحَكِيمُ
Yeye Ndiye Mwenyezi Mungu, kutakasika ni Kwake na kutukuka ni Kwake, Aliye Muumba, Muanzilishi wa uumbaji kulingana na hekima Yake, Aliyewapa sura viumbe Wake kwa namna Atakavyo. Ni Yake Yeye, kutakasika ni Kwake, Majina Mema na sifa tukufu. Vinamatakasa Yeye vyote vilivyoko mbinguni na ardhini, na Yeye ni Mshindi, Mkali wa mateso kwa maadui Wake, Mwingi wa hekima katika uendeshaji Wake mambo ya viumbe Vyake.
అరబీ భాషలోని ఖుర్ఆన్ వ్యాఖ్యానాలు:
 
భావార్ధాల అనువాదం సూరహ్: అల్-హష్ర్
సూరాల విషయసూచిక పేజీ నెంబరు
 
పవిత్ర ఖురాన్ యొక్క భావార్థాల అనువాదం - స్వాహిలి అనువాదం - అబ్దుల్లాహ్ ముహమ్మద్ మరియు నాసర్ ఖమీస్ - అనువాదాల విషయసూచిక

అనువాదం డా. అబ్దుల్లాహ్ ముహమ్మద్ అబూబక్ర్ మరియు షేక్ నాసిర్ ఖమీస్.

మూసివేయటం