Check out the new design

పవిత్ర ఖురాన్ యొక్క భావార్థాల అనువాదం - స్వాహిలి అనువాదం - అబ్దుల్లాహ్ ముహమ్మద్ మరియు నాసర్ ఖమీస్ * - అనువాదాల విషయసూచిక


భావార్ధాల అనువాదం సూరహ్: అల్-అన్ఆమ్   వచనం:
۞ وَلَوۡ أَنَّنَا نَزَّلۡنَآ إِلَيۡهِمُ ٱلۡمَلَٰٓئِكَةَ وَكَلَّمَهُمُ ٱلۡمَوۡتَىٰ وَحَشَرۡنَا عَلَيۡهِمۡ كُلَّ شَيۡءٖ قُبُلٗا مَّا كَانُواْ لِيُؤۡمِنُوٓاْ إِلَّآ أَن يَشَآءَ ٱللَّهُ وَلَٰكِنَّ أَكۡثَرَهُمۡ يَجۡهَلُونَ
Na lau kama sisi tungaliyaitikia maombi ya washirikina hawa na kuwateremshia Malaika kutoka mbinguni na tukawafufulia wafu wakazungumza nao na tukawakusanyia kila kitu walichokitaka wakakiona ana kwa ana, hawangaliyakubali yale uliyowaitia, ewe Mtume, na hawangaliyatumia, isipokuwa yule ambaye Mwenyezi Mungu Alimtakia uongofu. Lakini wengi wa hawa makafiri hawaijui haki ambayo umekuja nayo kutoka kwa Mwenyezi Mungu.
అరబీ భాషలోని ఖుర్ఆన్ వ్యాఖ్యానాలు:
وَكَذَٰلِكَ جَعَلۡنَا لِكُلِّ نَبِيٍّ عَدُوّٗا شَيَٰطِينَ ٱلۡإِنسِ وَٱلۡجِنِّ يُوحِي بَعۡضُهُمۡ إِلَىٰ بَعۡضٖ زُخۡرُفَ ٱلۡقَوۡلِ غُرُورٗاۚ وَلَوۡ شَآءَ رَبُّكَ مَا فَعَلُوهُۖ فَذَرۡهُمۡ وَمَا يَفۡتَرُونَ
Na kama tulivyokujaribu wewe, ewe Mtume, kwa maadui zako miongoni mwa washirikina, tuliwajaribu Manabii wote, amani iwashukie, kwa maadui miongoni mwa waasi wa watu wao na maadui miongoni mwa waasi wa majini, wanapelekeana wenyewe kwa wenyewe maneno waliyoyapamba kwa uharibifu, ili adanganyike mwenye kuyasikia na apate kupotea njia ya Mwenyezi Mungu. Na lau Mola wako, Aliyetukuka na kuwa juu, Alitaka, angaliweka kizuizi kati yao na ule uadui, lakini huo ni mtihani kutoka kwa Mwenyezi Mungu. Basi waache na kile wanachokibuni cha urongo na uzushi.
అరబీ భాషలోని ఖుర్ఆన్ వ్యాఖ్యానాలు:
وَلِتَصۡغَىٰٓ إِلَيۡهِ أَفۡـِٔدَةُ ٱلَّذِينَ لَا يُؤۡمِنُونَ بِٱلۡأٓخِرَةِ وَلِيَرۡضَوۡهُ وَلِيَقۡتَرِفُواْ مَا هُم مُّقۡتَرِفُونَ
Na ili zielekee huko nyoyo za makafiri ambao hawaamini maisha ya Akhera wala hawayafanyii matendo ya kuwafaa, na ili nafsi zao zipate kuyapenda, na ili wapate kuyafanya maovu ambayo wao ni wenye kuyafanya. Katika haya, pana onyo kubwa kwao.
అరబీ భాషలోని ఖుర్ఆన్ వ్యాఖ్యానాలు:
أَفَغَيۡرَ ٱللَّهِ أَبۡتَغِي حَكَمٗا وَهُوَ ٱلَّذِيٓ أَنزَلَ إِلَيۡكُمُ ٱلۡكِتَٰبَ مُفَصَّلٗاۚ وَٱلَّذِينَ ءَاتَيۡنَٰهُمُ ٱلۡكِتَٰبَ يَعۡلَمُونَ أَنَّهُۥ مُنَزَّلٞ مِّن رَّبِّكَ بِٱلۡحَقِّۖ فَلَا تَكُونَنَّ مِنَ ٱلۡمُمۡتَرِينَ
Sema, ewe Mtume, kuwaambia hawa washirikina, «Kwani kwa asiyekuwa Mwenyezi Mungu, Aliye Mola wangu na Mola wenu, natafuta uamuzi kati yangu na nyinyi, na hali Yeye, kutakasika na sifa pungufu ni Kwake, Amewateremshia Qur’ani ambayo ndani yake pana ufafanuzi wa uamuzi wa yale ambayo mlikuwa mkiteta juu yake kuhusu mambo yangu na mambo yenu?» Na Wana wa Isrāīl waliopewa na Mwenyezi Mungu Taurati na Injili wana ujuzi wa yakini kwamba hii Qur’ani imeteremshwa kwako, ewe Mtume, kutoka kwa Mola wako kwa haki. Basi usiwe, tena usiwe, ni miongoni mwa wenye shaka juu ya chochote ambacho tumekuletea wahyi.
అరబీ భాషలోని ఖుర్ఆన్ వ్యాఖ్యానాలు:
وَتَمَّتۡ كَلِمَتُ رَبِّكَ صِدۡقٗا وَعَدۡلٗاۚ لَّا مُبَدِّلَ لِكَلِمَٰتِهِۦۚ وَهُوَ ٱلسَّمِيعُ ٱلۡعَلِيمُ
Na limekamilika neno la Mola wako, nalo ni Qur’ani, likiwa lina ukweli wa habari na maneno, lenye uadilifu wa hukumu. Hakuna anayeweza kuyabadilisha maneno yake yaliyokamilika. Na Mwenyezi Mungu Aliyetukuka, Ndiye Mwenye kuyasikia wanayoyasema waja Wake, Ndiye mwenye kuyajua mambo yao yaliyo waziwazi na yaliyojificha
అరబీ భాషలోని ఖుర్ఆన్ వ్యాఖ్యానాలు:
وَإِن تُطِعۡ أَكۡثَرَ مَن فِي ٱلۡأَرۡضِ يُضِلُّوكَ عَن سَبِيلِ ٱللَّهِۚ إِن يَتَّبِعُونَ إِلَّا ٱلظَّنَّ وَإِنۡ هُمۡ إِلَّا يَخۡرُصُونَ
Na lau itakadiriwa, ewe Mtume, kwamba wewe uliwasikiliza wengi kati ya watu wanaokaa ardhini, kwa kweli wanagalikupoteza ukawa kando na dini ya Mwenyezi Mungu. Kwani wao hawaendi isipokuwa kwenye yale wanayoyaona kuwa ni haki kwa kuwaiga wakale wao. Na hawakuwa wao isipokuwa tu wanadhania na wanasema urongo.
అరబీ భాషలోని ఖుర్ఆన్ వ్యాఖ్యానాలు:
إِنَّ رَبَّكَ هُوَ أَعۡلَمُ مَن يَضِلُّ عَن سَبِيلِهِۦۖ وَهُوَ أَعۡلَمُ بِٱلۡمُهۡتَدِينَ
Na kwa hakika, Mola wako Ndiye Anayewajua zaidi wenye kupotea njia ya uongofu; na Yeye Anawajuwa zaidi, kuliko nyinyi, wale walio kwenye njia ya uongofu na usawa; hafichiki Kwake yoyote katika wao.
అరబీ భాషలోని ఖుర్ఆన్ వ్యాఖ్యానాలు:
فَكُلُواْ مِمَّا ذُكِرَ ٱسۡمُ ٱللَّهِ عَلَيۡهِ إِن كُنتُم بِـَٔايَٰتِهِۦ مُؤۡمِنِينَ
Basi kuleni, kati ya wanyama waliochinjwa, wale ambao jina la Mwenyezi Mungu lilitajwa wakati wa kuchinjwa, iwapo nyinyi mnaziamini hoja za Mwenyezi Mungu, aliyetukuka, zilizo wazi.
అరబీ భాషలోని ఖుర్ఆన్ వ్యాఖ్యానాలు:
 
భావార్ధాల అనువాదం సూరహ్: అల్-అన్ఆమ్
సూరాల విషయసూచిక పేజీ నెంబరు
 
పవిత్ర ఖురాన్ యొక్క భావార్థాల అనువాదం - స్వాహిలి అనువాదం - అబ్దుల్లాహ్ ముహమ్మద్ మరియు నాసర్ ఖమీస్ - అనువాదాల విషయసూచిక

అనువాదం డా. అబ్దుల్లాహ్ ముహమ్మద్ అబూబక్ర్ మరియు షేక్ నాసిర్ ఖమీస్.

మూసివేయటం