Check out the new design

แปล​ความหมาย​อัลกุรอาน​ - คำแปลภาษาสวาฮิลี - อับดุลลอฮ์ มุฮัมมัด และ นาศิร เคาะมีส * - สารบัญ​คำแปล


แปลความหมาย​ สูเราะฮ์: Al-Mu’minūn   อายะฮ์:
۞ وَلَوۡ رَحِمۡنَٰهُمۡ وَكَشَفۡنَا مَا بِهِم مِّن ضُرّٖ لَّلَجُّواْ فِي طُغۡيَٰنِهِمۡ يَعۡمَهُونَ
Na lau tungaliwahurumia na tukawaaondolea ukame na njaa, wangaliendelea kwenye ukafiri na ushindani, wakiwa katika hali ya kuduwaa na kukosa muelekeo.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
وَلَقَدۡ أَخَذۡنَٰهُم بِٱلۡعَذَابِ فَمَا ٱسۡتَكَانُواْ لِرَبِّهِمۡ وَمَا يَتَضَرَّعُونَ
Na kwa hakika, tuliwajaribu wao kwa kuwaonja kwa aina mbalimbali za mikasa, pamoja na hivyo wasimnyenyekee Mola wao na wasimuombe kwa unynyekevu wakati wa kushukiwa na hiyo mikasa.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
حَتَّىٰٓ إِذَا فَتَحۡنَا عَلَيۡهِم بَابٗا ذَا عَذَابٖ شَدِيدٍ إِذَا هُمۡ فِيهِ مُبۡلِسُونَ
Mpaka tulipowafungulia juu yao mlango wa adhabu kali huko Akhera, wakitahamaki wamo ndani yake, wamekata tamaa kupata kheri yoyote, wamechanganyikiwa hawajui wafanye nini.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
وَهُوَ ٱلَّذِيٓ أَنشَأَ لَكُمُ ٱلسَّمۡعَ وَٱلۡأَبۡصَٰرَ وَٱلۡأَفۡـِٔدَةَۚ قَلِيلٗا مَّا تَشۡكُرُونَ
Na yeye Ndiye Aliyewaumbia masikizi ya kuvisikia venye kusikika, na macho ya kuviona venye kuonekana, na nyoyo ili muelewe. Pamoja na hayo, shukrani zenu kwa hizi neema za mfululizo juu yenu bado ni chache hata hazitajiki.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
وَهُوَ ٱلَّذِي ذَرَأَكُمۡ فِي ٱلۡأَرۡضِ وَإِلَيۡهِ تُحۡشَرُونَ
Na yeye Ndiye Aliyewaumba watu wote katika ardhi, na Kwake Yeye mtakusanywa baada ya kufa kwenu, na hapo Atawalipa kwa mliyoyatenda, mema au maovu.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
وَهُوَ ٱلَّذِي يُحۡيِۦ وَيُمِيتُ وَلَهُ ٱخۡتِلَٰفُ ٱلَّيۡلِ وَٱلنَّهَارِۚ أَفَلَا تَعۡقِلُونَ
Na Yeye , Peke Yake, Ndiye Anayehuisha kutoka katia hali ya kutokuweko, na Ndiye Atakayefisha baada ya uhai. Na ni kwake Yeye kufuatana usiku na mchana na pia kupishana. Basi hamuuweki akilini mwenu uweza Wake na upweke Wake?
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
بَلۡ قَالُواْ مِثۡلَ مَا قَالَ ٱلۡأَوَّلُونَ
Lakini makafiri hawakuamini kuwa kuna kufufuliwa, lakini waliyakariri maneno ya wakale wao wakanushaji.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
قَالُوٓاْ أَءِذَا مِتۡنَا وَكُنَّا تُرَابٗا وَعِظَٰمًا أَءِنَّا لَمَبۡعُوثُونَ
walisema «Ati tutakapokufa na miili yetu ikatangamana na mchanga wa ardhi pamoja na mifupa yetu tutafufuliwa mara nyingine? Hili haliwi wala haliingii akilini.»
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
لَقَدۡ وُعِدۡنَا نَحۡنُ وَءَابَآؤُنَا هَٰذَا مِن قَبۡلُ إِنۡ هَٰذَآ إِلَّآ أَسَٰطِيرُ ٱلۡأَوَّلِينَ
Yameshasemwa maneno haya kuambiwa wazee wetu kitambo, kama vile unavyotuambia, ewe Muhammad, hatukuyaona kuwa yana uhakika. Hayakuwa haya isipokuwa ni porojo za watu wa kale.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
قُل لِّمَنِ ٱلۡأَرۡضُ وَمَن فِيهَآ إِن كُنتُمۡ تَعۡلَمُونَ
Waambie, «Ni ya nani Ardhi hii na walio ndani yake iwapo muna ujuzi?»
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
سَيَقُولُونَ لِلَّهِۚ قُلۡ أَفَلَا تَذَكَّرُونَ
Watakubali kwa lazima kwamba ni ya Mwenyezi Mungu, Yeye Ndiye Muumba wake na Ndiye Mwenye kuimiliki. Waambie, «Je, haliwi hilo kwenu ni lenye kuwafanya mukumbuke kuwa Yeye ni Muweza wa kuwafufua wafu na kuwarudishia uhai?»
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
قُلۡ مَن رَّبُّ ٱلسَّمَٰوَٰتِ ٱلسَّبۡعِ وَرَبُّ ٱلۡعَرۡشِ ٱلۡعَظِيمِ
Sema, «Ni nani Mola wa mbingu saba na Mola wa ‘Arsh iliyo kubwa, ambayo ndiyo kiumbe kikubwa kabisa na kilichoko juu kabisa?»
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
سَيَقُولُونَ لِلَّهِۚ قُلۡ أَفَلَا تَتَّقُونَ
Watasema kwa lazima kuwa hizo ni milki ya Mwenyezi Mungu. Basi waambie, «Mbona hamuogopi adhabu ya Mwenyezi Mungu mnapomuabudu asiyekuwa Yeye?»
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
قُلۡ مَنۢ بِيَدِهِۦ مَلَكُوتُ كُلِّ شَيۡءٖ وَهُوَ يُجِيرُ وَلَا يُجَارُ عَلَيۡهِ إِن كُنتُمۡ تَعۡلَمُونَ
Sema, «Ni nani mmiliki wa kila kitu? Na ni nani Ambaye mkononi Mwake kuna hazina za kila kitu? Na ni nani Anayempa himaya mwenye kutaka himaya Yake, ambapo hakuna anayeweza kumhami na kumlinda yule ambaye Mwenyezi Mungu Anataka kumuangamiza wala hakuna anayekinga shari Aliyoikadiria Mwenyezi Mungu, iwapo mnalijua hilo?»
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
سَيَقُولُونَ لِلَّهِۚ قُلۡ فَأَنَّىٰ تُسۡحَرُونَ
Watajibu kuwa hayo yote ni ya Mwenyezi Mungu. Sema uwaambie, «Vipi zinaondoka akili zenu na mnadanganywa na mnaepushwa njia ya kumpwekesha Mwenyezi Mungu na kumtii na kuyaamini mambo ya kufufuliwa na kurudishiwa uhai?»
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
 
แปลความหมาย​ สูเราะฮ์: Al-Mu’minūn
สารบัญสูเราะฮ์ หมายเลข​หน้า​
 
แปล​ความหมาย​อัลกุรอาน​ - คำแปลภาษาสวาฮิลี - อับดุลลอฮ์ มุฮัมมัด และ นาศิร เคาะมีส - สารบัญ​คำแปล

แปลโดย ดร.อับดุลลอฮ์ มุฮัมมัด อบูบักร์ และ ชัยค์ นาศิร เคาะมีส

ปิด