แปล​ความหมาย​อัลกุรอาน​ - คำแปลภาษาสวาฮิลี - อับดุลลอฮ์ มุหัมหมัด และ นาศิรฺ เคาะมีสฺ * - สารบัญ​คำแปล


แปลความหมาย​ อายะฮ์: (46) สูเราะฮ์: Al-‘Ankabūt
۞ وَلَا تُجَٰدِلُوٓاْ أَهۡلَ ٱلۡكِتَٰبِ إِلَّا بِٱلَّتِي هِيَ أَحۡسَنُ إِلَّا ٱلَّذِينَ ظَلَمُواْ مِنۡهُمۡۖ وَقُولُوٓاْ ءَامَنَّا بِٱلَّذِيٓ أُنزِلَ إِلَيۡنَا وَأُنزِلَ إِلَيۡكُمۡ وَإِلَٰهُنَا وَإِلَٰهُكُمۡ وَٰحِدٞ وَنَحۡنُ لَهُۥ مُسۡلِمُونَ
Na wala msijadiliane, enyi Waumini, na Mayahudi na Wanaswara isipokuwa kwa njia nzuri na maneno mazuri na kulingania kwenye haki kwa njia sahali yenye kupelekea kwenye lengo hilo, isipokuwa wale ambao wamekaa kando na haki wakafanya ushindani na kiburi na wakatangaza vita juu yenu, basi hao piganeni nao kwa upanga mpaka waamini au watoe jizia (kodi maalumu) kwa mkono na wao wakiwa katika hali ya unyonge. Na semeni, «Tumeiamini Qur’ani iliyoteremshwa kwetu, na tumeiamini Taurati na Injili ambazo mliteremshiwa, na Mola wetu na Mola wenu ni Mmoja Hana mshirika Wake katika uungu Wake, wala katika sifa Yake ya kuwa ni Mola, wala majina Yake na sifa Zake. Na sisi ni wenye kunyenyekea na kujifanya wanyonge Kwake kwa kumtii katika yale Aliyotuamrisha na Aliyotukataza.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
 
แปลความหมาย​ อายะฮ์: (46) สูเราะฮ์: Al-‘Ankabūt
สารบัญสูเราะฮ์ หมายเลข​หน้า​
 
แปล​ความหมาย​อัลกุรอาน​ - คำแปลภาษาสวาฮิลี - อับดุลลอฮ์ มุหัมหมัด และ นาศิรฺ เคาะมีสฺ - สารบัญ​คำแปล

แปลความหมายอัลกุรอานเป็นภาษาสวาฮิลีโดย ดร.อับดุลลอฮ์ มุฮัมหมัด อบูบักร และ ชัยค์ นาศิร เคาะมีส

ปิด