Check out the new design

แปล​ความหมาย​อัลกุรอาน​ - คำแปลภาษาสวาฮิลี - อับดุลลอฮ์ มุฮัมมัด และ นาศิร เคาะมีส * - สารบัญ​คำแปล


แปลความหมาย​ สูเราะฮ์: Fussilat   อายะฮ์:
إِنَّ ٱلَّذِينَ قَالُواْ رَبُّنَا ٱللَّهُ ثُمَّ ٱسۡتَقَٰمُواْ تَتَنَزَّلُ عَلَيۡهِمُ ٱلۡمَلَٰٓئِكَةُ أَلَّا تَخَافُواْ وَلَا تَحۡزَنُواْ وَأَبۡشِرُواْ بِٱلۡجَنَّةِ ٱلَّتِي كُنتُمۡ تُوعَدُونَ
Hakika ya wale waliosema, «Mola wetu ni Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka, Peke Yake kisha wakasimama imara kufuata Sheria Yake, Malaika watawateremkia wakati wa kufa waseme kuwaambia, «Msiogopeni kufa na yatakayokuwa baada yake, wala msiwe na masikitiko juu ya yale mtakayoyaacha nyuma yenu katika mambo ya kilimwengu, na furahikeni kwa Pepo ambyo mlikuwa mkiahidiwa.»
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
نَحۡنُ أَوۡلِيَآؤُكُمۡ فِي ٱلۡحَيَوٰةِ ٱلدُّنۡيَا وَفِي ٱلۡأٓخِرَةِۖ وَلَكُمۡ فِيهَا مَا تَشۡتَهِيٓ أَنفُسُكُمۡ وَلَكُمۡ فِيهَا مَا تَدَّعُونَ
Na Malaika watasema kuwaambia wao, «Sisi ndio wasaidizi wenu katika uhai wa ulimwenguni, tunawaelekeza sawa na tunawatunza kwa amri ya Mwenyezi Mungu, na pia tutakuwa na nyinyi huko Akhera. Na mtapata huko Peponi kila kile ambacho nafsi zenu zinakitamani katika vitu mnavyovichagua na ambavyo macho yenu yanatulia kwa kuvipata. Na chochote kile mtakachokitaka kitakuwa mbele yenu,
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
نُزُلٗا مِّنۡ غَفُورٖ رَّحِيمٖ
mkiandaliwa na kuneemeshwa kutoka kwa Mwingi wa kusamehe dhambi zenu, Mwingi wa huruma kwenu.»
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
وَمَنۡ أَحۡسَنُ قَوۡلٗا مِّمَّن دَعَآ إِلَى ٱللَّهِ وَعَمِلَ صَٰلِحٗا وَقَالَ إِنَّنِي مِنَ ٱلۡمُسۡلِمِينَ
Hakuna yoyote aliye na kauli nzuri zaidi kuliko yule anayelingania kupwekeshwa Mwenyezi Mungu na kuuabudiwa Yeye Peke Yake, na anayesema, «Mimi ni katika Waislamu wanaofuata amri Ya Mwenyezi Mungu na Sheria Yake.» Katika aya hii kuna kusisitiza kulingania kwa Mwenyezi Mungu Aliyetakasika na kueleza utukufu wa wanavyuoni wenye kulingania Kwake kwa ujuzi, kulingana na yale yaliyokuja kutoka kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu, rehema na amani zimshukie.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
وَلَا تَسۡتَوِي ٱلۡحَسَنَةُ وَلَا ٱلسَّيِّئَةُۚ ٱدۡفَعۡ بِٱلَّتِي هِيَ أَحۡسَنُ فَإِذَا ٱلَّذِي بَيۡنَكَ وَبَيۡنَهُۥ عَدَٰوَةٞ كَأَنَّهُۥ وَلِيٌّ حَمِيمٞ
Na halilingani jema la waliomuamini Mwenyezi Mungu, wakasimama imara kwenye Sheria Yake, wakawafanyia wema viumbe Vyake (hilo halilingani) na baya la waliomkanusha Yeye, wakaenda kinyume na amri Yake na wakawafanyia ubaya viumbe Vyake. Msukume, ewe Mtume, kwa msamaha wako, upole wako na hisani yako yule anayekufanyia ubaya, na upambane na ubaya wake kwako kwa kumfanyia wema. Hivyo basi yule aliyekutendea ubaya ambaye baina yako wewe na yeye kuna uadui atakuwa kama kwamba yeye ni mtu aliye jamaa yako wa karibu na mwenye huruma na wewe.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
وَمَا يُلَقَّىٰهَآ إِلَّا ٱلَّذِينَ صَبَرُواْ وَمَا يُلَقَّىٰهَآ إِلَّا ذُو حَظٍّ عَظِيمٖ
Na hawaafikiwi kwenye mambo haya yanayosifika vyema isipokuwa wale wanaojisubirisha juu ya mambo ambayo nafsi zao zinayachukia na wakajilazimisha kwa yale Anayoyapenda Mwenyezi Mungu. Na haafikiwi hayo isipokuwa mwenye fungu kubwa la hali njema ya duniani na Akhera.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
وَإِمَّا يَنزَغَنَّكَ مِنَ ٱلشَّيۡطَٰنِ نَزۡغٞ فَٱسۡتَعِذۡ بِٱللَّهِۖ إِنَّهُۥ هُوَ ٱلسَّمِيعُ ٱلۡعَلِيمُ
Na Shetani anapotia ndani ya nafsi yako ushawishi wa mawazo ya kukufanya umlipe mbaya kwa ubaya, basi omba himaya ya Mwenyezi Mungu na ushikamane na Yeye. Kwani Mwenyezi Mungu ni Mwenye kusikia sana maombi yako ya kujilinda Kwake, ni Mwenye kuyajua sana mambo ya viumbe Vyake vyote.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
وَمِنۡ ءَايَٰتِهِ ٱلَّيۡلُ وَٱلنَّهَارُ وَٱلشَّمۡسُ وَٱلۡقَمَرُۚ لَا تَسۡجُدُواْ لِلشَّمۡسِ وَلَا لِلۡقَمَرِ وَٱسۡجُدُواْۤ لِلَّهِۤ ٱلَّذِي خَلَقَهُنَّ إِن كُنتُمۡ إِيَّاهُ تَعۡبُدُونَ
Na miongoni mwa hoja za Mwenyezi Mungu kwa viumbe Vyake, dalili za upweke Wake na ukamilifu wa uweza Wake, ni kutafautiana mchana na usiku na kufuatana (kila mojawapo kuufuata mwingine) na kutafautiana jua na mwezi na kufuatana, vyote hivyo viko chini ya uendeshaji Wake na utendeshaji nguvu Wake. Msilisujudie jua wala mwezi, kwani hivyo viwili vinaendeshwa na vimeumbwa; na msujudieni Mwenyezi Mungu Aliyeviumba, iwapo nyinyi kwa kweli mnafuata amri Yake, mnasikia na mnamtii Yeye, basi muabuduni Yeye Peke Yake Asiye na mshirika.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
فَإِنِ ٱسۡتَكۡبَرُواْ فَٱلَّذِينَ عِندَ رَبِّكَ يُسَبِّحُونَ لَهُۥ بِٱلَّيۡلِ وَٱلنَّهَارِ وَهُمۡ لَا يَسۡـَٔمُونَ۩
Na wakifanya kiburi wshirikina hawa kwa kukataa kumsujudia Mwenyezi Mungu, basi Malaika waliyoko kwa Mola wako hawafanyi kiburi cha kukataa hilo, bali wanamsujudia Yeye na wanamtakasa na kila upungufu, usiku na mchana, na wao hawapumziki na hilo wala hawachoki.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
 
แปลความหมาย​ สูเราะฮ์: Fussilat
สารบัญสูเราะฮ์ หมายเลข​หน้า​
 
แปล​ความหมาย​อัลกุรอาน​ - คำแปลภาษาสวาฮิลี - อับดุลลอฮ์ มุฮัมมัด และ นาศิร เคาะมีส - สารบัญ​คำแปล

แปลโดย ดร.อับดุลลอฮ์ มุฮัมมัด อบูบักร์ และ ชัยค์ นาศิร เคาะมีส

ปิด