Check out the new design

แปล​ความหมาย​อัลกุรอาน​ - คำแปลภาษาสวาฮิลี - อับดุลลอฮ์ มุฮัมมัด และ นาศิร เคาะมีส * - สารบัญ​คำแปล


แปลความหมาย​ สูเราะฮ์: At-Tahrīm   อายะฮ์:
يَٰٓأَيُّهَا ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ تُوبُوٓاْ إِلَى ٱللَّهِ تَوۡبَةٗ نَّصُوحًا عَسَىٰ رَبُّكُمۡ أَن يُكَفِّرَ عَنكُمۡ سَيِّـَٔاتِكُمۡ وَيُدۡخِلَكُمۡ جَنَّٰتٖ تَجۡرِي مِن تَحۡتِهَا ٱلۡأَنۡهَٰرُ يَوۡمَ لَا يُخۡزِي ٱللَّهُ ٱلنَّبِيَّ وَٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ مَعَهُۥۖ نُورُهُمۡ يَسۡعَىٰ بَيۡنَ أَيۡدِيهِمۡ وَبِأَيۡمَٰنِهِمۡ يَقُولُونَ رَبَّنَآ أَتۡمِمۡ لَنَا نُورَنَا وَٱغۡفِرۡ لَنَآۖ إِنَّكَ عَلَىٰ كُلِّ شَيۡءٖ قَدِيرٞ
Enyi mliomuamini Mwenyezi Mungu na mtume Wake na mkafuata Sheria Zake kivitendo! Acheni madhambi yenu na mrudi kwenye kumtii Mwenyezi Mungu, kurudi kwa mwisho kusikokuwa na ufanyaji maasia tena kwa kutarajia Mola wenu Awafutie maovu ya matendo yenu na Awaingize kwenye mabustani ya Peponi ambayo chini ya majumba yake ya fahari inapita mito ya maji, Siku ambayo Mwenyezi Mungu Hatamfedhehi Nabii na walioamini pamoja naye wala hatawatesa, bali Atavipandisha juu vyeo vyao. Nuru ya watu hawa itakuwa inatembea mbele yao na kuliani mwao huku wakisema, «Mola wetu! Tukamilishie sisi nuru yetu mpaka tuvuke Ṣirāṭ na tuongoke njia ya kwenda Peponi, na utusamehe na uyatupilie mbali madhambi yetu na uyasitiri, kwani wewe Kwa hakika ni Muweza juu ya kila kitu.»
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
يَٰٓأَيُّهَا ٱلنَّبِيُّ جَٰهِدِ ٱلۡكُفَّارَ وَٱلۡمُنَٰفِقِينَ وَٱغۡلُظۡ عَلَيۡهِمۡۚ وَمَأۡوَىٰهُمۡ جَهَنَّمُۖ وَبِئۡسَ ٱلۡمَصِيرُ
Ewe Nabii! Pigana jihadi na wale waliouonyesha ukafiri waziwazi na wakautangaza, na pigana nao kwa upanga, na pigana jihadi na wale waliouficha ukafiri na kuufinika kwa hoja na kwa kusimamisha hukumu za Sheria na vitambulisho vyaa Dini. Na utumie ukali na ugumu katika kupigana jihadi na makundi mawili hayo. Na makazi yao ambayo watakwenda kukaa huko Akhera ni moto wa Jahanamu. Na ni marejeo maovu mno hayo watakayoyarejea!
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
ضَرَبَ ٱللَّهُ مَثَلٗا لِّلَّذِينَ كَفَرُواْ ٱمۡرَأَتَ نُوحٖ وَٱمۡرَأَتَ لُوطٖۖ كَانَتَا تَحۡتَ عَبۡدَيۡنِ مِنۡ عِبَادِنَا صَٰلِحَيۡنِ فَخَانَتَاهُمَا فَلَمۡ يُغۡنِيَا عَنۡهُمَا مِنَ ٱللَّهِ شَيۡـٔٗا وَقِيلَ ٱدۡخُلَا ٱلنَّارَ مَعَ ٱلدَّٰخِلِينَ
Mwenyezi Mungu Anapiga mfano wa hali ya makafiri- katika kutangamana kwao na Waislamu, kuwa karibu na wao na kutangamana nao na kwamba hilo halitawanufaisha kwa kuwa wamemkufuru Mwenyezi Mungu- kuwa ni kama hali ya mke wa Nabii wa Mwenyezi Mungu, Nūḥ, na mke wa Nabii wa Mwenyezi mungu, Lūṭ, kwa kuwa wote wawili walikuwa chini ya hifadhi ya ndoa ya waja wawili wema miongoni mwa waja wetu, ukapatikana kutoka kwao kuwafanyia uhaini wa kidini, kwani wote wawili walikuwa makafiri. Mitume wawili hawa hawakuweza kuwatetea wake zao na adhabu ya Mwenyezi Mungu, na wakaambiwa wake wawili hao, «Ingieni Motoni pamoja na wenye kuingia huko.» Katika kupiga mfano huu pana dalili ya kwamba kuwa karibu na Manabii na watu wema hakufai kitu iwapo mtu mwenyewe ana matendo mabaya.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
وَضَرَبَ ٱللَّهُ مَثَلٗا لِّلَّذِينَ ءَامَنُواْ ٱمۡرَأَتَ فِرۡعَوۡنَ إِذۡ قَالَتۡ رَبِّ ٱبۡنِ لِي عِندَكَ بَيۡتٗا فِي ٱلۡجَنَّةِ وَنَجِّنِي مِن فِرۡعَوۡنَ وَعَمَلِهِۦ وَنَجِّنِي مِنَ ٱلۡقَوۡمِ ٱلظَّٰلِمِينَ
Na Mwenyezi Mungu Anapiga mfano wa hali ya Waumini- waliomuamini Mwenyezi Munmgu, wakamuabudu Peke Yake na wakazifuata Sheria Zake kivitendo na kwamba wao hakuwadhuru wao kule kutangamana kwao na makfiri katika maingilaiano yao- kuwa ni kama hali ya mke wa Fir'awn aliyekuwa kwenye hifadhi ya ndoa ya aliyekuwa muovu mno miongoni mwa wale waliomkufuru Mwenyezi Mungu, na hali yeye alikuwa anamuamini Mwenyezi Mungu, pindi aliposema, «Mola wangu! Nijengee Nyumba huko kwako Peponi na uniokoe na utawala wa Fir'awn na ukafiri wake na yale matendo maovu yanayotokana na yeye, Na uniokoe na watu wenye kumfuata katika udhalimu na upotevu, na uniokoe na mateso yao.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
وَمَرۡيَمَ ٱبۡنَتَ عِمۡرَٰنَ ٱلَّتِيٓ أَحۡصَنَتۡ فَرۡجَهَا فَنَفَخۡنَا فِيهِ مِن رُّوحِنَا وَصَدَّقَتۡ بِكَلِمَٰتِ رَبِّهَا وَكُتُبِهِۦ وَكَانَتۡ مِنَ ٱلۡقَٰنِتِينَ
Na Mwenyezi Mungu Anapiga mfano kwa walioamini. Mfano wenyewe ni Maryam binti 'Imran aliyeihifadhi tupu yake na akailinda na uzinifu, basi mwenyezi Mungu Akamuamrisha Jibrili, amani imshukie, apulize kwenye mfuko wa nguo yake. Na ule mpulizo ukafika kwenye uzao wake. Hapo akabeba mimba ya ‘Īsā, amani imshukie, akayaamini maneno ya Mola wake, akafuata kivitendo Sheria Zake Alizozipasisha kwa waja Wake na vitabu Vyake Alivyoviteremsha kwa Mitume Wake, na akawa ni miongoni mwa wale wenye kumtii Yeye.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
 
แปลความหมาย​ สูเราะฮ์: At-Tahrīm
สารบัญสูเราะฮ์ หมายเลข​หน้า​
 
แปล​ความหมาย​อัลกุรอาน​ - คำแปลภาษาสวาฮิลี - อับดุลลอฮ์ มุฮัมมัด และ นาศิร เคาะมีส - สารบัญ​คำแปล

แปลโดย ดร.อับดุลลอฮ์ มุฮัมมัด อบูบักร์ และ ชัยค์ นาศิร เคาะมีส

ปิด