Check out the new design

แปล​ความหมาย​อัลกุรอาน​ - คำแปลภาษาสวาฮิลี - อะลีย์ มุห์สิน อัลบัรวานีย์ * - สารบัญ​คำแปล

XML CSV Excel API
Please review the Terms and Policies

แปลความหมาย​ สูเราะฮ์: Saba’   อายะฮ์:
قُلۡ جَآءَ ٱلۡحَقُّ وَمَا يُبۡدِئُ ٱلۡبَٰطِلُ وَمَا يُعِيدُ
Sema: Kweli imefika, na uwongo haujitokezi, wala haurudi.
Waambie: Uislamu umedhihiri, wala uwongo hauwezi kuwa ndio njia ya kuipinga Haki. Na hizo mbinu za zamani hazirejei tena.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
قُلۡ إِن ضَلَلۡتُ فَإِنَّمَآ أَضِلُّ عَلَىٰ نَفۡسِيۖ وَإِنِ ٱهۡتَدَيۡتُ فَبِمَا يُوحِيٓ إِلَيَّ رَبِّيٓۚ إِنَّهُۥ سَمِيعٞ قَرِيبٞ
Sema: Ikiwa mimi nimepotea, basi nimepotea kwa kudhuru nafsi yangu mwenyewe. Na ikiwa nimeongoka, basi ni kwa sababu ya kunifunulia Mola wangu Mlezi. Hakika Yeye ni Mwenye kusikia, Aliye karibu.
Waambie: Nikiiacha Haki basi madhara ya hayo yataniangukia mwenyewe. Na nikiongoka basi nimeongozwa na Mola wangu Mlezi. Yeye ni Mwenye kusikia kauli yangu na kauli yenu. Yupo karibu nami, na karibu yenu.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
وَلَوۡ تَرَىٰٓ إِذۡ فَزِعُواْ فَلَا فَوۡتَ وَأُخِذُواْ مِن مَّكَانٖ قَرِيبٖ
Na lau ungeli ona watapo babaika, basi hapana pa kukimbilia! Na watakamatwa mahala pa karibu.
Na lau kuwa utaona, ewe mwenye kuona, pale watapo fazaika makafiri kweli itapo dhihiri, basi hawatakuwa na pa kukimbilia. Na watachukuliwa wapelekwe kwenye Moto kutoka pahala karibu.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
وَقَالُوٓاْ ءَامَنَّا بِهِۦ وَأَنَّىٰ لَهُمُ ٱلتَّنَاوُشُ مِن مَّكَانِۭ بَعِيدٖ
Na watasema: Tunaiamini! Lakini wataipata wapi kutoka huko mahala mbali?
Na watasema, watapo iona adhabu: Tunaiamini Haki! Na vipi wao waipate Imani kwa wepesi huo kutoka pahala mbali na dunia ambayo wakati wake umekwisha pita?
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
وَقَدۡ كَفَرُواْ بِهِۦ مِن قَبۡلُۖ وَيَقۡذِفُونَ بِٱلۡغَيۡبِ مِن مَّكَانِۭ بَعِيدٖ
Na hapo kabla yake waliikataa, na wakiyatupilia mbali maneno ya ghaibu kutoka mahali mbali.
Na ilhali wao walikwisha ikataa Haki kabla ya Siku hii, na wakavurumiza kwa dhana ya uwongo kutoka mahala palipo mbali na ukweli.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
وَحِيلَ بَيۡنَهُمۡ وَبَيۡنَ مَا يَشۡتَهُونَ كَمَا فُعِلَ بِأَشۡيَاعِهِم مِّن قَبۡلُۚ إِنَّهُمۡ كَانُواْ فِي شَكّٖ مُّرِيبِۭ
Na watatiliwa kizuizi baina yao na hayo wanayo yatamani, kama walivyo fanyiwa wenzao zamani. Hakika hao walikuwa na shaka ya kutia wasiwasi.
Patawekewa kizuizi baina yao na hayo wanayo yatamani ya Imani ya kuwafaa, kama walivyo fanyiwa wenzao wa kabla yao walipo amini baada ya kwisha wakati wake. Kwa sababu wote hao wote walikuwa katika kuifanyia Haki shaka inayo pelekea kutuhumiwa.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
 
แปลความหมาย​ สูเราะฮ์: Saba’
สารบัญสูเราะฮ์ หมายเลข​หน้า​
 
แปล​ความหมาย​อัลกุรอาน​ - คำแปลภาษาสวาฮิลี - อะลีย์ มุห์สิน อัลบัรวานีย์ - สารบัญ​คำแปล

ฉบับแปลโดย อาลี มุห์เซน อัล-บัรวานีย์

ปิด