แปล​ความหมาย​อัลกุรอาน​ - คำแปลภาษาสวาฮิลี - อะลีย์ มุหฺสิน อัลบัรวานีย์ * - สารบัญ​คำแปล

XML CSV Excel API
Please review the Terms and Policies

แปลความหมาย​ อายะฮ์: (32) สูเราะฮ์: An-Nisā’
وَلَا تَتَمَنَّوۡاْ مَا فَضَّلَ ٱللَّهُ بِهِۦ بَعۡضَكُمۡ عَلَىٰ بَعۡضٖۚ لِّلرِّجَالِ نَصِيبٞ مِّمَّا ٱكۡتَسَبُواْۖ وَلِلنِّسَآءِ نَصِيبٞ مِّمَّا ٱكۡتَسَبۡنَۚ وَسۡـَٔلُواْ ٱللَّهَ مِن فَضۡلِهِۦٓۚ إِنَّ ٱللَّهَ كَانَ بِكُلِّ شَيۡءٍ عَلِيمٗا
Wala msitamani alicho wafadhili Mwenyezi Mungu baadhi yenu kuliko wengine. Wanaume wana fungu katika walio vichuma, na wanawake wana fungu katika walio vichuma. Na muombeni Mwenyezi Mungu fadhila zake. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mjuzi wa kila kitu.
Wala haifai wanaume kutamani yale waliyo khusishwa nayo wanawake, wala haiwafalii wanawake kutamani waliyo khusishwa nayo wanaume. Kwani kila kikundi kina sehemu yake kwa mujibu wa tabia ya maumbile ya kazi zinazo wawajibikia, na haki wanazo ongezewa. Basi kila mmoja ajielekeze kutaraji ziada ya fadhila za Mwenyezi Mungu kwa kukuza vipawa alivyo pewa yeye na kutafuta msaada juu ya waajibu ulio juu yake. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mjuzi timamu wa kila kitu, na mtu amepewa namna ya kila kitu kinacho msilihi.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
 
แปลความหมาย​ อายะฮ์: (32) สูเราะฮ์: An-Nisā’
สารบัญสูเราะฮ์ หมายเลข​หน้า​
 
แปล​ความหมาย​อัลกุรอาน​ - คำแปลภาษาสวาฮิลี - อะลีย์ มุหฺสิน อัลบัรวานีย์ - สารบัญ​คำแปล

การแปลความหมายอัลกุรอานเป็นภาษาสวาฮิลี โดย อะลีย์ มุหฺสิน อัลบัรวานีย์

ปิด