แปล​ความหมาย​อัลกุรอาน​ - คำแปลภาษาสวาฮิลี - อะลีย์ มุหฺสิน อัลบัรวานีย์ * - สารบัญ​คำแปล

XML CSV Excel API
Please review the Terms and Policies

แปลความหมาย​ สูเราะฮ์: An-Naba’   อายะฮ์:

Surat An-Naba

عَمَّ يَتَسَآءَلُونَ
WANAULIZANA nini?
Wanaulizana nini hao makafiri?
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
عَنِ ٱلنَّبَإِ ٱلۡعَظِيمِ
Ile khabari kuu!
Wanaulizana khabari kubwa, khabari ya kufufuliwa,
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
ٱلَّذِي هُمۡ فِيهِ مُخۡتَلِفُونَ
Ambayo kwayo wanakhitalifiana.
Ambayo wao wamezama ndani yake kukhitalifiana baina ya wenye kuikataa na wenye kuitilia shaka.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
كَلَّا سَيَعۡلَمُونَ
La! Karibu watakuja jua.
Kuwazuia kuulizana huko wanaambiwa kuwa watakuja ujua ukweli wa mambo hapo watapo ona kufufuliwa kumetokea khasa.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
ثُمَّ كَلَّا سَيَعۡلَمُونَ
Tena la! Karibu watakuja jua.
Tena kuwazuia, watakuja jua itapo wateremkia adhabu.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
أَلَمۡ نَجۡعَلِ ٱلۡأَرۡضَ مِهَٰدٗا
kaKwani hatukuifanya ardhi ma tandiko?
Kwani wao hawaoni Ishara za uweza wetu kwamba Sisi tumeifanya ardhi imetandikwa upatikane utulivu juu yake na iwezekane kutembea juu yake?
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
وَٱلۡجِبَالَ أَوۡتَادٗا
kama Na milima vigingi?
Na tukaifanya milima ni vigingi vya ardhi vya kuituliza? Sehemu ya gamba gumu lilio juu ya ardhi linfikilia kiasi ya kilomita 60 unene wake, na inazidi mikunjo, mifimbi, inapanda juu kuwa milima, na huteremka chini kuwa ni vina vya bahari; na hiyo hulingana kwa sababu ya uzito unao patikana kutokana na milima. Na kulingana huko hakuharibiki ila kwa kubugunyika, kwani gamba kavu la ardhi linazuiliwa na milima, kama vigingi vinavyo zuilia khema. (Rejea Maoni ya Wataalamu juu ya Aya 7 ya Surat Qaf).
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
وَخَلَقۡنَٰكُمۡ أَزۡوَٰجٗا
Na tukakuumbeni kwa jozi?
Na tukakuumbeni kwa jozi, wanaume na wanawake?
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
وَجَعَلۡنَا نَوۡمَكُمۡ سُبَاتٗا
Na tukakufanya kulala kwenu ni mapumziko?
Na tukafanya kulala kwenu ni mapumziko ya machofu ya kazi? Kulala usingizi ni kusita nishat'i ya sehemu ya ubongo yenye kutambua na kuwa macho. Yaani gamba la ubongo, au kupunguka nishat'i yake kwa wingi, ukilinganisha na daraja za nishat'i ya sehemu za viungo vilio baki. Na kwa hivyo kunapunguka nguvu na joto la mwili, tena mwili hapo wakati wa usingizi hupata kutua na kupumzika baada ya kuhangaika viungo au akili au vyote viwili. Basi kazi za kimwili zote hupunguka isipo kuwa kazi za kusaga chakula, na kupitisha mkojo katika mafigo, na kutoka majasho katika ngozi, kwani yakisita hayo hupatikana madhara juu ya maisha ya mtu. Ama kuvuta pumzi huko nako hupunguka, na huwa ni kwa ndani zaidi, na huwa kwa kifua zaidi kuliko kwa tumbo. Na mpigo wa mishipa hupungua kasi kwa kunavyo tokana na moyo, na hudhoofika mkazano wa musulo (muscular tension), na kwa hivyo huwa taabu kupata harakati za kinyume. Na yote haya ni ili binaadamu apate kupumzika wakati wa kulala.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
وَجَعَلۡنَا ٱلَّيۡلَ لِبَاسٗا
Na tukaufanya usiku ni nguo?
Na tumeufanya usiku ni sitara kwenu kwa kiza kinacho kufunikeni.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
وَجَعَلۡنَا ٱلنَّهَارَ مَعَاشٗا
Na tukaufanya mchana ni wa kuchumia maisha?
Na tumeufanya mchana ni wakati wa kuhangaika kwenu kutafuta cha kukusaidieni katika maisha yenu.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
وَبَنَيۡنَا فَوۡقَكُمۡ سَبۡعٗا شِدَادٗا
Na tukajenga juu yenu saba zenye nguvu?
Na tumesimamisha juu yenu mbingu saba zenye nguvu madhubuti.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
وَجَعَلۡنَا سِرَاجٗا وَهَّاجٗا
Na tukaifanya taa yenye mwanga na joto;
Na Sisi tumeliumba jua lenye mwangaza na linalo waka. Makusudio ya Assiraj Alwahhaaj, Taa yenye mwanga na joto, ni Jua. Na hayo kama ilivyo thibiti katika sayansi kuwa daraja ya joto la uso wake inafika daraja 6000. Ama kati yake daraja yake inazidi daraja 30 milioni kwa sababu ya mdidimizo mkubwa unao patikana juu ya madda ziliomo ndani yake. Na jua linatoa nishat'i hizi zifuatazo: 9 katika 100 ya miale ya Ultraviolet rays, 46 katika 100 ya miale ya mwangaza, 45 katika 100 miale ya joto, au Infra red rays. Na kwa hivyo hii Aya tukufu imeliita kuwa ni Taa yenye mwangaza na joto.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
وَأَنزَلۡنَا مِنَ ٱلۡمُعۡصِرَٰتِ مَآءٗ ثَجَّاجٗا
Na tukateremsha maji yanayo anguka kwa kasi kutoka mawinguni,
Na tumeteremsha kutokana na mawingu yaliyo karibia kunyesha maji yenye kumiminika kwa nguvu. Mvua ndio kitu pekee kinacho toka asli yake maji matamu katika ardhi. Na asli ya mvua ni kukusanyika vijisehemu vya maji yanayo panda kutoka baharini, na maziwa na mito, yakakusanyika kama mawingu na yakageuka chembe za mvua au vipande vya barafu, na khatimaye yakaanguka kwa sura ya mvua au theluji.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
لِّنُخۡرِجَ بِهِۦ حَبّٗا وَنَبَاتٗا
Ili tutoe kwayo nafaka na mimea.
Ili tutoe kwa maji haya nafaka na mimea kuwa ni chakula kwa ajili ya watu na wanyama.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
وَجَنَّٰتٍ أَلۡفَافًا
Na mabustani yenye miti iliyo kamatana.
Na mabustani yenye miti iliyo fungamana na matawi yake yameingiliana.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
إِنَّ يَوۡمَ ٱلۡفَصۡلِ كَانَ مِيقَٰتٗا
Hakika siku ya uamuzi imewekewa wakati wake,
Hakika siku ya uamuzi baina ya viumbe imewekewa miadi ilio kwisha kadiriwa kwa ajili ya kufufuliwa.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
يَوۡمَ يُنفَخُ فِي ٱلصُّورِ فَتَأۡتُونَ أَفۡوَاجٗا
Siku litapo pulizwa barugumu, nanyi mtakuja kwa makundi,
Siku litakapo pulizwa barugumu na kufufuliwa watu, mtakuja kwenye mkutano makundi kwa makundi.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
وَفُتِحَتِ ٱلسَّمَآءُ فَكَانَتۡ أَبۡوَٰبٗا
Na mbingu zitafunguliwa, ziwe milango.
Na mbingu zitapasuliwa kila upande hata zitakuwa ni milango milango.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
وَسُيِّرَتِ ٱلۡجِبَالُ فَكَانَتۡ سَرَابًا
Na milima itaondolewa na itakuwa kama sarabi.
Na milima itaondolewa baada ya kung'olewa mwahala mwake, na kuvurugwa, ikawa unaiona kama sura ya milima na hali hiyo ni kifusi tu kilicho rindikwa, kama uonavyo mangati, sarabi, unaona kama sura ya maji nayo si maji.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
إِنَّ جَهَنَّمَ كَانَتۡ مِرۡصَادٗا
Hakika Jahannamu inangojea!
Hakika Jahannamu imekuwa kama ni kitu kinacho ngojea, walinzi wake wanawangojea watu watakao kuja kuingia.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
لِّلطَّٰغِينَ مَـَٔابٗا
Kwa walio asi ndio makaazi yao,
Yawe ni marejeo na mafikio kwa wenye kupindukia mipaka ya Mwenyezi Mungu.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
لَّٰبِثِينَ فِيهَآ أَحۡقَابٗا
Wakae humo karne baada ya karne,
Watakaa humo dahari baada ya dahari.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
لَّا يَذُوقُونَ فِيهَا بَرۡدٗا وَلَا شَرَابًا
Hawataonja humo chochote kibaridi wala kinywaji,
Hawataonja humo hata chembe ya upepo wa kuburudisha joto lake, wala kinywaji cha kupoza kiu chao.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
إِلَّا حَمِيمٗا وَغَسَّاقٗا
Ila maji yamoto sana na usaha,
Lakini watakunywa maji yalio pita ukomo kwa umoto wake, na usaha unao miminika kutokana na ngozi za watu wa Motoni.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
جَزَآءٗ وِفَاقًا
Ndio jaza muwafaka.
Malipo ya kuwafikiana na vitendo vyao viovu.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
إِنَّهُمۡ كَانُواْ لَا يَرۡجُونَ حِسَابٗا
Hakika hao hawakuwa wakitaraji kuwa kuna hisabu.
Kwani hao hawakutaraji kuwa itakuwapo kuhisabiwa, hata watende ya kuwaokoa humo.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
وَكَذَّبُواْ بِـَٔايَٰتِنَا كِذَّابٗا
Na wakikanusha Aya zetu kwa nguvu.
Wakazikadhibisha Ishara za Mwenyezi Mungu zenye kuthibitisha kufufuliwa kwa mkadhibisho mkali.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
وَكُلَّ شَيۡءٍ أَحۡصَيۡنَٰهُ كِتَٰبٗا
Na kila kitu Sisi tumekidhibiti kwa kukiandika.
Na kila kitu tumekidhibiti kwa kukiandika.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
فَذُوقُواْ فَلَن نَّزِيدَكُمۡ إِلَّا عَذَابًا
Basi onjeni! Nasi hatutakuzidishieni ila adhabu!
Basi onjeni, wala hampati kwetu ila kuzidishiwa adhabu tu.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
إِنَّ لِلۡمُتَّقِينَ مَفَازًا
Hakika wachamngu wanastahiki kufuzu,
Hakika wenye kumcha Mola wao Mlezi watapata kuokoka na adhabu, na wataipata Pepo,
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
حَدَآئِقَ وَأَعۡنَٰبٗا
Mabustani na mizabibu,
Na mabustani yenye matunda, na mizabibu mizuri,
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
وَكَوَاعِبَ أَتۡرَابٗا
Na wake walio lingana nao,
Na wanawari walio watipwatipwa wa hirimu yao,
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
وَكَأۡسٗا دِهَاقٗا
Na bilauri zilizo jaa,
Na bilauri safi zilizo jaa pomoni,
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
لَّا يَسۡمَعُونَ فِيهَا لَغۡوٗا وَلَا كِذَّٰبٗا
Hawatasikia humo upuuzi wala uwongo,
Hawasikii huko Peponi upuuzi wala uwongo.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
جَزَآءٗ مِّن رَّبِّكَ عَطَآءً حِسَابٗا
Malipo kutoka kwa Mola wako Mlezi, kipawa cha kutosha.
Ni malipo kutokana na Mola wako Mlezi, kwa fadhila yake na ihsani ya kutosha.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
رَّبِّ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضِ وَمَا بَيۡنَهُمَا ٱلرَّحۡمَٰنِۖ لَا يَمۡلِكُونَ مِنۡهُ خِطَابٗا
Mola Mlezi wa mbingu na ardhi na vilio baina yao, Arrahman, Mwingi wa rehema; hawamiliki usemi mbele yake!
Mola Mlezi wa mbinguni na duniani na vilio baina yao, ambaye rehema yake imeenea juu ya kila kitu. Hapana yeyote mwenye madaraka ya kusema mbele yake.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
يَوۡمَ يَقُومُ ٱلرُّوحُ وَٱلۡمَلَٰٓئِكَةُ صَفّٗاۖ لَّا يَتَكَلَّمُونَ إِلَّا مَنۡ أَذِنَ لَهُ ٱلرَّحۡمَٰنُ وَقَالَ صَوَابٗا
Siku atakapo simama Roho na Malaika kwa safu. Hawatasema ila Mwingi wa rehema aliye mruhusu, na atasema yaliyo sawa tu.
Siku atakapo simama Jibrili na Malaika walio teuliwa nao wamenyenyekea, hasemi mmoja wao ila akipewa idhini na Arrahman, Mwingi wa rehema, kuwa aseme, naye atasema lilio sawa tu.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
ذَٰلِكَ ٱلۡيَوۡمُ ٱلۡحَقُّۖ فَمَن شَآءَ ٱتَّخَذَ إِلَىٰ رَبِّهِۦ مَـَٔابًا
Hiyo ndiyo Siku ya haki. Basi anaye taka na ashike njia arejee kwa Mola wake Mlezi
Hiyo ndiyo siku isiyo na shaka. Basi atakaye na ashike njia ya kwenda kwa Mola wake Mlezi arejee kwa Imani, na a'mali njema.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
إِنَّآ أَنذَرۡنَٰكُمۡ عَذَابٗا قَرِيبٗا يَوۡمَ يَنظُرُ ٱلۡمَرۡءُ مَا قَدَّمَتۡ يَدَاهُ وَيَقُولُ ٱلۡكَافِرُ يَٰلَيۡتَنِي كُنتُ تُرَٰبَۢا
Hakika tumekuhadharisheni adhabu iliyo karibu kufika; Siku ambayo mtu atakapo ona yaliyo tangulizwa na mikono yake; na kafiri atasema: Laiti ningeli kuwa udongo!
Hakika Sisi tumekuhadharisheni na adhabu itakayo tokea karibu, siku atakapo angalia mtu vitendo vyake vilivyo tangulizwa na mikono yake, na atakapo sema kafiri kwa kutamani kuokoka: Laiti ningeli bakia udongo baada ya kufa, nisifufuliwe wala nisihisabiwe!
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
 
แปลความหมาย​ สูเราะฮ์: An-Naba’
สารบัญสูเราะฮ์ หมายเลข​หน้า​
 
แปล​ความหมาย​อัลกุรอาน​ - คำแปลภาษาสวาฮิลี - อะลีย์ มุหฺสิน อัลบัรวานีย์ - สารบัญ​คำแปล

การแปลความหมายอัลกุรอานเป็นภาษาสวาฮิลี โดย อะลีย์ มุหฺสิน อัลบัรวานีย์

ปิด