Salin ng mga Kahulugan ng Marangal na Qur'an - الترجمة السواحلية - علي محسن البرواني * - Indise ng mga Salin

XML CSV Excel API
Please review the Terms and Policies

Salin ng mga Kahulugan Ayah: (61) Surah: Hūd
۞ وَإِلَىٰ ثَمُودَ أَخَاهُمۡ صَٰلِحٗاۚ قَالَ يَٰقَوۡمِ ٱعۡبُدُواْ ٱللَّهَ مَا لَكُم مِّنۡ إِلَٰهٍ غَيۡرُهُۥۖ هُوَ أَنشَأَكُم مِّنَ ٱلۡأَرۡضِ وَٱسۡتَعۡمَرَكُمۡ فِيهَا فَٱسۡتَغۡفِرُوهُ ثُمَّ تُوبُوٓاْ إِلَيۡهِۚ إِنَّ رَبِّي قَرِيبٞ مُّجِيبٞ
Na kina Thamud tuliwapelekea ndugu yao Swaleh. Akasema: Enyi watu wangu! Muabuduni Mwenyezi Mungu. Nyinyi hamna Mungu ila Yeye. Yeye ndiye aliye kuumbeni katika ardhi, na akakuwekeni humo. Basi mwombeni msamaha, kisha mtubu kwake. Hakika Mola wangu Mlezi yupo karibu, anaitikia maombi.
Na kwa kina Thamud tulimtuma mmoja wao ambaye amefungana nao kwa nasaba na mapenzi, naye ni Swaleh. Akawaambia: Enyi watu wangu! Muabuduni Mwenyezi Mungu pekee. Nyinyi hamna anaye stahiki kuabudiwa isipo kuwa Yeye. Yeye ndiye aliye kuumbeni kwenye ardhi, na akakuwekeni muiimarishe, na muitoe mavuno ya kukufaeni kheri yake...Basi mwombeni Yeye apate kukusameheni makosa yenu yaliyo kwisha tangulia. Kisha mrejee kwake na majuto kwa mlivyo muasi, na mkubali kumtii, kila mnapo tumbukia katika madhambi. Hakika Mola wangu Mlezi yupo karibu kwa rehema, na Mwenye kupokea maombi kwa mwenye kutaka msamaha na kumwomba. Tazama maelezo ya ki-ilimu juu ya Aya 73 katika Sura Al-Aa'raaf (7).
Ang mga Tafsir na Arabe:
 
Salin ng mga Kahulugan Ayah: (61) Surah: Hūd
Indise ng mga Surah Numero ng Pahina
 
Salin ng mga Kahulugan ng Marangal na Qur'an - الترجمة السواحلية - علي محسن البرواني - Indise ng mga Salin

ترجمة معاني القرآن الكريم إلى اللغة السواحلية، ترجمها علي محسن البرواني.

Isara