Salin ng mga Kahulugan ng Marangal na Qur'an - الترجمة السواحلية - علي محسن البرواني * - Indise ng mga Salin

XML CSV Excel API
Please review the Terms and Policies

Salin ng mga Kahulugan Ayah: (16) Surah: At-Tawbah
أَمۡ حَسِبۡتُمۡ أَن تُتۡرَكُواْ وَلَمَّا يَعۡلَمِ ٱللَّهُ ٱلَّذِينَ جَٰهَدُواْ مِنكُمۡ وَلَمۡ يَتَّخِذُواْ مِن دُونِ ٱللَّهِ وَلَا رَسُولِهِۦ وَلَا ٱلۡمُؤۡمِنِينَ وَلِيجَةٗۚ وَٱللَّهُ خَبِيرُۢ بِمَا تَعۡمَلُونَ
Je, mlidhani kuwa mtaachwa tu, bila ya Mwenyezi Mungu kuwajuulisha wale walio pigana Jihadi kati yenu, na wala hawakumfanya mwendani wao isipo kuwa Mwenyezi Mungu na Mtume wake na Waumini wenziwe? Na Mwenyezi Mungu anazo khabari za yote mnayo yatenda.
Enyi Waumini! Msidhani kuwa Mwenyezi Mungu Mtukufu atakuacheni hivi hivi bila ya kukutieni mtihanini kwa Jihadi na mfano wa hayo. Ndio mwendo wake Mwenyezi Mungu kufanya mitihani, upate dhihiri ujuzi wake kwa wale kati yenu wanao pigana Jihadi, wenye ikhlasi (yaani nyoyo safi), na wala hawawafanyi marafiki, wendani na walinzi, isipo kuwa Mwenyezi Mungu na Mtume wake na Waumini wenzao. Na Mwenyezi Mungu ni Mwenye kujua vyema vitendo vyenu vyote, na atakulipeni kwavyo.
Ang mga Tafsir na Arabe:
 
Salin ng mga Kahulugan Ayah: (16) Surah: At-Tawbah
Indise ng mga Surah Numero ng Pahina
 
Salin ng mga Kahulugan ng Marangal na Qur'an - الترجمة السواحلية - علي محسن البرواني - Indise ng mga Salin

ترجمة معاني القرآن الكريم إلى اللغة السواحلية، ترجمها علي محسن البرواني.

Isara