Kur'an-ı Kerim meal tercümesi - الترجمة السواحلية - علي محسن البرواني * - Mealler fihristi

XML CSV Excel API
Please review the Terms and Policies

Anlam tercümesi Sure: Sûretu'l-Zelzele   Ayet:

Surat Az-Zalzalah

إِذَا زُلۡزِلَتِ ٱلۡأَرۡضُ زِلۡزَالَهَا
Itakapo tetemeshwa ardhi kwa mtetemeko wake!
Ikitisika ardhi kwa mtikiso mkubwa, na ikasukika kwa ukomo wa kutisika na kusukika kunako mkinika na ikaweza kuchukua!
Arapça tefsirler:
وَأَخۡرَجَتِ ٱلۡأَرۡضُ أَثۡقَالَهَا
Na itakapo toa ardhi mizigo yake!
Na ardhi ikatoa yote yaliomo katika ndani ya tumbo lake, ikiwa khazina au maiti walio kwisha zikwa!
Arapça tefsirler:
وَقَالَ ٱلۡإِنسَٰنُ مَا لَهَا
Na mtu akasema: Ina nini?
Na binaadamu akasema kwa kushtuka na khofu: Ardhi hii ina nini hata inatikisika hivi, na inatoa vilivyomo tumboni mwake, ndio Saa imefika?
Arapça tefsirler:
يَوۡمَئِذٖ تُحَدِّثُ أَخۡبَارَهَا
Siku hiyo itahadithia khabari zake.
Siku hiyo ardhi itamsimulia mtu khabari zake zilio mshitua,
Arapça tefsirler:
بِأَنَّ رَبَّكَ أَوۡحَىٰ لَهَا
Kwa sababu Mola wake Mlezi ameifunulia!
Kwani Mlezi wake na Muumba wake atakuwa kaifunulia, kaipa Wahyi, na kaiamuru itetemeke na ijisuke suke, ndio ikafanya upesi kutekeleza amri.
Arapça tefsirler:
يَوۡمَئِذٖ يَصۡدُرُ ٱلنَّاسُ أَشۡتَاتٗا لِّيُرَوۡاْ أَعۡمَٰلَهُمۡ
Siku hiyo watu watatoka kwa mfarakano wakaonyweshwe vitendo vyao!
Siku hiyo watu watatoka makaburini mbio, nao wamo katika mtafaruku, wapate kuziona hisabu zao na malipo yao aliyo waahidi Mwenyezi Mungu.
Arapça tefsirler:
فَمَن يَعۡمَلۡ مِثۡقَالَ ذَرَّةٍ خَيۡرٗا يَرَهُۥ
Basi anaye tenda chembe ya wema, atauona!
Basi mwenye kufanya hata kitu chenye uzito wa punje ya mchanga cha kheri ataiona katika daftari lake, na atapata malipo yake.
Arapça tefsirler:
وَمَن يَعۡمَلۡ مِثۡقَالَ ذَرَّةٖ شَرّٗا يَرَهُۥ
Na anaye tenda chembe ya uovu atauona!
Na mwenye kufanya shari ya uzito wa chembe ya mchanga ataiona kadhaalika, na atapata malipo yake. Wala Mola wako Mlezi hatamdhulumu yeyote.
Arapça tefsirler:
 
Anlam tercümesi Sure: Sûretu'l-Zelzele
Surelerin fihristi Sayfa numarası
 
Kur'an-ı Kerim meal tercümesi - الترجمة السواحلية - علي محسن البرواني - Mealler fihristi

ترجمة معاني القرآن الكريم إلى اللغة السواحلية، ترجمها علي محسن البرواني.

Kapat