Kwa Jina la Mwenyezi Mungu, Mwingi wa rehema, Mwenye kurehemu.
[1] Bismillaahi inamaanisha, ninaanza "kwa jina la Mwenyezi Mungu." Nayo ipo mwanzoni mwa kila Sura ya Qur-ani isipokuwa Surat Tawba. (Tafsir Aayat Al-Ahkam cha Muhammad bin Ali Assaayis).
Sifa njema zote ni za Mwenyezi Mungu, Mola Mlezi wa walimwengu.[1]
[1] Mola Mlezi ni yule anayewalea walimwengu wote. Nao walimwengu ni kila kisichokuwa Mwenyezi Mungu. Na ulezi wake Mwenyezi Mungu Mtukufu kwa viumbe wake ni wa aina mbili: Wa kiujumla na wa mahususi. Ama wa kiujumla ni kuumba kwake viumbe, kuwapa riziki, na kuwaongoza katika yale yaliyo na masilahi yao. Nao ulezi wake mahususi ni kulea kwake vipenzi wake kwa imani, na kuwawezesha kuifikia, na kuwakamilishia imani hiyo. (Tafsir Assa'dii)
[1] Katika misingi waliyokubaliana juu yake watangulizi wema wa umma huu na maimamu wake ni kuamini kwamba Mwenyezi Mungu ana majina na sifa nzuri. (Tafsir Assa'di)
[1] Kuanzia aya ya kwanza hadi aya hii, ni kana kwamba Mwenyezi Mungu aliyetakasika anasema: "Enyi waja wangu, ikiwa mnanisifu na mnanitukuza kwa sababu ya ukamilifu wa dhati yangu na sifa zangu, basi nisifuni, kwani Mimi kwa hakika ni “Mwenyezi Mungu.” Na ikiwa ni kwa sababu ya wema wangu, na ulezi wangu, na neema zangu, basi Mimi kwa hakika ndiye “Mola Mlezi wa walimwengu.” Na ikiwa ni kwa sababu ya matarajio na matumaini yenu katika siku zijazo, basi mimi kwa hakika ndiye “Mwingi wa Rehema, Mwenye kurehemu.” Na ikiwa ni kwa sababu ya hofu, basi mimi kwa hakika ndiye "Mmiliki wa Siku ya Kiyama." (Tafsiri ya Al-Alusi)
Wewe tu tunakuabudu, na Wewe tu tunakuomba msaada.[1]
[1] Mwenyezi Mungu alitaja kuomba msaada baada ya kutaja ibada ijapokuwa kuomba msaada kunaingia humo (katika ibada); kwa sababu mja katika ibada zake zote anahitaji kuomba msaada wa Mwenyezi Mungu Mtukufu. Kwani, Mwenyezi Mungu asipomsaidia, hatapata anachokitaka kama vile kutekeleza maamrisho na kuacha makatazo. (Tafsir Assa'dii)
[1] Aya hii inajumuisha kubainisha kuwa mja hana njia ya kupata furaha yake (mafanikio) isipokuwa kwa kudumu kwenye njia iliyonyooka. Na kwamba hana njia yoyote ya kumfanya anyooke isipokuwa kwa kuongolewa na Mola wake Mlezi kuifikia; kama vile hana njia yoyote ya kumuabudu isipokuwa kwa msaada wake. Kwa hivyo, hana njia ya kunyooka kwenye njia hiyo (ya uwongofu) isipokuwa kwa uwongofu wake (Mwenyezi Mungu). (Tafsiri ya Ibn al-Qayyim)
Njia ya wale uliowaneemesha. Siyo ya wale waliokasirikiwa, wala waliopotea.[1]
[1] Kisha (Mwenyezi Mungu) akaeleza kuwa njia ya watu wa uwongofu huu ni tofauti na njia ya watu wa waliokasirikiwa na watu wa upotovu. Hivyo basi, viumbe wakagawanyika katika makundi matatu kuhusiana na uwongofu huu: Aliyeneemeshwa kwa kuupata kisha bahati yake katika neema hiyo ikaendelea kulingana na bahati yake katika maelezo yake na migawanyiko yake. Na (kundi la pili) mpotevu ambaye hakupewa uwongofu huu, na wala hakufanikiwa kuupata. Na (kundi la tatu) aliyekasirikiwa; ambaye aliujua (uwongofu) lakini hakuwezeshwa kutenda kama (uwongofu )unavyohitaji. (Tafsiri ya Ibn al-Qayyim)
Kur'an-ı Kerim meal tercümesi - Savahili Dili Tercüme - Rowad Tercüme Merkezi - Mealler fihristi
Rowad Tercüme Merkezi Ekibi tarafından Rabvede'ki Tebliğ, İrşat ve Toplum Bilinçlendirme Derneği ve Dünya dillerinde İslami içerik ve hizmet cemiyeti işbirliğiyle tercüme edilmiştir.
Contents of the translations can be downloaded and re-published, with the following terms and conditions:
1. No modification, addition, or deletion of the content.
2. Clearly referring to the publisher and the source (QuranEnc.com).
3. Mentioning the version number when re-publishing the translation.
4. Keeping the transcript information inside the document.
5. Notifying the source (QuranEnc.com) of any note on the translation.
6. Updating the translation according to the latest version issued from the source (QuranEnc.com).
7. Inappropriate advertisements must not be included when displaying translations of the meanings of the Noble Quran.
Arama sonuçları:
API specs
Endpoints:
Sura translation
GET / https://quranenc.com/api/v1/translation/sura/{translation_key}/{sura_number} description: get the specified translation (by its translation_key) for the speicified sura (by its number)
Parameters: translation_key: (the key of the currently selected translation) sura_number: [1-114] (Sura number in the mosshaf which should be between 1 and 114)
Returns:
json object containing array of objects, each object contains the "sura", "aya", "translation" and "footnotes".
GET / https://quranenc.com/api/v1/translation/aya/{translation_key}/{sura_number}/{aya_number} description: get the specified translation (by its translation_key) for the speicified aya (by its number sura_number and aya_number)
Parameters: translation_key: (the key of the currently selected translation) sura_number: [1-114] (Sura number in the mosshaf which should be between 1 and 114) aya_number: [1-...] (Aya number in the sura)
Returns:
json object containing the "sura", "aya", "translation" and "footnotes".