42 : 68

يَوۡمَ يُكۡشَفُ عَن سَاقٖ وَيُدۡعَوۡنَ إِلَى ٱلسُّجُودِ فَلَا يَسۡتَطِيعُونَ

Siku ya Kiyama, mambo yatakuwa magumu na kitisho chake kitakuwa kikubwa, na hapo Allah Mtukufu atakuja ili kutoa uamuzi baina ya viumbe, atafunua muundi Wake usiofanana na kitu chochote. Amesema mtume, (rehema za Allah Mtukufu na amani zimshukie), «Atafunua Mola wetu muundi Wake, hapo amsujudie kila mwanamume aliyeamini na mwanamke aliyeamini, na atasalia yule aliyekuwa akisujudu duniani kwa kujionesha na kusikika, mgongo wake ukigeuka na ukiwa mfupa mmoja.» Imepokewa na Bukhari na Muslim. info
التفاسير: |
next

Al-Qalam

prev
:
0:00 0:00