Check out the new design

قرآن کریم کے معانی کا ترجمہ - سواحلی ترجمہ - عبد اللہ محمد اور ناصر خمیس * - ترجمے کی لسٹ


معانی کا ترجمہ سورت: قیامہ   آیت:
كَلَّا بَلۡ تُحِبُّونَ ٱلۡعَاجِلَةَ
Mambo sivyo kama mlivyodai, enyi mkusanyiko wa washirikina, kuwa hakuna kufufuliwa wala kulipwa.
عربی تفاسیر:
وَتَذَرُونَ ٱلۡأٓخِرَةَ
Bali nyinyi ni watu mnaopenda dunia na pambo lake na mnaacha Akhera na starehe zake.
عربی تفاسیر:
وُجُوهٞ يَوۡمَئِذٖ نَّاضِرَةٌ
Nyuso za watu wema Siku ya Kiyama zitakuwa ni zenye kung’ara, nzuri na zenye furaha,
عربی تفاسیر:
إِلَىٰ رَبِّهَا نَاظِرَةٞ
zitamuona Mola Aliyeziumba na Anayezimiliki, na zitastarehe kwa hilo.
عربی تفاسیر:
وَوُجُوهٞ يَوۡمَئِذِۭ بَاسِرَةٞ
Nyuso za watu wabaya Silku ya Kiyama zitakuwa ni zenye kukunjana na kusinyaa,
عربی تفاسیر:
تَظُنُّ أَن يُفۡعَلَ بِهَا فَاقِرَةٞ
zinatazamia kushukiwa na msiba mkubwa wenye kuvunja.
عربی تفاسیر:
كَلَّآ إِذَا بَلَغَتِ ٱلتَّرَاقِيَ
Ni kweli! Pindi roho itakapofika sehemu za juu za kifua,
عربی تفاسیر:
وَقِيلَ مَنۡۜ رَاقٖ
na wakasema baadhi ya waliohudhuria kuwaambia wengine, «Je kuna mtu wa kumzungua na kumpoza kutokana na hali hii aliyonayo?»
عربی تفاسیر:
وَظَنَّ أَنَّهُ ٱلۡفِرَاقُ
Na yule ambaye yuko katika hali ya kufa akajua kwamba lile lililomshukia ni kuaga dunia, kwa kuwa anawaona Malaika wa mauti.
عربی تفاسیر:
وَٱلۡتَفَّتِ ٱلسَّاقُ بِٱلسَّاقِ
Na ikashikana shida ya mwisho wa duniani na shida ya mwanzo wa Akhera. Kwa Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka.
عربی تفاسیر:
إِلَىٰ رَبِّكَ يَوۡمَئِذٍ ٱلۡمَسَاقُ
Watu watapelekwa Siku ya Kiyama: ima Peponi au Motoni.
عربی تفاسیر:
فَلَا صَدَّقَ وَلَا صَلَّىٰ
Hakuwa kafiri ni mwenye kumuamini Mtume na Qur’ani, wala hakuwa ni mwenye kumtekelezea Mwenyezi Mungu Aliyetukuka Swala za faradhi.
عربی تفاسیر:
وَلَٰكِن كَذَّبَ وَتَوَلَّىٰ
Lakini aliikanusha Qur’ani na akaipa mgongo Imani,
عربی تفاسیر:
ثُمَّ ذَهَبَ إِلَىٰٓ أَهۡلِهِۦ يَتَمَطَّىٰٓ
kisha akaenda kwa watu wake akijiona hali ya kujigamba katika kutembea kwake. Basi maangamivu
عربی تفاسیر:
أَوۡلَىٰ لَكَ فَأَوۡلَىٰ
ni yako baada ya maangamivu!
عربی تفاسیر:
ثُمَّ أَوۡلَىٰ لَكَ فَأَوۡلَىٰٓ
Kisha maangamivu ni yako baada ya maangamivu!
عربی تفاسیر:
أَيَحۡسَبُ ٱلۡإِنسَٰنُ أَن يُتۡرَكَ سُدًى
Je anadhani huyu binadamu anayekanusha kufufuliwa kuwa ataachwa bure: haamrishwi wala hakatazwi, hahesabiwi wala hateswi?
عربی تفاسیر:
أَلَمۡ يَكُ نُطۡفَةٗ مِّن مَّنِيّٖ يُمۡنَىٰ
Kwani hakuwa binadamu huyu ni tone la manii dhaifu linalotokana na maji matwevu yanayomwagwa na kumiminwa kwenye kizazi,
عربی تفاسیر:
ثُمَّ كَانَ عَلَقَةٗ فَخَلَقَ فَسَوَّىٰ
kisha yakawa ni kipande cha damu iliyo kavu. Mwenyezi Mungu Akaliumba kwa uweza Wake na Akazilinganisha sura zake katika umbo la mwili lililo zuri kabisa?
عربی تفاسیر:
فَجَعَلَ مِنۡهُ ٱلزَّوۡجَيۡنِ ٱلذَّكَرَ وَٱلۡأُنثَىٰٓ
Akafanya kutokana na binadamu huyu jinsi mbili: ya kiume na ya kike. Je kwani hakuwa Mola huyo Muumba wa vitu hivyo ni Muweza wa kuwarudisha viumbe wakiwa hai baada ya kutoweka kwao.
عربی تفاسیر:
أَلَيۡسَ ذَٰلِكَ بِقَٰدِرٍ عَلَىٰٓ أَن يُحۡـِۧيَ ٱلۡمَوۡتَىٰ
Ndio! Anaweza. Yeye, kutakasika na sifa za upungufu ni Kwake, kwa hakika ni Muweza wa hilo.
عربی تفاسیر:
 
معانی کا ترجمہ سورت: قیامہ
سورتوں کی لسٹ صفحہ نمبر
 
قرآن کریم کے معانی کا ترجمہ - سواحلی ترجمہ - عبد اللہ محمد اور ناصر خمیس - ترجمے کی لسٹ

ڈاکٹر عبد اللہ محمد ابو بکر اور شیخ ناصر خمیس نے ترجمہ کیا ہے۔

بند کریں