Bản dịch ý nghĩa nội dung Qur'an - Dịch thuật tiếng Swahili - 'Ali Muhsin Al-Barwani * - Mục lục các bản dịch

XML CSV Excel API
Please review the Terms and Policies

Ý nghĩa nội dung Câu: (68) Chương: Chương Yunus
قَالُواْ ٱتَّخَذَ ٱللَّهُ وَلَدٗاۗ سُبۡحَٰنَهُۥۖ هُوَ ٱلۡغَنِيُّۖ لَهُۥ مَا فِي ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَمَا فِي ٱلۡأَرۡضِۚ إِنۡ عِندَكُم مِّن سُلۡطَٰنِۭ بِهَٰذَآۚ أَتَقُولُونَ عَلَى ٱللَّهِ مَا لَا تَعۡلَمُونَ
Wamesema: Mwenyezi Mungu ana mwana. Subhanahu, Aliye takasika! Yeye ni Mkwasi, Mwenye Kujitosheleza. Vyote viliomo katika mbingu na katika ardhi ni vyake peke yake. Nyinyi hamna uthibitisho wowote wa haya! Mnamzulia Mwenyezi Mungu msiyo yajua?
Na ikiwa wanao abudu masanamu wamefanya ushirikina wa kuabudu mawe, na hawakumtakasa Mwenyezi Mungu kwa haki ya kumtakasa, na wakasema kuwa Allah, Mwenyezi Mungu, ana mwana, basi Mwenyezi Mungu ametakasika na hayo. Yeye hana haja ya kuwa na mwana; kwani kuwa na mwana kunaonyesha wazi kutaka kubakia ukoo wako baada ya kufa kwako. Na Mwenyezi Mungu hafi. Yeye ni Mwenye kubakia milele. Na vyote viliomo katika mbingu na viliomo katika ardhi ni vyake, vimeumbwa na vinaendeshwa na Yeye. Na nyinyi wazushi, hamna hoja yoyote wala dalili ya hayo mnayo zua! Basi msikhitalifiane juu ya Mwenyezi Mungu kwa mambo yasiyo na msingi wa hakika.
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
 
Ý nghĩa nội dung Câu: (68) Chương: Chương Yunus
Mục lục các chương Kinh Số trang
 
Bản dịch ý nghĩa nội dung Qur'an - Dịch thuật tiếng Swahili - 'Ali Muhsin Al-Barwani - Mục lục các bản dịch

Bản dịch ý nghĩa nội dung Kinh Qur'an bằng tiếng Swahili do 'Ali Muhsin Al-Barwani dịch thuật

Đóng lại