Basi ilipo fika amri yetu tuliigeuza nchi juu chini, na tukawateremshia mvua ya changarawe za udongo mgumu ulio kamatana wa Motoni,
Ulipo fika wakati wa adhabu tuliyo ikadiria na tukaitolea hukumu, tuliupindua mji ule walio kuwa wakiishi ndani kaumu Lut' juu chini. Na tukawanyeshea mvua ya mawe ya udongo ulio okwa Motoni hata ukawa changarawe!
Zilizo tiwa alama kwa Mola wako Mlezi. Na haya hayako mbali na wenye kudhulumu wengineo.
Wakawa wanaangukiwa na hayo mawe mfululizo kuwa ni adhabu inayo toka kwa Mola wako Mlezi, ewe Nabii! Na hayo si mbali kumfikilia kila mwenye kudhulumu katika kaumu yako.
Na kwa watu wa Madyana tuliwatumia ndugu yao Shua'ib. Akasema: Enyi watu wangu! Muabuduni Mwenyezi Mungu. Nyinyi hamna Mungu ila Yeye, wala msipunguze vipimo na mizani. Mimi nakuoneni mmo katika hali njema, nami nakukhofieni adhabu ya Siku kubwa hiyo itakayo kuzungukeni.
Na kwa watu wa Madyana tulimtuma ndugu yao kwa nasaba na mapenzi na kuoneana huruma, Shua'ib. Aliwaambia: Enyi watu wangu! Muabuduni Mwenyezi Mungu Mmoja peke yake. Nyinyi hamna anaye stahiki kuabudiwa isipo kuwa Yeye. Wala msipunguze vipimo na mizani mnapo wauzia watu vitu vya kupimwa kwa pishi au kwa mizani. Hakika mimi nakuoneni ni watu wa kutarajiwa kheri kwa kumshukuru na kumt'ii Mwenyezi Mungu, na kuwapa watu haki zao kaamili. Na mimi nakukhofieni ikiwa hamtaishukuru kheri ya Mwenyezi Mungu na hamuitikii amri yake, isije ikakuteremkieni adhabu ya siku msio weza kuvikimbia vitisho vyake, kwa kuwa hivyo huwazinga wanao adhibiwa wasipate njia ya kusalimika. Hizi Aya mbili zinakataza kupunja kwa vipimo na mizani kwa kuwa ni ukhalifu unao stahiki kupewa adhabu na kuaziriwa. Makosa haya ya kupunja na udanganyifu pia yanahisabiwa ni ukhalifu hata katika kanuni za kutungwa za dikrii. Na katika Qur'ani tukufu ni moja katika njia ya kulinda mali. Nchi ya Madyana ipo baina ya kaskazi ya Hijazi na kusini ya Sham. Na hii ilikuwa imejaa miti. Ikiitwa Al-aykah,(yaani Machakani). Na Mwenyezi Mungu aliwapelekea adhabu kwa sababu ya uasi wao.
Na enyi watu wangu! Timizeni vipimo na mizani kwa uadilifu wala msiwakhini watu vitu vyao; wala msieneze uovu katika nchi mkafanya uharibifu.
Enyi watu wangu! Toeni vipimo na mizani sawa na kwa uadilifu pale mnapo uza, wala msiwapunje watu vitu vyao, wala msifanye ujeuri na fisadi katika nchi kwa kwiba mali ya watu na kupokonya, au kuvamia wapita njia, mkifanya fisadi ndio chumo la maisha yenu
Alivyo kubakishieni Mwenyezi Mungu ndiyo bora kwa ajili yenu, ikiwa nyinyi ni Waumini. Wala mimi siye mlinzi wenu.
Kidogo kinacho kuzidieni katika mali ya halali aliyo kuruzukuni Mwenyezi Mungu ni bora kwenu kuliko chungu ya mali mnayo yakusanya kwa njia ya haramu, ikiwa nyinyi kweli mnamuamini Mwenyezi Mungu, na mnaepuka aliyo kukatazeni. Basi jipimeni nafsi zenu, na mumuangalie Mola wenu Mlezi. Mimi si mlinzi wenu wa kuchunga vitendo vyenu na kukupimieni.
Wakasema: Ewe Shua'ibu! Ni swala zako ndizo zinazo kuamrisha tuyaache waliyo kuwa wakiyaabudu baba zetu, au tuache kufanya tupendavyo katika mali zetu? Ama hakika wewe ni mstahamilivu kweli na mwongofu!
Wakasema kwa maskhara na kukejeli: Ewe Shua'ibu! Hivyo ni hizo swala zako ndizo zinazo kuamrisha kutushikilia tuache kuabudu masanamu waliyo kuwa wakiyaabudu baba zetu, na tuache kustarehe kutumia mali zetu kama tunavyoona wenyewe kuwa ni maslaha yetu? Hakika huo ndio mwisho wa upumbavu na utovu wa akili, wala haulingani na akili na rai njema tunazo kujua unazo; kwani wewe ni maarufu kwa ustahamilivu wako na uwongofu wako!
Akasema: Enyi watu wangu! Mwaonaje ikiwa ninayo dalili wazi inayo tokana na Mola wangu Mlezi, na ikawa Yeye ameniruzuku riziki njema kutoka kwake? Wala mimi sipendi kukukhalifuni nikafanya yale ninayo kukatazeni. Sitaki ila kutengeneza kiasi ninavyo weza. Na sipati kuwezeshwa haya ila na Mwenyezi Mungu. Kwake Yeye ninategemea, na kwake Yeye naelekea.
Yeye akasema: Enyi watu! Hebu nambieni, ikiwa mimi nina hoja iliyo wazi na ya yakini kutokana na Mola Mlezi wangu, naye akaniruzuku kwa fadhila yake riziki iliyo njema, je ingeli nifalia mimi nifiche aliyo niamrisha kukufikishieni, nako ni kuacha kuabudu masanamu, na kukutakeni mtimize vipimo na mizani, na muache kufanya uharibifu katika nchi? Na mimi si kama ninapenda kwenda kutenda haya ninayo kukatazeni, wala sitaki kwa mawaidha yangu, na nasaha zangu, na amri zangu, na makatazo yangu, ila kutengeneza kwa kadri ya ukomo wa uwezo wangu, na juhudi yangu, kama nilivyo jaaliwa. Wala sina uwezo wa kuifikilia haki ila kwa msaada wa Mwenyezi Mungu na kuungwa mkono naye, na ninamtegemea Yeye peke yake. Na kwake Yeye tu ndio ninarejea.
Contents of the translations can be downloaded and re-published, with the following terms and conditions:
1. No modification, addition, or deletion of the content.
2. Clearly referring to the publisher and the source (QuranEnc.com).
3. Mentioning the version number when re-publishing the translation.
4. Keeping the transcript information inside the document.
5. Notifying the source (QuranEnc.com) of any note on the translation.
6. Updating the translation according to the latest version issued from the source (QuranEnc.com).
7. Inappropriate advertisements must not be included when displaying translations of the meanings of the Noble Quran.
Kết quả tìm kiếm:
API specs
Endpoints:
Sura translation
GET / https://quranenc.com/api/v1/translation/sura/{translation_key}/{sura_number} description: get the specified translation (by its translation_key) for the speicified sura (by its number)
Parameters: translation_key: (the key of the currently selected translation) sura_number: [1-114] (Sura number in the mosshaf which should be between 1 and 114)
Returns:
json object containing array of objects, each object contains the "sura", "aya", "translation" and "footnotes".
GET / https://quranenc.com/api/v1/translation/aya/{translation_key}/{sura_number}/{aya_number} description: get the specified translation (by its translation_key) for the speicified aya (by its number sura_number and aya_number)
Parameters: translation_key: (the key of the currently selected translation) sura_number: [1-114] (Sura number in the mosshaf which should be between 1 and 114) aya_number: [1-...] (Aya number in the sura)
Returns:
json object containing the "sura", "aya", "translation" and "footnotes".