Bản dịch ý nghĩa nội dung Qur'an - Dịch thuật tiếng Swahili - 'Ali Muhsin Al-Barwani * - Mục lục các bản dịch

XML CSV Excel API
Please review the Terms and Policies

Ý nghĩa nội dung Câu: (59) Chương: Chương Al-Isra'
وَمَا مَنَعَنَآ أَن نُّرۡسِلَ بِٱلۡأٓيَٰتِ إِلَّآ أَن كَذَّبَ بِهَا ٱلۡأَوَّلُونَۚ وَءَاتَيۡنَا ثَمُودَ ٱلنَّاقَةَ مُبۡصِرَةٗ فَظَلَمُواْ بِهَاۚ وَمَا نُرۡسِلُ بِٱلۡأٓيَٰتِ إِلَّا تَخۡوِيفٗا
Na hapana kinacho tuzuia kupeleka miujiza ila ni kuwa watu wa zamani waliikanusha. Na tuliwapa Wathamudi ngamia jike kuwa ni Ishara iliyo dhaahiri, lakini walidhulumu kwaye. Nasi hatupeleki Ishara ila kwa ajili ya kuhadharisha.
Watu wako wamekutaka uwaletee Ishara na miujiza. Nao hawakukinaika kwa yaliyo wajia ambayo huwakinaisha wenye akili. Na mwendo wetu umekwisha wapitia hao wanao taka miujiza, na wanapo kubaliwa wasiamini, nao ni kuwang'olea mbali kwa adhabu kama tulivyo wafanyia wa kale. Miongoni mwa hao ni watu wa Thamud. Walitaka miujiza, akawa ngamia mke ni muujiza wazi kwao wa kuondoa shaka zote. Wakamkanusha, yakatokea kwao yaliyo tokea! Na imekuwa hikima ya Mwenyezi Mungu kuwa asiwakubalie hayo waliyo yataka, kwa kuchelea wasiikatae miujiza, kwa kutarajia watakuja amini miongoni mwao, au watakuja zaa watakao amini. Na miujiza hakika Sisi huwapelekea watu kwa kuwatia khofu na kitisho.
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
 
Ý nghĩa nội dung Câu: (59) Chương: Chương Al-Isra'
Mục lục các chương Kinh Số trang
 
Bản dịch ý nghĩa nội dung Qur'an - Dịch thuật tiếng Swahili - 'Ali Muhsin Al-Barwani - Mục lục các bản dịch

Bản dịch ý nghĩa nội dung Kinh Qur'an bằng tiếng Swahili do 'Ali Muhsin Al-Barwani dịch thuật

Đóng lại