Bản dịch ý nghĩa nội dung Qur'an - Dịch thuật tiếng Swahili - 'Ali Muhsin Al-Barwani * - Mục lục các bản dịch

XML CSV Excel API
Please review the Terms and Policies

Ý nghĩa nội dung Câu: (212) Chương: Chương Al-Baqarah
زُيِّنَ لِلَّذِينَ كَفَرُواْ ٱلۡحَيَوٰةُ ٱلدُّنۡيَا وَيَسۡخَرُونَ مِنَ ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْۘ وَٱلَّذِينَ ٱتَّقَوۡاْ فَوۡقَهُمۡ يَوۡمَ ٱلۡقِيَٰمَةِۗ وَٱللَّهُ يَرۡزُقُ مَن يَشَآءُ بِغَيۡرِ حِسَابٖ
Walio kufuru wamepambiwa maisha ya duniani; na wanawafanyia maskhara walio amini. Na wenye kuchamngu watakuwa juu yao Siku ya Kiyama. Na Mwenyezi Mungu humruzuku amtakaye bila ya hisabu.
Na sababu ya kupotoka na kukufuru ni kuitaka dunia. Wale walio kufuru wamepambiwa matamanio ya maisha ya kidunia wakawa wanawakejeli wale walio amini kwa kushughulikia kwao maisha ya Akhera. Na Mwenyezi Mungu atawaweka walio amini pahala pa juu kabisa kuliko wao katika Akhera. Ama kuwa hawa makafiri wana mali zaidi na mapambo ya kidunia hakuonyeshi ubora wao, kwani riziki ya Mwenyezi Mungu haipimwi kwa mujibu wa kuamini na kukufuru, bali inakwenda kama apendavyo Yeye mwenyewe. Wapo watu huzidishiwa hiyo riziki kwa "Istidraaji" kumpururia kamba tu, na wapo wanao nyimwa neema za dunia kama ni mtihani, majaribio.
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
 
Ý nghĩa nội dung Câu: (212) Chương: Chương Al-Baqarah
Mục lục các chương Kinh Số trang
 
Bản dịch ý nghĩa nội dung Qur'an - Dịch thuật tiếng Swahili - 'Ali Muhsin Al-Barwani - Mục lục các bản dịch

Bản dịch ý nghĩa nội dung Kinh Qur'an bằng tiếng Swahili do 'Ali Muhsin Al-Barwani dịch thuật

Đóng lại