Check out the new design

Bản dịch ý nghĩa nội dung Qur'an - 斯瓦西里语翻译 - 阿里·穆哈辛·拜拉瓦尼 * - Mục lục các bản dịch

XML CSV Excel API
Please review the Terms and Policies

Ý nghĩa nội dung Chương: Al-Zukhruf   Câu:
وَمَا نُرِيهِم مِّنۡ ءَايَةٍ إِلَّا هِيَ أَكۡبَرُ مِنۡ أُخۡتِهَاۖ وَأَخَذۡنَٰهُم بِٱلۡعَذَابِ لَعَلَّهُمۡ يَرۡجِعُونَ
Na hatukuwaonyesha Ishara yoyote ila hiyo ilikuwa kubwa zaidi kuliko nyenginewe. Na tukawakamata kwa adhabu ili warejee.
Na kila muujiza katika miujiza iliyo wajia mfululizo, kwa uwazi wa hoja zake juu ya ukweli wa Mtume, na kuwa kila mmoja peke yake unatimiza makusudio hayo kwa ukamilifu wa kila njia, na ukamilifu wa nafsi yake, hata ukiuangalia waweza kusema: Muujiza huu ni mkubwa kuliko ule mwengine. Na walipo shikilia kuendelea na uasi tuliwapatiliza kwa balaa za namna kwa namna, ili warejee, waache upotovu wao.
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
وَقَالُواْ يَٰٓأَيُّهَ ٱلسَّاحِرُ ٱدۡعُ لَنَا رَبَّكَ بِمَا عَهِدَ عِندَكَ إِنَّنَا لَمُهۡتَدُونَ
Na wakasema: Ewe mchawi! Tuombee kwa Mola wako Mlezi kwa ile ahadi aliyo kuahidi; hakika sisi tutakuwa wenye kuongoka.
Wakasema, kumlilia Musa balaa zilipo waenea: Ewe mchawi - ndio Mwanachuoni kikwao - Tuombee kwa Mola wako Mlezi, kwa kutawasali na ahadi yake aliyo kupa, atuondolee adhabu hii! Hakika sisi tukifarijiwa bila ya shaka tutaongoka.
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
فَلَمَّا كَشَفۡنَا عَنۡهُمُ ٱلۡعَذَابَ إِذَا هُمۡ يَنكُثُونَ
Basi tulipo waondolea adhabu hiyo, mara wakaingia kuvunja ahadi.
Mwenyezi Mungu alipo waondolea masaibu yale kwa kuitikia dua za Musa, wakamshitukia kwa kuvunja ile ahadi yao ya kuamini.
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
وَنَادَىٰ فِرۡعَوۡنُ فِي قَوۡمِهِۦ قَالَ يَٰقَوۡمِ أَلَيۡسَ لِي مُلۡكُ مِصۡرَ وَهَٰذِهِ ٱلۡأَنۡهَٰرُ تَجۡرِي مِن تَحۡتِيٓۚ أَفَلَا تُبۡصِرُونَ
Na Firauni alitangaza kwa watu wake, akisema: Enyi watu wangu! Kwani mimi sinao huu ufalme wa Misri, na hii mito inapita chini yangu? Je! Hamwoni?
Firauni akawatangazia watu wake kutangaza nguvu zake na madaraka yake: Kwani huu ufalme wa Misri si wangu mimi peke yangu, wala hapana mwenginewe, na hii mito ambayo mnaiona inapita chini ya jumba langu? Hamyaoni haya? Basi hamzingatii mnayo yaona ya nguvu zangu na udhaifu wa Musa? Na Firauni alitaka kwa wito wake kuutia imara ut'iifu wao.
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
أَمۡ أَنَا۠ خَيۡرٞ مِّنۡ هَٰذَا ٱلَّذِي هُوَ مَهِينٞ وَلَا يَكَادُ يُبِينُ
Au mimi si bora kuliko huyu aliye mnyonge, wala hawezi kusema waziwazi?
Firauni akasema akizidisha ujabari: Bali mimi ni bora kuliko dhaifu huyu mnnyonge, asiye weza hata kubainisha wazi huo wito wake kwa ulimi wa fasaha.
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
فَلَوۡلَآ أُلۡقِيَ عَلَيۡهِ أَسۡوِرَةٞ مِّن ذَهَبٍ أَوۡ جَآءَ مَعَهُ ٱلۡمَلَٰٓئِكَةُ مُقۡتَرِنِينَ
Basi mbona hakuvikwa vikuku vya dhahabu, au hawakuja Malaika pamoja naye wakamwandama?
Akazidi kusema kuchochea kumkadhibisha Musa: Lau ingeli kuwa Mola wake Mlezi angeli mvika vikuku vya dhahabu kwa kumpa funguo za utawala, au akamsaidia kwa Malaika wa kumuunga mkono, ingeli kuwa yeye ni mkweli katika madai yake ya Utume?
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
فَٱسۡتَخَفَّ قَوۡمَهُۥ فَأَطَاعُوهُۚ إِنَّهُمۡ كَانُواْ قَوۡمٗا فَٰسِقِينَ
Basi aliwachezea watu wake, na wakamt'ii. Kwa hakika hao walikuwa watu wapotovu.
Firauni akawa anawachochea watu wake, na akawaathiri kwa udanganyifu huu, nao wakamt'ii katika upotovu wake. Kwani hao walikuwa watu walio kwisha toka kwenye Dini ya Mwenyezi Mungu Iliyo Nyooka.
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
فَلَمَّآ ءَاسَفُونَا ٱنتَقَمۡنَا مِنۡهُمۡ فَأَغۡرَقۡنَٰهُمۡ أَجۡمَعِينَ
Walipo tukasirisha tuliwapatiliza tukawazamisha wote!
Basi walipo tughadhibisha hadi ya kutughadhibisha, kwa kupita kwao mipaka ya ufisadi, tuliwaangamiza kwa kuwazamisha wote.
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
فَجَعَلۡنَٰهُمۡ سَلَفٗا وَمَثَلٗا لِّلۡأٓخِرِينَ
Walipo tukasirisha tuliwapatiliza tukawazamisha wote!
Tukamfanya Firauni na kaumu yake kuwa ni viongozi wa makafiri wa baada yao katika kustahiki mfano wa adhabu yao, na kuwa ni masimulizi ya namna ya ajabu ya watu wote kuyazingatia.
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
۞ وَلَمَّا ضُرِبَ ٱبۡنُ مَرۡيَمَ مَثَلًا إِذَا قَوۡمُكَ مِنۡهُ يَصِدُّونَ
Na alipo pigiwa mfano Mwana wa Mariamu, watu wako waliupiga ukelele.
Na alipo pigiwa mfano Isa bin Maryam katika kuwa kwake kama Adam kwa kuwa Mwenyezi Mungu alimuumba kwa udongo, kisha akamwambia: Kuwa, na akawa, subhanallah. Basi yeye ni mtumwa aliye umbwa, aliye neemeshwa kwa kupewa Unabii, subhanallah. Haifai kumuabudu badala ya Mwenyezi Mungu. Na watu wako wanapuuza hizo sifa zinazo pigiwa mfano, na wala hawafahamu.
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
وَقَالُوٓاْ ءَأَٰلِهَتُنَا خَيۡرٌ أَمۡ هُوَۚ مَا ضَرَبُوهُ لَكَ إِلَّا جَدَلَۢاۚ بَلۡ هُمۡ قَوۡمٌ خَصِمُونَ
Wakasema: Miungu yetu kwani si bora kuliko huyu? Hawakukupigia mfano huo ila kwa ubishi tu. Bali hao ni watu wagomvi!
Makafiri wamesema: Je! Miungu yetu na Isa, nani bora? Ikiwa yeye yuko Motoni basi sisi na miungu yetu tutakuwa pamoja naye. Hawakupigii mfano huu wewe ila kutafuta ubishi tu, na kushindana kwa maneno, si kwa ajili ya kuitafuta kweli ilivyo. Bali hawa ni watu ambao ni shadidi wa khasama, wamebobea kwa hayo.
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
إِنۡ هُوَ إِلَّا عَبۡدٌ أَنۡعَمۡنَا عَلَيۡهِ وَجَعَلۡنَٰهُ مَثَلٗا لِّبَنِيٓ إِسۡرَٰٓءِيلَ
Hakuwa yeye (Isa) ila ni Mtumwa tuliye mneemesha na tukamfanya ni mfano kwa Wana wa Israili.
Isa si chochote ila ni mja tuliye mneemesha kwa kumpa Unabii, na tumemfanya awe ni zingatio la ajabu kama ni mithali, kwa kumuumba bila ya baba, kwa Wana wa Israili, wapate ushahidi wa ukamilifu wa uweza wetu.
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
وَلَوۡ نَشَآءُ لَجَعَلۡنَا مِنكُم مَّلَٰٓئِكَةٗ فِي ٱلۡأَرۡضِ يَخۡلُفُونَ
Na tungeli penda tungeli wafanyia miongoni mwenu Malaika katika ardhi wakifuatana.
Na lau tungeli taka, tungeli wageuza baadhi yenu, enyi watu, mkawa ni Malaika mkifuatana katika ardhi, kama wanavyo kufuateni watoto wenu, mjue kwamba Malaika wananyenyekea kufuata kudra ya Mwenyezi Mungu. Basi vipi wao wastahiki Ungu?
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
 
Ý nghĩa nội dung Chương: Al-Zukhruf
Mục lục các chương Kinh Số trang
 
Bản dịch ý nghĩa nội dung Qur'an - 斯瓦西里语翻译 - 阿里·穆哈辛·拜拉瓦尼 - Mục lục các bản dịch

阿里·穆哈辛·拜拉瓦尼翻译

Đóng lại