Bản dịch ý nghĩa nội dung Qur'an - Dịch thuật tiếng Swahili - 'Ali Muhsin Al-Barwani * - Mục lục các bản dịch

XML CSV Excel API
Please review the Terms and Policies

Ý nghĩa nội dung Câu: (11) Chương: Chương Al-Anfal
إِذۡ يُغَشِّيكُمُ ٱلنُّعَاسَ أَمَنَةٗ مِّنۡهُ وَيُنَزِّلُ عَلَيۡكُم مِّنَ ٱلسَّمَآءِ مَآءٗ لِّيُطَهِّرَكُم بِهِۦ وَيُذۡهِبَ عَنكُمۡ رِجۡزَ ٱلشَّيۡطَٰنِ وَلِيَرۡبِطَ عَلَىٰ قُلُوبِكُمۡ وَيُثَبِّتَ بِهِ ٱلۡأَقۡدَامَ
Alipo kufunikeni kwa usingizi uwe ni uaminisho kutoka kwake, na akakuteremshieni maji kutoka mbinguni ili kukusafisheni kwayo na kukuondoleeni uchafu wa Shet'ani, na kuzipa nguvu nyoyo zenu, na kuitia imara miguu yenu.
Enyi Waumini! Kumbukeni wakati mlipo ingiwa khofu kwa upungufu wa maji, na kuwaogopa maadui. Mwenyezi Mungu alikupeni utulivu, kwa kukuleteeni usingizi, mkalala mkatua. Akakuteremshieni maji kutoka mbinguni mkajisafishia, na mkauondoa wasiwasi wa Shetani, na nyoyo zenu zikawa imara kwa msaada wa Rahmani na pia ardhi ikashikamana kwa hayo maji, na miguu yenu ikaweza kukanyaga bila ya kudidimia katika mchanga. Aya hii inaashiria fadhila ya Mwenyezi Mungu Mtukufu juu ya wapiganaji Waumini kwa kupatikana hali ya amani kwa kupumzika kwa usingizi, na kuteremka mvua kwa kujitahirisha na kukoga, na kushikamana mchanga kwa kuwepo maji, basi nyayo zikasimama imara. Inajuulikana kuwa mchanga laini unawaletea taabu wapiganaji na unakuwa pingamizi katika kwenda huku na huko ambako ni katika dharura za vita muhimu. Na aya ya pili inaeleza maneno ya Mwenyezi Mungu Mtukufu kuwaambia Malaika wawathibitishe Waumini na watie khofu katika nyoyo za makafiri. Na ni maarufu kuwa khofu ikiwatawala askari katika midani huwaletea kuemewa. Na katika Aya hii tukufu panaashiriwa pahali pa kupiga napo ni juu ya shingo na kuvikata vidole vinavyo kamata silaha mkononi.
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
 
Ý nghĩa nội dung Câu: (11) Chương: Chương Al-Anfal
Mục lục các chương Kinh Số trang
 
Bản dịch ý nghĩa nội dung Qur'an - Dịch thuật tiếng Swahili - 'Ali Muhsin Al-Barwani - Mục lục các bản dịch

Bản dịch ý nghĩa nội dung Kinh Qur'an bằng tiếng Swahili do 'Ali Muhsin Al-Barwani dịch thuật

Đóng lại