《古兰经》译解 - 斯瓦希里语翻译 - 阿布杜拉·穆罕默德和纳赛尔·海米斯。 * - 译解目录


含义的翻译 段: (221) 章: 拜格勒
وَلَا تَنكِحُواْ ٱلۡمُشۡرِكَٰتِ حَتَّىٰ يُؤۡمِنَّۚ وَلَأَمَةٞ مُّؤۡمِنَةٌ خَيۡرٞ مِّن مُّشۡرِكَةٖ وَلَوۡ أَعۡجَبَتۡكُمۡۗ وَلَا تُنكِحُواْ ٱلۡمُشۡرِكِينَ حَتَّىٰ يُؤۡمِنُواْۚ وَلَعَبۡدٞ مُّؤۡمِنٌ خَيۡرٞ مِّن مُّشۡرِكٖ وَلَوۡ أَعۡجَبَكُمۡۗ أُوْلَٰٓئِكَ يَدۡعُونَ إِلَى ٱلنَّارِۖ وَٱللَّهُ يَدۡعُوٓاْ إِلَى ٱلۡجَنَّةِ وَٱلۡمَغۡفِرَةِ بِإِذۡنِهِۦۖ وَيُبَيِّنُ ءَايَٰتِهِۦ لِلنَّاسِ لَعَلَّهُمۡ يَتَذَكَّرُونَ
Wala msiwaoe, enyi Waislamu, wanawake washirikina wanaoabudu masanamu mpaka waingie katika Uislamu. Na mjue kwamba mwanamke kijakazi, asiyekuwa na mali wala utukufu wa nasaba, anayemuamini Mwenyezi Mungu, ni bora kuliko mwanamke mshirikina, hata kama huyo mshirikina muungwana atawavutia. Wala msiwaoze wanawake wenu waumini, wakiwa ni vijakazi au waungwana, wanaume washirikina mpaka wamuamini Mwenyezi Mungu na Mtume Wake. Na mjue kwamba mtumwa mwenye Imani, pamoja na ufukara wake, ni bora kuliko mshirikina, hata kama huyo mshirikina atawavutia. Hao wasifikao na ushirikina, wanaume na wanawake, wanamwita kila atangamanaye nao kwenye mambo yapelekayo Motoni. Na Mwenyezi Mungu, Aliyetakasika na kila sifa ya upungufu, Anawaita waja Wake kwenye dini Yake ya haki inayowapeleka Peponi na kusamehawa madhambi yao kwa idhini Yake. Na Yeye Anabainisha aya Zake na hukumu Zake kwa watu, ili wapate kukumbuka na wazingatie.
阿拉伯语经注:
 
含义的翻译 段: (221) 章: 拜格勒
章节目录 页码
 
《古兰经》译解 - 斯瓦希里语翻译 - 阿布杜拉·穆罕默德和纳赛尔·海米斯。 - 译解目录

古兰经斯瓦希里文译解,阿布杜拉·穆罕默德·艾布·拜克尔博士和谢赫纳赛尔·哈米斯翻译。

关闭