《古兰经》译解 - 斯瓦希里语翻译 - 阿布杜拉·穆罕默德和纳赛尔·海米斯。 * - 译解目录


含义的翻译 段: (4) 章: 拜格勒
وَٱلَّذِينَ يُؤۡمِنُونَ بِمَآ أُنزِلَ إِلَيۡكَ وَمَآ أُنزِلَ مِن قَبۡلِكَ وَبِٱلۡأٓخِرَةِ هُمۡ يُوقِنُونَ
Na wao ndio ambao wanayaamini yaliyoteremshwa kwako, ewe Mtume, ya Qurani, na yalioteremshwa kwako ya hekima, ambayo ni Sunnah, na Vitabu vyote vilivyoteremshwa kwa Mitume kabla yako, kama Taurati, Injil na vinginevyo, na wanaiamini Nyumba ya Maisha baada ya kufa na yaliyomo ndani ya Nyumba hiyo ya kuhesabiwa na kulipwa. Wanaamini hayo kwa nyoyo zao, imani ya kidhati inayodhihiri kwenye ndimi zao na viungo vyao. Kutajwa Siku ya Mwisho mahususi ni kwa sababu kuiamini ni mojawapo ya vitu vikubwa zaidi vyenye kusukuma na kuhimiza kufanya vitendo vya kumtii Mwenyezi Mungu, kujiepusha na vitendo vya haramu na kuifanyia hesabu nafsi.
阿拉伯语经注:
 
含义的翻译 段: (4) 章: 拜格勒
章节目录 页码
 
《古兰经》译解 - 斯瓦希里语翻译 - 阿布杜拉·穆罕默德和纳赛尔·海米斯。 - 译解目录

古兰经斯瓦希里文译解,阿布杜拉·穆罕默德·艾布·拜克尔博士和谢赫纳赛尔·哈米斯翻译。

关闭