《古兰经》译解 - 斯瓦希里语翻译 - 阿布杜拉·穆罕默德和纳赛尔·海米斯。 * - 译解目录


含义的翻译 段: (127) 章: 尼萨仪
وَيَسۡتَفۡتُونَكَ فِي ٱلنِّسَآءِۖ قُلِ ٱللَّهُ يُفۡتِيكُمۡ فِيهِنَّ وَمَا يُتۡلَىٰ عَلَيۡكُمۡ فِي ٱلۡكِتَٰبِ فِي يَتَٰمَى ٱلنِّسَآءِ ٱلَّٰتِي لَا تُؤۡتُونَهُنَّ مَا كُتِبَ لَهُنَّ وَتَرۡغَبُونَ أَن تَنكِحُوهُنَّ وَٱلۡمُسۡتَضۡعَفِينَ مِنَ ٱلۡوِلۡدَٰنِ وَأَن تَقُومُواْ لِلۡيَتَٰمَىٰ بِٱلۡقِسۡطِۚ وَمَا تَفۡعَلُواْ مِنۡ خَيۡرٖ فَإِنَّ ٱللَّهَ كَانَ بِهِۦ عَلِيمٗا
Watu wanakutaka, ewe Nabii, uwaelezee mambo yaliyowatatiza kuyafahamu yanayowahusu wanawake na hukumu zao. Sema, «Mwenyezi Mungu Anawafafanulia kuhusu mambo yao na yale mnayosomewa ndani ya Qur’ani kuhusu mayatima wa kike ambao hamuwapi mafungu yao waliyoandikiwa na Mwenyezi Mungu ya mahari, mirathi na haki nyiginezo, na mkawa mnapenda kuwaoa au hamuna hamu ya kuwaoa. Na pia Mwenyezi Mungu Anawafafanulia kuhusu mambo ya madhaifu miongoni mwa watoto na ulazima wa kuwasimamia mayatima kwa uadilifu na kuacha kuwafanyia maonevu kwa kuwanyima haki zao. Na wema wowote mnaoufanya, Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka, Anaujua, hakuna kinachofichika Kwake kuhuso huo na mwengineo.
阿拉伯语经注:
 
含义的翻译 段: (127) 章: 尼萨仪
章节目录 页码
 
《古兰经》译解 - 斯瓦希里语翻译 - 阿布杜拉·穆罕默德和纳赛尔·海米斯。 - 译解目录

古兰经斯瓦希里文译解,阿布杜拉·穆罕默德·艾布·拜克尔博士和谢赫纳赛尔·哈米斯翻译。

关闭