《古兰经》译解 - 斯瓦希里语翻译 - 阿布杜拉·穆罕默德和纳赛尔·海米斯。 * - 译解目录


含义的翻译 段: (95) 章: 玛仪戴
يَٰٓأَيُّهَا ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ لَا تَقۡتُلُواْ ٱلصَّيۡدَ وَأَنتُمۡ حُرُمٞۚ وَمَن قَتَلَهُۥ مِنكُم مُّتَعَمِّدٗا فَجَزَآءٞ مِّثۡلُ مَا قَتَلَ مِنَ ٱلنَّعَمِ يَحۡكُمُ بِهِۦ ذَوَا عَدۡلٖ مِّنكُمۡ هَدۡيَۢا بَٰلِغَ ٱلۡكَعۡبَةِ أَوۡ كَفَّٰرَةٞ طَعَامُ مَسَٰكِينَ أَوۡ عَدۡلُ ذَٰلِكَ صِيَامٗا لِّيَذُوقَ وَبَالَ أَمۡرِهِۦۗ عَفَا ٱللَّهُ عَمَّا سَلَفَۚ وَمَنۡ عَادَ فَيَنتَقِمُ ٱللَّهُ مِنۡهُۚ وَٱللَّهُ عَزِيزٞ ذُو ٱنتِقَامٍ
Enyi ambao mlimuamini Mwenyezi Mungu, Mtume Wake na mkafuata sheria Zake kivitendo, msiue viwindwa wa barani na nyinyi muko kwenye ihramu ya Hija au Umra au mkawa muko ndani ya Haram. Na yoyote mwenye kuua kiwindwa yoyote kati ya viwindwa wa barani kwa kusudi, basi malipo yake ni achinje, miongoni mwa wanyama- howa: ngamia au ng’ombe au mbuzi na kondoo, anayefanana na kiwindwa huyo, baada ya waadilifu wawili kumfanyia makadirio, na amgawe kwa masikini wa eneo la Ḥarām au anunue chakula kwa thamani ya mfano wake na awagawie masikini wa eneo la Haram, kila masikini nusu pishi au afunge, badala yake, siku moja kwa kila nusu pishi ya chakula hicho. Mwenyezi Mungu Ameyapasisha malipo haya , ili mkosa apate matokeo ya kitendo chake. Na wale ambao ilitukia kwao kufanya lolote kama hilo kabla ya kuharamishwa, basi Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka, Ashawasamehe. Na yoyote mwenye kurudia uhalifu huo kwa kusudi, baada ya kuharamishwa, huyo amejihatarisha kupata mateso ya Mwenyezi Mungu. Na Mwenyezi Mungu ni Mwenye nguvu katika mamlaka Yake, na miongoni mwa enzi Yake ni kuwa Yeye atamtesa anayemuasi Akitaka, hakuna chenye kumzuia kufanya hivyo.
阿拉伯语经注:
 
含义的翻译 段: (95) 章: 玛仪戴
章节目录 页码
 
《古兰经》译解 - 斯瓦希里语翻译 - 阿布杜拉·穆罕默德和纳赛尔·海米斯。 - 译解目录

古兰经斯瓦希里文译解,阿布杜拉·穆罕默德·艾布·拜克尔博士和谢赫纳赛尔·哈米斯翻译。

关闭