《古兰经》译解 - 斯瓦希里语翻译 - 阿布杜拉·穆罕默德和纳赛尔·海米斯。 * - 译解目录


含义的翻译 段: (34) 章: 艾奈尔姆
وَلَقَدۡ كُذِّبَتۡ رُسُلٞ مِّن قَبۡلِكَ فَصَبَرُواْ عَلَىٰ مَا كُذِّبُواْ وَأُوذُواْ حَتَّىٰٓ أَتَىٰهُمۡ نَصۡرُنَاۚ وَلَا مُبَدِّلَ لِكَلِمَٰتِ ٱللَّهِۚ وَلَقَدۡ جَآءَكَ مِن نَّبَإِيْ ٱلۡمُرۡسَلِينَ
Hakika makafiri waliwakanusha Mitume kabla yako Aliyowatuma Mwenyezi Mungu, Aliyotukuka, kwa umma wao. Wao waliudhiwa katika kufuata njia Yake na wakasubiri juu ya hilo na wakaendelea katika ulinganizi wao na bidii yao mpaka ikawajia nusura ya Mwenyezi Mungu. Na hakuna mwenye kuyageuza maneno ya Mwenyezi Mungu, nayo ni yale Aliyoyateremsha kwa Nabii Wake Muhammad , rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, yenye ahadi Yake kwamba Atampa ushindi juu ya wanaomfanyia uadui. Na hakika imekujia wewe, ewe Mtume, habari ya Mitume waliokuwa kabla yako na nusura ya Mwenyezi Mungu iliyohakikishika kwao na mateso ya Mwenyezi Mungu na ghadhabu Zake zilizowafikia wenye kuwakanausha. Basi wewe una kiolezo chema na mfano wa kuiga kutoka kwa Mitume waliotangulia. Katika hili pana kumliwaza Mtume , rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie,.
阿拉伯语经注:
 
含义的翻译 段: (34) 章: 艾奈尔姆
章节目录 页码
 
《古兰经》译解 - 斯瓦希里语翻译 - 阿布杜拉·穆罕默德和纳赛尔·海米斯。 - 译解目录

古兰经斯瓦希里文译解,阿布杜拉·穆罕默德·艾布·拜克尔博士和谢赫纳赛尔·哈米斯翻译。

关闭