《古兰经》译解 - 斯瓦希里语翻译 - 阿布杜拉·穆罕默德和纳赛尔·海米斯。 * - 译解目录


含义的翻译 段: (70) 章: 艾奈尔姆
وَذَرِ ٱلَّذِينَ ٱتَّخَذُواْ دِينَهُمۡ لَعِبٗا وَلَهۡوٗا وَغَرَّتۡهُمُ ٱلۡحَيَوٰةُ ٱلدُّنۡيَاۚ وَذَكِّرۡ بِهِۦٓ أَن تُبۡسَلَ نَفۡسُۢ بِمَا كَسَبَتۡ لَيۡسَ لَهَا مِن دُونِ ٱللَّهِ وَلِيّٞ وَلَا شَفِيعٞ وَإِن تَعۡدِلۡ كُلَّ عَدۡلٖ لَّا يُؤۡخَذۡ مِنۡهَآۗ أُوْلَٰٓئِكَ ٱلَّذِينَ أُبۡسِلُواْ بِمَا كَسَبُواْۖ لَهُمۡ شَرَابٞ مِّنۡ حَمِيمٖ وَعَذَابٌ أَلِيمُۢ بِمَا كَانُواْ يَكۡفُرُونَ
Na waache, ewe Mtume, hawa washirikina ambao wameifanya dini ya Uislamu ni mchezo na pumbao, wazifanyia shere aya za Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka, na yamewaghuri wao maisha ya kilimwengu pamoja na pambo lake. Na wakumbushe, kwa Qur’ani, hawa washirikina na wengineo, ili nafsi isifungike kwa madhambi yake na kumkanusha kwake Mola wake. Haina, isipokuwa Mwenyezi Mungu, mlinzi mwenye kuinusuru akaiokoa na adhabu Yake, wala muombezi mwenye kuiyombea mbele Yake. Na ikitoa ili kujikomboa kiwango kiwacho cha fidia haitakubaliwa kwake. Hao ndio ambao wamefungika na dhambi zao. Watakuwa na kinywaji moto sana na adhabu yenye kuumiza Motoni, kwa sababu ya kumkanusha kwao Mwnyezi Mungu, Aliyetukuka, Mtume Wake, Muhammad, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, na dini ya Uislamu.
阿拉伯语经注:
 
含义的翻译 段: (70) 章: 艾奈尔姆
章节目录 页码
 
《古兰经》译解 - 斯瓦希里语翻译 - 阿布杜拉·穆罕默德和纳赛尔·海米斯。 - 译解目录

古兰经斯瓦希里文译解,阿布杜拉·穆罕默德·艾布·拜克尔博士和谢赫纳赛尔·哈米斯翻译。

关闭