《古兰经》译解 - 斯瓦希里语翻译-阿里·穆哈森·伯瓦尼 * - 译解目录

XML CSV Excel API
Please review the Terms and Policies

含义的翻译 段: (82) 章: 开海菲
وَأَمَّا ٱلۡجِدَارُ فَكَانَ لِغُلَٰمَيۡنِ يَتِيمَيۡنِ فِي ٱلۡمَدِينَةِ وَكَانَ تَحۡتَهُۥ كَنزٞ لَّهُمَا وَكَانَ أَبُوهُمَا صَٰلِحٗا فَأَرَادَ رَبُّكَ أَن يَبۡلُغَآ أَشُدَّهُمَا وَيَسۡتَخۡرِجَا كَنزَهُمَا رَحۡمَةٗ مِّن رَّبِّكَۚ وَمَا فَعَلۡتُهُۥ عَنۡ أَمۡرِيۚ ذَٰلِكَ تَأۡوِيلُ مَا لَمۡ تَسۡطِع عَّلَيۡهِ صَبۡرٗا
Na ama ukuta, huo ulikuwa ni wa vijana wawili mayatima kule mjini. Na chini yake ilikuwako khazina yao; na baba yao alikuwa ni mtu mwema. Basi Mola wako Mlezi alitaka wafikie utu uzima na wajitolee khazina yao wenyewe, kuwa ni rehema itokayo kwa Mola wako Mlezi. Wala mimi sikutenda hayo kwa amri yangu. Hiyo ndiyo tafsiri ya hayo ambayo wewe hukuweza kuyasubiria.
Ama ule ukuta nilio usimamisha, bila ya ujira, ulikuwa wa vijana wawili mayatima katika watu wa ule mji. Na chini yake ilikuwako khazina walio achiwa na baba yao. Naye alikuwa ni mtu mwema. Basi Mwenyezi Mungu alitaka kuwahifadhia khazina yao ile mpaka wakue wawe na akili zao, na wajitolee wenyewe khazina yao kuwa ni rehema kwao, na kumtukuza baba yao kwa kupitia dhuriya zake. Nami sikufanya niliyo yafanya kwa jitahada ya nafsi yangu. Bali nimefanya hayo kwa kuongozwa na Mwenyezi Mungu. Hii ni tafsiri ya hayo yaliyo fichikana kwako wewe Musa, nawe usiweze kuyavumilia.
阿拉伯语经注:
 
含义的翻译 段: (82) 章: 开海菲
章节目录 页码
 
《古兰经》译解 - 斯瓦希里语翻译-阿里·穆哈森·伯瓦尼 - 译解目录

古兰经斯瓦希里语译解,阿里·穆哈森·伯瓦尼翻译

关闭