Na mti utokao katika mlima wa Sinai, unatoa mafuta na kuwa kitoweo kwa walao.
Na tumekuumbieni mti wa zaituni unao ota katika jimbo la Mlima wa Sinai. Katika matunda yake yanapatikana mafuta yanayo kufaeni. Na hizo zaituni ni kitoweo cha chakula kwa wanao kula. "Na mti utokao katika mlima wa Sinai, unatoa mafuta na kuwa kitoweo kwa walao." Aya hii tukufu inathibitisha kuwa mti wa zaituni ni miongoni mwa neema alizo mneemesha Mwenyezi Mungu binaadamu na ambazo baadhi yake zimetajwa katika Aya zilizo tangulia. Na la kuongeza kwenye Aya hii ni kuwa mzaituni ni miongoni mwa miti ya mbao inayo ishi muda mrefu sana, zaidi ya mamia ya miaka. Kwa hivyo hauhitajii juhudi kubwa kwa mtu, bali huendelea kuzaa wenyewe mfululizo. Kadhaalika una sifa ya kuwa daima kijani, unapendeza kuutazama. Uchunguzi wa kisayansi unaonyesha kwamba zaituni ni katika chakula kizuri. Kwani ndani yake imo Protein nyingi. Vile vile zimo chumvi za Calcium, chuma na Phospohorous. Na hivi ni muhimu na vya kutegemewa katika chakula cha binaadamu. Na juu ya hivyo zaituni inayo Vitamin A na Vitamin B. Na kutokana na tunda lake hutolewa mafuta ya zaituni, ambayo ni mafuta bora ya mafuta mepesi. Mafuta haya hutumiwa katika chakula. Uchunguzi wa kitabibu unaongeza kusema kuwa zipo faida nyengine katika mafuta ya zaituni, nazo ni kuwa zinasaidia kwa jumla katika viungo vya usagaji wa chakula, na khasa maini. Nayo yanashinda ubora mafuta yote yanayo tokana na mimea na wanyama, kwa kuwa hayasabibishi maradhi ya mishipa ya damu kama mafuta mengineyo, na kadhaalika yanalainisha ngozi. Na mafuta ya zaituni yana matumizi mengine mengi katika sanaa (ufundi), kwani yanatumiwa katika kufanya sabuni nzuri kabisa, na vitu vinginevyo katika ufanyaji wa vyakula na vitu vya sanaa.
Contents of the translations can be downloaded and re-published, with the following terms and conditions:
1. No modification, addition, or deletion of the content.
2. Clearly referring to the publisher and the source (QuranEnc.com).
3. Mentioning the version number when re-publishing the translation.
4. Keeping the transcript information inside the document.
5. Notifying the source (QuranEnc.com) of any note on the translation.
6. Updating the translation according to the latest version issued from the source (QuranEnc.com).
7. Inappropriate advertisements must not be included when displaying translations of the meanings of the Noble Quran.
搜索结果:
API specs
Endpoints:
Sura translation
GET / https://quranenc.com/api/v1/translation/sura/{translation_key}/{sura_number} description: get the specified translation (by its translation_key) for the speicified sura (by its number)
Parameters: translation_key: (the key of the currently selected translation) sura_number: [1-114] (Sura number in the mosshaf which should be between 1 and 114)
Returns:
json object containing array of objects, each object contains the "sura", "aya", "translation" and "footnotes".
GET / https://quranenc.com/api/v1/translation/aya/{translation_key}/{sura_number}/{aya_number} description: get the specified translation (by its translation_key) for the speicified aya (by its number sura_number and aya_number)
Parameters: translation_key: (the key of the currently selected translation) sura_number: [1-114] (Sura number in the mosshaf which should be between 1 and 114) aya_number: [1-...] (Aya number in the sura)
Returns:
json object containing the "sura", "aya", "translation" and "footnotes".