《古兰经》译解 - 斯瓦希里语翻译-阿里·穆哈森·伯瓦尼 * - 译解目录

XML CSV Excel API
Please review the Terms and Policies

含义的翻译 段: (119) 章: 尼萨仪
وَلَأُضِلَّنَّهُمۡ وَلَأُمَنِّيَنَّهُمۡ وَلَأٓمُرَنَّهُمۡ فَلَيُبَتِّكُنَّ ءَاذَانَ ٱلۡأَنۡعَٰمِ وَلَأٓمُرَنَّهُمۡ فَلَيُغَيِّرُنَّ خَلۡقَ ٱللَّهِۚ وَمَن يَتَّخِذِ ٱلشَّيۡطَٰنَ وَلِيّٗا مِّن دُونِ ٱللَّهِ فَقَدۡ خَسِرَ خُسۡرَانٗا مُّبِينٗا
Na hakika nitawapoteza na nitawatia matamanio, na nitawaamrisha, basi watakata masikio ya wanyama, na nitawaamrisha, basi watabadili aliyo umba Mwenyezi Mungu. Na mwenye kumfanya Shet'ani kuwa ni mlinzi wake badala ya Mwenyezi Mungu, basi huyo amekhasiri khasara ya dhaahiri.
Hakika kiapo chake Shetani ni kuwa atawapoteza wale anao wapumbaza kwa kuwatenga mbali na Haki, na kuchochea pumbao lao na matamanio yao, mpaka wakawa wamepotea wanatanga tanga katika mawazo na tamaa za uwongo. Wakisha kuwa katika kuzainiwa huku na tamaa hizo chini ya utawala wake Shetani, tena huwatokomeza kwenye mambo yasiyo ingia akilini, na huwapelekea hao wafikiri kufanya hayo ni ibada. Na ilhali haya yote ni mawazo ya uwongo tu. Basi huwatia wasiwasi wakatenda mambo, kama kwa mfano kuwakata masikio baadhi ya ngamia wao, wageuze khulka aliyo iumba Mwenyezi Mungu. Wakafanya kuwa ngamia aliye katwa masikio yake hachinjwi, wala hafanyishwi kazi, wala hazuiliwi kwenda machungani atakavyo. Yote haya ni kwa amri yake Shetani kuwazaini. Tena huwatia wasiwasi mpaka wakaona kuwa hayo ni katika dini. Na hakika wao inakuwa wanamfuata yeye Shetani, na wanamfanya yeye ndiye wa kuwanusuru, na ndiye wa kumfuata badala ya Mwenyezi Mungu. Na mwenye kumfanya Shetani ndiye msaidizi wake wa kumfuata, basi amekhasiri khasara kubwa iliyo wazi. Kwani hapo anakuwa amepotea njia ya Haki, na ameipumbaza akili yake, na utampata ufisadi duniani, na adhabu Akhera.
阿拉伯语经注:
 
含义的翻译 段: (119) 章: 尼萨仪
章节目录 页码
 
《古兰经》译解 - 斯瓦希里语翻译-阿里·穆哈森·伯瓦尼 - 译解目录

古兰经斯瓦希里语译解,阿里·穆哈森·伯瓦尼翻译

关闭