《古兰经》译解 - 斯瓦希里语翻译-阿里·穆哈森·伯瓦尼 * - 译解目录

XML CSV Excel API
Please review the Terms and Policies

含义的翻译 段: (36) 章: 尼萨仪
۞ وَٱعۡبُدُواْ ٱللَّهَ وَلَا تُشۡرِكُواْ بِهِۦ شَيۡـٔٗاۖ وَبِٱلۡوَٰلِدَيۡنِ إِحۡسَٰنٗا وَبِذِي ٱلۡقُرۡبَىٰ وَٱلۡيَتَٰمَىٰ وَٱلۡمَسَٰكِينِ وَٱلۡجَارِ ذِي ٱلۡقُرۡبَىٰ وَٱلۡجَارِ ٱلۡجُنُبِ وَٱلصَّاحِبِ بِٱلۡجَنۢبِ وَٱبۡنِ ٱلسَّبِيلِ وَمَا مَلَكَتۡ أَيۡمَٰنُكُمۡۗ إِنَّ ٱللَّهَ لَا يُحِبُّ مَن كَانَ مُخۡتَالٗا فَخُورًا
Muabuduni Mwenyezi Mungu wala msimshirikishe na chochote. Na wafanyieni wema wazazi wawili na jamaa na mayatima na masikini na jirani wa karibu na jirani wa mbali, na rafiki wa ubavuni na mpita njia, na walio milikiwa na mikono yenu ya kulia. Hakika Mwenyezi Mungu hawapendi wenye kiburi wanao jifakhiri,
Nanyi muabuduni Mwenyezi Mungu peke yake, wala msimfanyie washirika katika Ungu na kuabudiwa. Na watendeeni wema wazazi wenu bila ya taksiri yoyote, na pia jamaa zenu, na mayatima, na walio fakirika kwa sababu ya kuemewa au kupata masaibu katika mali yao, na jirani mliye karibiana naye kwa nasaba, na jirani mtu mbali, na mwenzio katika kazi au njia au majlisi, na msafiri mhitaji asiye kuwa na kituo katika nchi maalumu, na watumwa wenu wanaume na wanawake mlio wamiliki. Hakika Mwenyezi Mungu hampendi anaye jipa ubora juu ya watu wengine, na hawachukulii watu kwa huruma, na anakithirisha kujisifu mwenyewe kwa kujifakhiri.
阿拉伯语经注:
 
含义的翻译 段: (36) 章: 尼萨仪
章节目录 页码
 
《古兰经》译解 - 斯瓦希里语翻译-阿里·穆哈森·伯瓦尼 - 译解目录

古兰经斯瓦希里语译解,阿里·穆哈森·伯瓦尼翻译

关闭