《古兰经》译解 - 斯瓦希里语翻译-阿里·穆哈森·伯瓦尼 * - 译解目录

XML CSV Excel API
Please review the Terms and Policies

含义的翻译 段: (88) 章: 尼萨仪
۞ فَمَا لَكُمۡ فِي ٱلۡمُنَٰفِقِينَ فِئَتَيۡنِ وَٱللَّهُ أَرۡكَسَهُم بِمَا كَسَبُوٓاْۚ أَتُرِيدُونَ أَن تَهۡدُواْ مَنۡ أَضَلَّ ٱللَّهُۖ وَمَن يُضۡلِلِ ٱللَّهُ فَلَن تَجِدَ لَهُۥ سَبِيلٗا
Mmekuwaje kuwa makundi mawili kwa khabari ya wanaafiki, na hali Mwenyezi Mungu amewageuza kwa sababu ya yale waliyo yachuma? Je! Mnataka kumwona mwongofu ambaye Mwenyezi Mungu amemhukumu kuwa kapotea? Na aliye mhukumu Mwenyezi Mungu kuwa amekwisha potea wewe hutampatia njia.
Haikufaliini, enyi Waumini, kukhitalifiana katika mas-ala yaliyo khusu wanaafiki, ambao wanadhihirisha Uislamu na wanaficha ukafiri. Haikufaliini kukhitalifiana kwa mas-ala yao, kuwa ati wao ni Waumini au makafiri? Wauwawe au waachiliwe? Je, wameelekea kuongoka au hawatarajiwi uwongofu? Fahamu zao zimegeuzwa kwa yaliyo chumwa na vitendo vyao. Shari imekuwa ndio inayo wahukumu, basi usimtarajie kuongoka yule ambaye Mwenyezi Mungu kwa ujuzi wake wa tangu na tangu kesha mkadiria asiongoke. Kwani aliye andikwa katika ujuzi wa Mwenyezi Mungu wa tangu azali kuwa ni mwenye kupotea basi huna njia ya kumwongoa.
阿拉伯语经注:
 
含义的翻译 段: (88) 章: 尼萨仪
章节目录 页码
 
《古兰经》译解 - 斯瓦希里语翻译-阿里·穆哈森·伯瓦尼 - 译解目录

古兰经斯瓦希里语译解,阿里·穆哈森·伯瓦尼翻译

关闭