Na kwa hakika yeye ni alama ya Saa ya Kiyama. Basi usiitilie shaka, na nifuateni. Hii ndiyo Njia Iliyo Nyooka.
Na hakika Isa kwa kuzuka kwake bila ya baba, na kuponyesha kwake vipofu na wakoma ni dalili ya kukaribia Saa ya Kiyama. Basi usiwe na shaka nayo. Na fuateni uwongofu wangu na Mtume wangu. Hii ninayo kuitieni ndiyo Njia Iliyo Nyooka yenye kufikilia Uwokovu.
Na alipo kuja Isa na dalili zilizo wazi, alisema: Nimekujieni na hikima, na ili nikuelezeni baadhi ya yale mliyo khitalifiana. Basi mcheni Mwenyezi Mungu, na mnit'ii mimi.
Na alipo tumwa Isa kwa Wana wa Israili naye ana miujiza iliyo wazi, na Ishara zenye kubainisha, aliwaambia: Nimekujieni na sharia yenye hikima nzuri, inayo kuiteni muifuate Tawhidi (Imani ya Mwenyezi Mungu Mmoja). Na nimekujieni nikubainishieni baadhi ya mambo mnayo khitalifiana kwayo katika mambo ya Dini ili mpatane kwenye Haki. Basi iogopeni adhabu ya Mwenyezi Mungu, na mnit'ii mimi katika hayo ninayo kuitieni.
Kwa hakika Mwenyezi Mungu ni Mola wangu Mlezi, na ni Mola wenu Mlezi. Basi Muabuduni Yeye tu. Hii ndiyo Njia Iliyo Nyooka.
Hakika Mwenyezi Mungu, peke yake, ndiye Muumba wangu, na ni Muumba wenu, basi muabuduni Yeye pasi mwenginewe. Na ihafidhini sharia yake. Hii ninayo kuitieni muifuate ni Njia Iliyo Nyooka itakayo kufikisheni kwenye uwokovu.
Lakini makundi kwa makundi yao yalikhitalifiana wao kwa wao. Ole wao walio dhulumu kwa adhabu ya siku chungu.
Makundi mbali mbali yakakhitalifiana baina ya Wakristo baada ya Isa, kwa kufarikiana juu yake. Maangamizo yatawafika hao walio dhulumu kwa waliyo yasema juu ya Isa ya ukafiri, watapata adhabu kali na chungu Siku ya Kiyama.
Siku hiyo marafiki watakuwa ni maadui, wao kwa wao, isipo kuwa wachamngu.
Marafiki walio kusanyika duniani kwa upotovu, watakuwa maadui wao kwa wao siku itakapo wafikia Saa kwa ghafla, na yatakatika mapenzi yote, ila mapenzi ya wenye kuogopa, nao wangali duniani, kuiogopa adhabu ya Mwenyezi Mungu, na wakashikamana huko duniani katika kumt'ii Yeye.
Enyi waja wangu! Hamtakuwa na khofu siku hiyo, wala hamtahuzunika.
Mwenyezi Mungu atawaambia wachamngu kwa kuwafanyia hishima: Enyi waja wangu! Leo msikhofu adhabu yoyote, wala msihuzunike. Mmekwisha salimika na adhabu. Na Mwenyezi Mungu amekudhaminieni thawabu.
Ingieni Peponi, nyinyi na wake zenu; mtafurahishwa humo.
Siku ya Kiyama wataambiwa kwa kufanyiwa hishima: Ingieni Peponi, nyinyi na wake zenu, nanyi mmo katika furaha iliyo kubwa, ambayo itadhihiri kwenye nyuso zenu.
Watakuwa wanapitishiwa sahani za dhahabu na vikombe; na vitakuwamo ambavyo nafsi zinavipenda na macho yanavifurahia, na nyinyi mtakaa humo milele.
Na baada ya kuingia Peponi watakuwa wakizungukiwa kwa sahani za dhahabu, na bilauri kadhaalika, na humo watapata vyakula namna mbali mbali, na vinywaji vya kila namna. Na humo Peponi watapata kila kitamaniacho moyo, na kituzacho macho. Na kukamilisha furaha wataambiwa: Nyinyi mtakaa milele katika neema hizi.
Contents of the translations can be downloaded and re-published, with the following terms and conditions:
1. No modification, addition, or deletion of the content.
2. Clearly referring to the publisher and the source (QuranEnc.com).
3. Mentioning the version number when re-publishing the translation.
4. Keeping the transcript information inside the document.
5. Notifying the source (QuranEnc.com) of any note on the translation.
6. Updating the translation according to the latest version issued from the source (QuranEnc.com).
7. Inappropriate advertisements must not be included when displaying translations of the meanings of the Noble Quran.
搜索结果:
API specs
Endpoints:
Sura translation
GET / https://quranenc.com/api/v1/translation/sura/{translation_key}/{sura_number} description: get the specified translation (by its translation_key) for the speicified sura (by its number)
Parameters: translation_key: (the key of the currently selected translation) sura_number: [1-114] (Sura number in the mosshaf which should be between 1 and 114)
Returns:
json object containing array of objects, each object contains the "sura", "aya", "translation" and "footnotes".
GET / https://quranenc.com/api/v1/translation/aya/{translation_key}/{sura_number}/{aya_number} description: get the specified translation (by its translation_key) for the speicified aya (by its number sura_number and aya_number)
Parameters: translation_key: (the key of the currently selected translation) sura_number: [1-114] (Sura number in the mosshaf which should be between 1 and 114) aya_number: [1-...] (Aya number in the sura)
Returns:
json object containing the "sura", "aya", "translation" and "footnotes".