《古兰经》译解 - 斯瓦希里语翻译-阿里·穆哈森·伯瓦尼 * - 译解目录

XML CSV Excel API
Please review the Terms and Policies

含义的翻译 段: (116) 章: 玛仪戴
وَإِذۡ قَالَ ٱللَّهُ يَٰعِيسَى ٱبۡنَ مَرۡيَمَ ءَأَنتَ قُلۡتَ لِلنَّاسِ ٱتَّخِذُونِي وَأُمِّيَ إِلَٰهَيۡنِ مِن دُونِ ٱللَّهِۖ قَالَ سُبۡحَٰنَكَ مَا يَكُونُ لِيٓ أَنۡ أَقُولَ مَا لَيۡسَ لِي بِحَقٍّۚ إِن كُنتُ قُلۡتُهُۥ فَقَدۡ عَلِمۡتَهُۥۚ تَعۡلَمُ مَا فِي نَفۡسِي وَلَآ أَعۡلَمُ مَا فِي نَفۡسِكَۚ إِنَّكَ أَنتَ عَلَّٰمُ ٱلۡغُيُوبِ
Na pale Mwenyezi Mungu atakapo sema: Ewe Isa bin Maryamu! Ati wewe uliwaambia watu: Nifanyeni mimi na mama yangu kuwa ni miungu badala ya Mwenyezi Mungu? (Na Isa) atasema: Subhanaka, Wewe umetakasika! Hainifalii mimi kusema ambayo si haki yangu. Ikiwa nilisema basi bila ya shaka umekwisha yajua. Wewe unayajua yaliyo ndani ya nafsi yangu, lakini mimi siyajui yaliyo katika nafsi yako. Hakika Wewe ndiye Mjuzi mkubwa wa yaliyo fichikana.
Ewe Nabii! Taja yatakayo tokea Siku ya Kiyama, Mwenyezi Mungu atapo mwambia Isa bin Maryamu kauli ya kutangaza haki: Ati wewe ndiye uliye waambia: Nifanyeni mimi na mama yangu kuwa ni miungu, na muache kumuabudu Mwenyezi Mungu wa pekee? Isa atasema: Mimi ninakutakasa mtakaso wa ukamilifu ya kuwa Wewe huna mshirika. Wala hainifalii mimi nitake jambo ambalo sina haki nalo hata chembe. Lau kuwa nimesema hayo, basi Wewe ungeli jua. Kwani Wewe unayajua yaliyo fichikana ndani ya nafsi yangu, licha yanayo dhihiri kwa kuyasema. Wala mimi siyajui unayo nificha. Hakika Wewe ndiye Mwenye ujuzi ulio enea kila kilicho fichikana na kilicho ghibu. (Wakristo wote wanamuabudu Yesu, na Wakatoliki wanamwomba Maryamu pia, na wanamwita: "Mama wa Mungu")
阿拉伯语经注:
 
含义的翻译 段: (116) 章: 玛仪戴
章节目录 页码
 
《古兰经》译解 - 斯瓦希里语翻译-阿里·穆哈森·伯瓦尼 - 译解目录

古兰经斯瓦希里语译解,阿里·穆哈森·伯瓦尼翻译

关闭