《古兰经》译解 - 斯瓦希里语翻译-阿里·穆哈森·伯瓦尼 * - 译解目录

XML CSV Excel API
Please review the Terms and Policies

含义的翻译 段: (119) 章: 艾奈尔姆
وَمَا لَكُمۡ أَلَّا تَأۡكُلُواْ مِمَّا ذُكِرَ ٱسۡمُ ٱللَّهِ عَلَيۡهِ وَقَدۡ فَصَّلَ لَكُم مَّا حَرَّمَ عَلَيۡكُمۡ إِلَّا مَا ٱضۡطُرِرۡتُمۡ إِلَيۡهِۗ وَإِنَّ كَثِيرٗا لَّيُضِلُّونَ بِأَهۡوَآئِهِم بِغَيۡرِ عِلۡمٍۚ إِنَّ رَبَّكَ هُوَ أَعۡلَمُ بِٱلۡمُعۡتَدِينَ
Na kwa nini msile katika walio somewa jina la Mwenyezi Mungu, naye amekwisha kubainishieni alivyo kuharimishieni, isipo kuwa vile mnavyo lazimishwa? Na hakika wengi wanapoteza kwa matamanio yao bila ya kuwa na ilimu. Hakika Mola wako Mlezi ndiye Mjuzi kushinda wote kuwajua wanao pindukia mipaka.
Na hakika hapana sababu yoyote au dalili ya kukuzuieni kula nyama aliye tajiwa jina la Mwenyezi Mungu Mtukufu juu yake wakati wa kuchinja miongoni mwa nyama hoa. (yaani nyama wa kufuga.) Na Mwenyezi Mungu Aliye takasika na Aliye tukuka amekwisha kubainishieni vilio harimishwa, katika hali isiyo kuwa ya dharura, kama mzoga na damu (na nguruwe). Watu wengi wanaacha Haki, si kwa lolote, ila kufuata pumbao la nafsi zao tu, bila ya kuwa wamepewa ilimu, au hoja iliyo thibiti kwao. Kama hao Waarabu walio jiharimishia wenyewe baadhi ya wanyama wa kufuga. Wala nyinyi hamna makosa kwa kula kilicho zaliwa, bali wao ndio wamepita mipaka kwa kuharimisha kilicho halali. Na Mwenyezi Mungu peke yake ndiye Mjuzi wa hao walio pindukia mipaka kwa ujuzi usio na mfano wake kwa hakika.
阿拉伯语经注:
 
含义的翻译 段: (119) 章: 艾奈尔姆
章节目录 页码
 
《古兰经》译解 - 斯瓦希里语翻译-阿里·穆哈森·伯瓦尼 - 译解目录

古兰经斯瓦希里语译解,阿里·穆哈森·伯瓦尼翻译

关闭