《古兰经》译解 - 斯瓦希里语翻译-阿里·穆哈森·伯瓦尼 * - 译解目录

XML CSV Excel API
Please review the Terms and Policies

含义的翻译 段: (124) 章: 艾奈尔姆
وَإِذَا جَآءَتۡهُمۡ ءَايَةٞ قَالُواْ لَن نُّؤۡمِنَ حَتَّىٰ نُؤۡتَىٰ مِثۡلَ مَآ أُوتِيَ رُسُلُ ٱللَّهِۘ ٱللَّهُ أَعۡلَمُ حَيۡثُ يَجۡعَلُ رِسَالَتَهُۥۗ سَيُصِيبُ ٱلَّذِينَ أَجۡرَمُواْ صَغَارٌ عِندَ ٱللَّهِ وَعَذَابٞ شَدِيدُۢ بِمَا كَانُواْ يَمۡكُرُونَ
Na inapo wajia Ishara, wao husema: Hatutoamini mpaka tupewe mfano wa walio pewa Mitume wa Mwenyezi Mungu. Mwenyezi Mungu ndiye Mjuzi kuliko wote kujua wapi anaweka ujumbe wake. Itawafikia hao walio kosa udhalili na adhabu kali kutoka kwa Mwenyezi Mungu kwa sababu ya vitimbi walivyo kuwa wakivifanya.
Hakika hawa wakuu wa wakosefu huwahusudu watu walio pewa na Mwenyezi Mungu ilimu, na Unabii, na uwongofu. Basi ikiwajia hoja ya kukata hawaikubali, lakini husema: Hatuikubali Haki mpaka tuteremshiwe wahyi kama wanavyo teremshiwa Mitume. Na hali ni Mwenyezi Mungu peke yake ndiye Mwenye ujuzi ambao haulingani na ujuzi wa mtu yoyote, kujua nani anaye stahiki kupata Utume wake. Ni Yeye ndiye anaye teuwa nani katika viumbe vyake ampe Utume wake. Hawa wenye inda, ikiwa wanataka ukubwa kwa inadi ya namna hii, basi watakuja pata unyonge na udhalili hapa duniani kwa sababu hiyo, na kesho Akhera watakuja pata adhabu kali kwa sababu ya huko kupanga kwao uwovu.
阿拉伯语经注:
 
含义的翻译 段: (124) 章: 艾奈尔姆
章节目录 页码
 
《古兰经》译解 - 斯瓦希里语翻译-阿里·穆哈森·伯瓦尼 - 译解目录

古兰经斯瓦希里语译解,阿里·穆哈森·伯瓦尼翻译

关闭