《古兰经》译解 - 斯瓦希里语翻译-阿里·穆哈森·伯瓦尼 * - 译解目录

XML CSV Excel API
Please review the Terms and Policies

含义的翻译 段: (137) 章: 艾奈尔姆
وَكَذَٰلِكَ زَيَّنَ لِكَثِيرٖ مِّنَ ٱلۡمُشۡرِكِينَ قَتۡلَ أَوۡلَٰدِهِمۡ شُرَكَآؤُهُمۡ لِيُرۡدُوهُمۡ وَلِيَلۡبِسُواْ عَلَيۡهِمۡ دِينَهُمۡۖ وَلَوۡ شَآءَ ٱللَّهُ مَا فَعَلُوهُۖ فَذَرۡهُمۡ وَمَا يَفۡتَرُونَ
Na kadhaalika hao washirika wao wamewapambia wengi katika washirikina kuwauwa watoto wao ili kuwaangamiza na kuwavurugia dini yao. Na lau kuwa Mwenyezi Mungu angeli penda wasinge fanya hayo. Basi waache na hayo wanayo yazua.
Kama ilivyo kuwa hayo mawazo yao yalivyo wapambia huo mgawanyo wa dhulma katika mazao ya mimea, na ngamia, na ng'ombe, na kondoo, alio umba Mwenyezi Mungu, basi kadhaalika mawazo yao yamewapambia, kutokana na hayo masanamu ambayo wanadai kuwa ni washirika wa Mwenyezi Mungu, kuwauwa watoto wao pale wanapo zaliwa, na kuwa ati waliweka nadhiri kwa miungu yao kuwachinja watoto wao! Na hakika hayo mawazo yao yanawaangamiza na yanawavurugia mambo ya dini, kwa hivyo hawaielewi vilivyo! Na ilivyo kuwa mawazo yao yamezisaliti akili zao hadi hiyo, basi wewe waachilie mbali wao na hayo wanayo mzulia Mwenyezi Mungu Mtukufu, na kukuzulia wewe. Nao watakuja pata malipo ya huo uzushi wao. Na hayo ndio matakwa ya Mwenyezi Mungu, kwani angeli taka wasingeli fanya hayo.
阿拉伯语经注:
 
含义的翻译 段: (137) 章: 艾奈尔姆
章节目录 页码
 
《古兰经》译解 - 斯瓦希里语翻译-阿里·穆哈森·伯瓦尼 - 译解目录

古兰经斯瓦希里语译解,阿里·穆哈森·伯瓦尼翻译

关闭